Ifahamu Concorde ndege ya abiria aina ya Jet iliyoundwa miaka ya 1950s kwa ushirikiano wa Wahandisi kutoka Ufaransa na Uingereza Pamoja na kuundwa miaka mingi iliyopita lakin mpaka leo bado ni maarufu na ya kustajaabisha. Ilipewa jina la Concorde kwa maana ya Makubaliano au Muungano.
1. Concorde iliruka kwa mara ya kwanza 1969 na ndege hiz zilianza kazi rasmi 1976. Zimefanya kazi miaka 27 mpaka March 10, 2003 zilipo staafu kuruka.
2. Ilikuwa na uwezo wa kubeba Rubani wawili, Mwandisi wa ndege mmoja na wafanyakaz wengine 6 pamoja na abiria kuanzia 92 hadi 128.
3. Concorde ilikuwa na uwezo wa kusafiri kasi ya Supersonic yaani ni kasi zaidi ya kasi ya sauti au Mach 2 yaani mara mbili zaidi ya kasi ya sauti.
4. Concorde ilikuwa na uwezo wa kukimbia kasi ya kilomita 400 kwa saa katika uwanja wa kukimbilia ili ipate nguvu ya kuinuka na kuachia ardhi.
5. Baada ya kuachia ardhi ilikuwa inapanda juu kuelekea katika Altitude ya kusafiria kwa kila sekunde moja mita 60.
6. Ikiwa ardhini au ikiwa inataka kutua ilikuwa na uwezo wa kushusha pua yake ili kuongeza uwezo wa marubani kuona mbele kwa sababu pua yake ilikuwa ndefu sana.
7.Ilikuwa inatua katika uwanja ikiwa na kasi ya kilomita 300 kwa saa.
8. Ilikuwa ikisafiri katika Altitude yake ya kusafiria ambayo ni futi 60,000 kutoka usawa wa bahari au mita 18,000 au kilomita 18 ambapo umbali ule ulikuwa ukitumiwa na Concorde pekee....yani ikiwa katika Altitude hiyo wanakuwa peke yao hakuna ndege zilizokuwa na uwezo wa kufika altitude hiyo.
9. Ikiwa katika Altitude ya kusafiria ilikuwa na uwezo wa kwenda kasi ya kilomita 2180 kwa saa.
10. Concorde ilikuwa inatumia masaa matatu na nusu kutoka London kwenda New York tofauti na ndege zingine ambazo ni masaa 8. Waingereza walijitungia usemi usemao " Arrive before you Leave" yani Wasili/fika kabla hujaondoka. Usemi huu ulitokea kwa sababu ya utofauti wa masaa uliopo kati ya London na New York ambayo ni masaa matano "5" London ikiwa mbele ya New York kwa masaa hayo. Ina maana ukitoka London saa 5 asubuh unafika New York kabla ya saa 5  ya asubuh kwa local time ya hapo. " Arrive before you Leave"  .
11. Kutokana na kasi yake....Pua yake ilikuwa inapata joto hadi kufikia 130c yani ni zaid ya maji yaliyochemka joto lake. Inapokuwa imetua kila eneo la ndege kwa nje lilikuwa ni la moto sana hadi vioo pia.
12. Concorde ikiwa katika kasi ya Supersonic au Mach 2 ....joto lililosababishwa na mkandamizo wa hewa liliifanya ndege kutanuka na kuongezeka urefu kuanzia inch 6 hadi 9.
13. Concorde ilikuwa inatumia lita 22,000 kwa saa moja. Mafuta mengi zaid yalitumika ikiwa katika kasi ya Subsonic ambayo ni kasi inayotumiwa na ndege za kawaida au ikiwa inatoka katika gate kwenda kwenye Runway. Concorde ilikuwa inabeba tani za mafuta kwenye matenki yake katika mabawa.
14. Concorde ilikuwa na kipimia mionzi ambacho kiliwasaidia Marubani kujua kama mionzi imezidi na kama imezidi walikuwa washusha kidogo ndege kutoka feet 60,000 hadi feet 47,000 au mita 14,000.
15. Abiria waliotumia usafiri wa Concorde walikuwa wa kipato kikubwa. Mfano miaka ya 97 ticket ya round trip ilikuwa ni dola 7995 mtu mmoja sawa na mara 30 ya nauli kwa usafir wa ndege za bei ya chini katika route hiyo.
16. Katika miaka yote iliyofanya kazi Shirika hilo la Concorde ni ndege moja pekee ndio iliyopata ajali ikiwa inatokea Paris kuelekea New York. Ikiwa katika uwanja wa kukimbilia Concorde ilikanyaga kipande cha bati gumu lililotoka kwa bahati mbaya katika ndege iliyokuwa mbele yake...yani ndege iliyoitangulia Concorde kuruka.
Kipande kilipelekea Concorde kupata pancha tairi za nyuma upande wa kushoto kisha tairi hiyo kurusha kipande cha chuma kwa kasi kuelekea katika tank za mafuta na kusababisha mlipuko. Sekunde chache baadae Rubani walipoteza udhibiti wa ndege hiyo baada ya kuruka na iliishia kuanguka karibu na hotel killing everyone on board and four people on the ground.
Waliuawa abiria 100, Marubani na wahudumu pamoja na watu wanne waliokuwa karibu na eneo la ajali.
17. Concorde iliruka kwa mara ya mwisho March 10, 2003 ikiwa na Marubani pamoja na wahandisi tu. Huo ndio ukawa mwisho wa Concorde hadi leo hii zikiwa zimebakia kama makumbusho tu.
Umeshawahi kusikia mtu anaambiwa " we ushakuwa konkodi wa kitu fulani au ushakuwa konkodi we mtoto hutaki kusikia"
Bado haijatokea ndege ya abiria kama Concorde hadi leo hii.