Wakati mwingi sio usaliti kama wengi mnavyochukulia,ni maudhi madogo madogo ambayo huwa hayavumiliki kirahisi,nadhani kama uko kwenye ndoa utakuwa unanielewa nazungumzia kitu gani.Usaliti mnaanzaga nyie wakimalizia wanawake ndo wanaonekana wabaya
usiache mke wako wa ndoa,Imenitokea ghafla sana kila nikikumbuka matendo yake mabaya kwangu nashindwa kumsamehe na ninamchukia kupita maelezo. Kifupi hata nikimuona hasira inanipanda na hata mawasiliano naye sitaki. Hua napenda kua mbali na watu na kukaa alone tu. Nimebadilika sana mpaka marafiki wananishangaa kua nimepoa mno na sionekani. Ila ukweli ni kua nimeumizwa moyo mpaka basi. Sitaki kujua habari zake na sitaki ajue zangu. Mpka sasa hua nasafiri safari nyingi but hawezi jua nipo wapi na nafanya nini.
Nimekua na relationships na wasichana wengi mpaka kichwa kinauma ila sio serious relationships just for chating. Ila wao wanajua niko serious but ukweli kua niko frustrated. Nimeamua kuaachana nao but mmoja ndio ananiumiza kichwa maana yuko serious kupita maelezo. Hta jinsi ya kumuambia kua niko married nashindwa kupata pa kuanzia. Ki ukweli niko confused sana na sioni faida ya kuoa. Nimekua kwenye shida for a long time na nahisi nikiwa single nitakua na uhuru. Sijajua nifanyeje ila nko bored balaaa na haya maisha ya ndoa. Ndoa ya moto balaaa mpka hamu ya kuishi inapotea. Nashindwa kufikiria kurepair my relationship kitu nachofikiria ni divorce tu. Kwa sasa nimeamua kua kimya na kuishi alone kwanza nisome mchezo unaendaje but majaribu nayo ndio yanazidi kwani naposafiri nakua tempted sana.
Hili ndio swala la msing what made you be angry at her huo ndio mwanzo wa yote mengne yote ni matokeo tuEbu tuambie mkeo kakufanya nini kwanza mpk umchukie ivyo kingine ao wanawake zako usiwafiche kuhusu kuoa uwa mnaona aibu au
Ila mm naona kama huo ni utoto na ulimbukeni wala sio ujanja
Mkuu hapa nimejifunza kituIla mm naona kama huo ni utoto na ulimbukeni wala sio ujanja
Nimesoma upesi upesi na nikaamua niisome tena kwa ukimya mzuri nikagundua mawili au matatu yafuatayo;
Hao wanawake unaowadanganya nao watakuja kuumia siku moja wakiujua ukweli, kwahio na wewe jiweke kwenye nafasi yao. Kumbuka kuna ujana na kuna utu uzima. Huwezi kuwa mtu mzima kisha ukaishi maisha ya ujana....utapotea.
- Una tatizo la kutojiamini, huamini kama umeoa, huamini kuwa uan familia bado unaamini kwenye ujana
- Una asili ya ubinafsi kwahio inakuapa shida sana ku-share na wengine, mkeo ndio mtu wako wa ku-share naye mambo mengi sijasema mambo yote nimesema mambo mengi.
- una kiburi na kujikweza, hutaki kushindwa, hutaki kuelewa, ndio yako ndio NDIO na hapana yako ndio Hapana, misimamo ya style hii haiwezi kamwe kukupa amani
- Umejiingiza kwenye mahusiano mengine kwa kisingizio cha kutendwa vibaya na mkeo, japo umeshindwa kusema kosa lako at least kwa ujumla wake tu
- Hauko tayari kushaurika, hivyo utapotea zaidi badala ya kufanikiwa.
- Wanawake wengi watakuumiza zaidi na hakuna atakayekupa faraja.
The way forward; jifunze kujishusha, jifunze kuzungungumza, jifunze communication skills, soma maandiko mbali mbali jinsi ya kupunguza hasira na kiburi. Jichanganye na usitake kujiona wa maaana kuliko wengine, Brother, utaishi kwa amani tele out of that ujue kisukari, cancer, presha na mengineyo yanakusubiri. Pole, njoo inbox
Asante nashukuruMkuu hapa nimejifunza kitu
Mwingine kule katimua.pole
naona ndio msimu wake huu