Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Yaani kuna lijimama mmoja kazi yake ni kuwawekea vijana wadogo mitego na kuwanasa na kuwafanya wa watelekeze ma-gfs wao.
Kisa ni kuwa ana mrundo wa fedha na vijana wetu ambao wanapenda vya mteremko hutimkia huko. Amewavunja akina dada wengi moyo na kuwasonenesha kwa mapigo yake hayo ya kiutu uzima ya kuwanyang'anya mabwana zao ambao wengine walikuwa kwenye pilika pilika za kufunga pingu za maisha ............
Yaani kweli huu ni uungwana?
Akiulizwa hujigamba eti mwenye nguvu mpishe...........lakini baada ya kuwatumia hawa dogo dogo atakavyo huwatelekeza...........na hachukui kijana asiye na mwenzie hata kidogo.......kwa sababu apenda sana mashindano na masifa..........Tumfanyeje huyo "sugar mummy" maana amekuwa ni balaa hapa mtaani kwangu........................
Kisa ni kuwa ana mrundo wa fedha na vijana wetu ambao wanapenda vya mteremko hutimkia huko. Amewavunja akina dada wengi moyo na kuwasonenesha kwa mapigo yake hayo ya kiutu uzima ya kuwanyang'anya mabwana zao ambao wengine walikuwa kwenye pilika pilika za kufunga pingu za maisha ............
Yaani kweli huu ni uungwana?
Akiulizwa hujigamba eti mwenye nguvu mpishe...........lakini baada ya kuwatumia hawa dogo dogo atakavyo huwatelekeza...........na hachukui kijana asiye na mwenzie hata kidogo.......kwa sababu apenda sana mashindano na masifa..........Tumfanyeje huyo "sugar mummy" maana amekuwa ni balaa hapa mtaani kwangu........................