Ifahamu ACT-Tanzania/Wazalendo

Ifahamu ACT-Tanzania/Wazalendo

Hamjambo wanaJF.............Kwa wale na wanachama wa chama cha MABADILIKO na UWAZI(ACT-Wazalendo) Tusemezane hapa...............

UTANGULIZI
Anna+picha.jpg


Kuhusu ACT

Itikadi

ACT-Tanzania ni chama cha siasa nchini Tanzania kinachoamini katika misingi ya Ujamaa Demokrasia (Democratic Socialism).

Misingi mikuu ya ujamaa wa kidemokrasia ni undugu, usawa, uhuru, heshima kwa kila mtu na demokrasia.

ACT-Tanzania inatambua kuwa sisi wananchi wa Tanzania ndiyo raslimali kubwa ya nchi, na kwamba nchi yetu imejaliwa raslimali nyingi ambazo zikivunwa na kutumika vizuri

zinaweza kuboresha maisha na kuchangia katika maendeleo ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Hivyo basi, shabaha kuu ya ACT-Tanzania ni kuhakikisha kuwa utajiri wa nchi unatumika kuboresha maisha ya watu na kuchochea uwezo wao katika kuchangia kujenga

uchumi shirikishi ambapo kila mtu ana fursa sawa za maendeleo.

Ngao za Ujamaa wa Kidemokrasia

Ngao tatu za Ujamaa wa kidemokrasia (Democratic Socialism) kwa mujibu wa ACT-Wazalendo ni:

I) Undugu ni hifadhi ya jamii ya asili kwa Afrika, na hivyo kila mtanzania na kila mwafrika ana jukumu la kumsaidia mwenzake anayekabiliwa na tatizo au janga popote alipo

bila kutarajia malipo ya aina yeyote

II) Serikali ina haki na wajibu wa kutengeneza sheria na kanuni zenye kulenga kuleta usawa wa kibinadamu katika jamii. Aidha, Serikali ina haki na wajibu wa kusimamia

moja kwa moja sekta nyeti katika jamii zenye maslahi mapana ya kiusalama na kiuchumi kwa nchi

III) Viongozi na watumishi wa umma wana wajibu wa kuhakikisha kwamba wanaishi na kuenenda katika misingi inayalinda heshima ya ofisi za umma na kwamba hawatumii

nafasi zao kwa manufaa yao binafsi na jamaa zao.

Ili kuwasaidia na kuwawezesha viongozi na watumishi wa umma kuenenda katika misingi ya uadilifu, kuna haja ya kuwekewa miiko na maadili maalumu ya viongozi

Falsafa

Falsafa ya ACT Tanzania ni UNYERERE, ikiwa ni dhamira ya kurudisha, kuhuisha na kupigania misingi mama iliyoasisi Taifa la Tanzania, kama ilivyoanishwa katika Azimio la

Arusha na kwa mazingira ya Tanzania ya sasa.


A) Bendera ya Chama yenye rangi ya Zambarau, ambayo ndio alama kuu ya Chama. Rangi hii inawakilisha taswira ya mchanganyiko wa wanachama kutoka kona na pembe

zote za nchi; utambuzi wa umuhimu wa wanawake na familia katika jamii; na alama ya kujali makundi yenye mahitaji maalum katika jamii wakiwemo watu wenye ulemavu,

watoto na wazee.

B) Bendera ya Taifa ikiashiria uzalendo, upendo na utayari wa kulilinda na kulitumikia Taifa la Tanzania.

C) Mkono uliofunguka ukiashiria Uwazi.
 
Back
Top Bottom