Huyu ni mpenzi au bomu la machozi?

Huyu ni mpenzi au bomu la machozi?

Kibirizi

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2011
Posts
604
Reaction score
149
Mimi nina mahusiano na binti mmoja kwa sasa mahusiano yetu yamefikia miaka mitatu. Lakini cha kushangaza kila ninapokutana naye lazima nitoke machozi, yaani lazima atapigiwa simu ambazo zinanikwaza na nikijaribu kudadisha mwisho wa siku lazima nitoke machozi. Pia nikikagua simu yake lazima nitakuta meseji ambazo zitanitoa machozi.
Kwangu huyu amekuwa zaidi ya bomu la machozi sasa nashindwa kuelewa huyu ni nini hasa, msaada tafadhari yaani mpaka naogopa kukutana naye.
 
We subiri kuletewa virus,we una ushahidi kwamba si mwaminifu si uachane naye ala!!!
 
Hapo jibu liko wazi fanya kuachana nae maana ushahid unao kua s muaminifu unataka had kumfuma akiwa uchi ndo ujue anadhamiria unayoyaona?? halaf mwanaume mzima unalialia kias hiko ndo mana anakufanya mwehu maana kakuona unampenda sana!!
 
Leo nalivua pendo nililolipenda zamani

mwasiti huyo hebu sikiliza
 
Yani wewe miaka mitatu unalia tu, halafu bado hujajua cha kufanya? Sasa kama anakuliza kila siku unasubiri nini hapo kwake, au mwenzetu kulia ni sehemu yako ya maisha?
 
Sasa hapo unataka kufa,maana naona kulia hakutoshi.
TUPA KULE MTU KAMA HUYO WA NINI.
 
Mwanamke hachunguzwi, ila kama unapenda maumivu endelea kumchunguza.
Cha msingi ni kwenda mdogo mdogo na kupotezea, ile fikra ya kua unapigiwa itakutoka na utaishi vizuri sana na amani juu ya mpenzi wako umpendae, usimuache mkuu.

Mimi nina mahusiano na binti mmoja kwa sasa mahusiano yetu yamefikia miaka mitatu. Lakini cha kushangaza kila ninapokutana naye lazima nitoke machozi, yaani lazima atapigiwa simu ambazo zinanikwaza na nikijaribu kudadisha mwisho wa siku lazima nitoke machozi. Pia nikikagua simu yake lazima nitakuta meseji ambazo zitanitoa machozi.
Kwangu huyu amekuwa zaidi ya bomu la machozi sasa nashindwa kuelewa huyu ni nini hasa, msaada tafadhari yaani mpaka naogopa kukutana naye.
 
Yani wewe miaka mitatu unalia tu, halafu bado hujajua cha kufanya? Sasa kama anakuliza kila siku unasubiri nini hapo kwake, au mwenzetu kulia ni sehemu yako ya maisha?

ana kiwanda cha kuzalisha machoz
 
Hli suala nalo linahitaji semina elekezi kweli?
 
pole sana i wonder why watu huwachezea watu wanaowapenda kwa roho na kweli jamani
 
Utakuwa na tatizo kitaalamu linaitwa Dacryocystitis ama wakati mwingine huitwa lacrimal sac....nafikiri ndilo linalokusababisha kila ukikutana na huyo mke wa kijiji unatokwa machozi...by the way embu jaribu kuwa mwanaume halafu tuone kama bado tatizo lako litaendelea kukusumbua!
 
sasa kama unaogopa kukutananae unasubiri nini kuachananae na kutafuta mwingine,au mpaka upate vvu!??
 
Ukiwa ushazoea kuliliwa halafu unasikia kuna mtu analia lia kwa ma.laya hasira zinapanda hadi puani
 
Kwangu huyu amekuwa zaidi ya bomu la machozi sasa nashindwa kuelewa huyu ni nini hasa, msaada tafadhari yaani mpaka naogopa kukutana naye.

Hivi ni kwamba umekatwa kichwa kiasi huwezi kufikiri?

Mtu ambaye wewe unamuita ni mwandani wako washindwa kumuelewa, je sisi tusomjua tutamuelewaje!!

Mungu hajakupa kichwa ili ufugie nywele pekee, tumia ubongo wako vizuri...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom