ChizzoDrama
JF-Expert Member
- Sep 29, 2019
- 1,317
- 1,229
Marijani Rajabu
Umahiri mkubwa wa kupiga ala tofauti tofauti za Muziki kutoka kwa magwiji wa muziki Africa kipindi hicho kama; Sory Kandia Koutare toka huko guinea na Tabu Ley Rochereau (Tabu ley) aliye kuwa kiongozi wa Orchestre Afrisa International.
☆ Ulimvutia zaidi kijana mdogo wa umri wa miaka 15 tu, mwenye mapenzi na muziki na kipaji kikubwa ndani yake. Mzawa wa Kariakoo Dar es Salaam akiwa na asili ya Kigoma (kwa maana ya chimbuko la wazazi wake). Tarehe ya 23, mwezi March mwaka wa 1955, ndiyo siku ambayo.
☆ Mtoto huyu wa Africa alizaliwa katika familia ya kawaida kabisa ya mchapakazi na mchapishaji wa majarada mzee Rajabu, vijana wa sasa wangesema (Rajabu Sr). Ilipofika mwaka 1970 tu, akiwa bado mwanafunzi Marijani alifanikiwa kujiunga na bendi ya STC Jazz Band (The jets).
☆ Chini ya bendi hii ambayo ilikuwa ikiongozwa na mkongwe Raphael Sabuni ilipata mualiko kwenda katika tamasha huko Nairobi Kenya, safari iliyo zaa tungo kadhaa zilizorekodiwa chini Phillips record ambazo inasadikika ni mchango mkubwa wa utunzi wa marijani ulifanikisha hilo.
☆ Ikumbukwe Marijani alikuwa bado kijana mdogo, hivyo kutokana na umri wake kufanya shughuli hizo ilileta shida katika bendi ile ambayo kimsingi ilikuwa ya umma hivyo ililazimu akae mbali kwa katazo la kutojihusisha nalo, kwa hofu ya kuvunja sheria.
☆ Baadae mwaka 1972, Marijani alijiunga na bendi ya The Trippers Band (trippers kwa lugha ya kikwetu ni wasafiri) kwa mnaochanganyikiwa kidogo na lugha 😁😁. The Tripper ikiongozwa na David Mussa kama Mkurugenzi (muimbaji), na muimbaji kiongozi kwa jina la Ali Rajabu.
☆ Walifanikiwa kuachia vibao kadha wa kadha maarufu kama;
● Rosa Nenda Shule
● Mkuki Moyoni
● Georgina
● Olilla
Ambapo kwa taarifa Bwana David Mussa alikiri kuuzwa kwa nakala takribani 10,000 za santuri, jambo lililo pelekea waweze kununua vyombo vya bendi (Pichani, J Mussa).
☆ Palipo na wengi basi mambo huwa mengi vilevile (waswahili wanasema). Baada ya kupata mafanikio hayo wanahisa (wazee wa bendi), kati yao kukatokea mtafaruku ambao ulipelekea kutokuelewana kabisa na hatimaye bendi ikasambaratika. The trippers au Safari Band ikatoweka.
☆ Hata hivyo huo ulikuwa mwisho wa Trippers Band na siyo mwisho wa safari ya muziki ya gwiji Marijani rajabu. Ambaye ilipofika mwaka 1976, alipata wazo la kuanzisha band ambapo ilipidi kwanza kupata wadhamini, hapo ndipo anaingia Mzee Zakaria Ndabemeye kuokoa jahazi.
☆ Sasa kilichobaki ilikua ni kutengeneza kikosi cha mashambulizi (eeh ndiyo), maana bendi kwa wakati ule ushindani wake ulikuwa mkubwa mnoo kama Simba na Yanga hivi sasa.
Basi usajiri ukaanza (usiniulize dirisha kubwa au dogo 😁😁) na Kikosi kikawa hivi 👇
● Abel Baltazar (toka Msondo)
● Kassim Mponda ( toka Trippers)
● Said Mohamed (toka Polisi Jazz)
● C, Chimule (toka Urafiki)
● Balesa Kakere (toka Biashara Jazz)
● Joseph Bernad (Toka Trippers)
● Ali Rajabu (Toka Trippers)
● King Michael (Dar Jazz)
☆ Baada ya kuwa na mtafaruku na mmoja ya waimbaji wenziwe aliyefahamika kama Abel Baltazar juu ya kile kilicho itwa ubishi. Chidumule anasimulia kuwa kuna moja ya tungo ambayo iliimbwa na ikatokea kufanana sana na moja ya tungo huko congo, hivyo ililazimu Marijani.
☆ Abadili namna ya uimbaji huo kusudi usishabihiane, jambo ambalo marijani hakulihafiki, hivyo kupelekea kufukuzwa katika bendi, ambapo baadae alirudishwa baada ya waimbaji wengi kuikimbia tena bendi hiyo
☆ Baada ya kurudi tena Dar es Salaam International hiyo ilikuwa 1978 inaenda 1979, yule hasimu wake bwana Abel Baltazar alitimka na baadhi ya waimbaji wenzake na kwenda kuanzisha bendi ya Ochestra MLlimani Park.
☆ Hama hama ile ya waimbaji kama walivyo pendwa kuitwa na siyo (wasanii), Marijani alikutana na watu wapya kabisa katika bendi baada ya ujio wake mara ya pili, wakongwe kama, Chistopher Kasongo, Mohammed Tungwa, Hamis Milambo, Athumani Momba na Alex Kanyimbo.
☆ Ni katika kipindi hiki hiki baada ya ujio huu Marijani aliweza pia kushika mkono wasanii waliokuwa wachanga ambao baadae wakaja kuwa wakubwa sana katika uwanda huu. Wasanii kama Fresh Jumbe ambaye kwa sasa makazi yake ni Japan Tokyo, akiendelea na shughuli za muziki katika kumbi.
☆ Alifanikisha pia kutoa album iliyokuwa na vibao kama Zuena na Mwanameka, vibao vilivyokuwa gumzo na vingine vikifanyiwa sample mpaka leo hii na wasanii wa Bongo Fleva, lakini katika kazi kubwa yote hiyo pesa aliyo ambulia ilikuwa ni 2500/= Th toka RTD
☆ Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD), ambao ndiyo walihusika na recording nzima hiyo ilikuwa ni mwaka 1983 na ilipofika mwaka 1987. Bend ya Dar International ilikufa na hii ni kutokana na sababu za uchakavu wa vyombo na malipo yasiyoridhisha.
☆ Nyota wetu wa mchezo wa leo anaingia katika kundi lile lile la masikini wenye majina makubwa mpaka pale umauti ulipo mfika. Na kwa ushahidi wa wazi kabisa Marijani alianza kutembeza kanda za nyimbo zake mitaani ili kujipatia chochote kutokana na ugumu wa maisha.
☆ Zipo bendi kadhaa ambazo gwiji huyu alipita japo siyo kwa mafanikio makubwa kama;
● Arusha jazz
● Mwenge Jazz
Pia akiambatana na Muhidin Maalim Ngurumo, mwaka huo wa 1987 katika kuhadhimisha miaka 20 ya azimio la arusha la 1967, waliongoza jopo la waimbaji zaidi ya 50 na kuunda Tanzania All Stars kwa mara ya kwanza (huu umekuwa utamaduni ambapo kila maadhimisho).
Basi waimbaji wa aina tofauti za muziki hujumuika pamoja na kuhamasisha uzalendo kupitia uimbaji.
Huyo ndiyo MARIJANI RAJABU (marijani wa zuwena)
Imeandikwa na ChizzoDrama ✍
Umahiri mkubwa wa kupiga ala tofauti tofauti za Muziki kutoka kwa magwiji wa muziki Africa kipindi hicho kama; Sory Kandia Koutare toka huko guinea na Tabu Ley Rochereau (Tabu ley) aliye kuwa kiongozi wa Orchestre Afrisa International.
☆ Ulimvutia zaidi kijana mdogo wa umri wa miaka 15 tu, mwenye mapenzi na muziki na kipaji kikubwa ndani yake. Mzawa wa Kariakoo Dar es Salaam akiwa na asili ya Kigoma (kwa maana ya chimbuko la wazazi wake). Tarehe ya 23, mwezi March mwaka wa 1955, ndiyo siku ambayo.
☆ Mtoto huyu wa Africa alizaliwa katika familia ya kawaida kabisa ya mchapakazi na mchapishaji wa majarada mzee Rajabu, vijana wa sasa wangesema (Rajabu Sr). Ilipofika mwaka 1970 tu, akiwa bado mwanafunzi Marijani alifanikiwa kujiunga na bendi ya STC Jazz Band (The jets).
☆ Chini ya bendi hii ambayo ilikuwa ikiongozwa na mkongwe Raphael Sabuni ilipata mualiko kwenda katika tamasha huko Nairobi Kenya, safari iliyo zaa tungo kadhaa zilizorekodiwa chini Phillips record ambazo inasadikika ni mchango mkubwa wa utunzi wa marijani ulifanikisha hilo.
☆ Ikumbukwe Marijani alikuwa bado kijana mdogo, hivyo kutokana na umri wake kufanya shughuli hizo ilileta shida katika bendi ile ambayo kimsingi ilikuwa ya umma hivyo ililazimu akae mbali kwa katazo la kutojihusisha nalo, kwa hofu ya kuvunja sheria.
☆ Baadae mwaka 1972, Marijani alijiunga na bendi ya The Trippers Band (trippers kwa lugha ya kikwetu ni wasafiri) kwa mnaochanganyikiwa kidogo na lugha 😁😁. The Tripper ikiongozwa na David Mussa kama Mkurugenzi (muimbaji), na muimbaji kiongozi kwa jina la Ali Rajabu.
☆ Walifanikiwa kuachia vibao kadha wa kadha maarufu kama;
● Rosa Nenda Shule
● Mkuki Moyoni
● Georgina
● Olilla
Ambapo kwa taarifa Bwana David Mussa alikiri kuuzwa kwa nakala takribani 10,000 za santuri, jambo lililo pelekea waweze kununua vyombo vya bendi (Pichani, J Mussa).
☆ Palipo na wengi basi mambo huwa mengi vilevile (waswahili wanasema). Baada ya kupata mafanikio hayo wanahisa (wazee wa bendi), kati yao kukatokea mtafaruku ambao ulipelekea kutokuelewana kabisa na hatimaye bendi ikasambaratika. The trippers au Safari Band ikatoweka.
☆ Hata hivyo huo ulikuwa mwisho wa Trippers Band na siyo mwisho wa safari ya muziki ya gwiji Marijani rajabu. Ambaye ilipofika mwaka 1976, alipata wazo la kuanzisha band ambapo ilipidi kwanza kupata wadhamini, hapo ndipo anaingia Mzee Zakaria Ndabemeye kuokoa jahazi.
☆ Sasa kilichobaki ilikua ni kutengeneza kikosi cha mashambulizi (eeh ndiyo), maana bendi kwa wakati ule ushindani wake ulikuwa mkubwa mnoo kama Simba na Yanga hivi sasa.
Basi usajiri ukaanza (usiniulize dirisha kubwa au dogo 😁😁) na Kikosi kikawa hivi 👇
● Abel Baltazar (toka Msondo)
● Kassim Mponda ( toka Trippers)
● Said Mohamed (toka Polisi Jazz)
● C, Chimule (toka Urafiki)
● Balesa Kakere (toka Biashara Jazz)
● Joseph Bernad (Toka Trippers)
● Ali Rajabu (Toka Trippers)
● King Michael (Dar Jazz)
☆ Baada ya kuwa na mtafaruku na mmoja ya waimbaji wenziwe aliyefahamika kama Abel Baltazar juu ya kile kilicho itwa ubishi. Chidumule anasimulia kuwa kuna moja ya tungo ambayo iliimbwa na ikatokea kufanana sana na moja ya tungo huko congo, hivyo ililazimu Marijani.
☆ Abadili namna ya uimbaji huo kusudi usishabihiane, jambo ambalo marijani hakulihafiki, hivyo kupelekea kufukuzwa katika bendi, ambapo baadae alirudishwa baada ya waimbaji wengi kuikimbia tena bendi hiyo
☆ Baada ya kurudi tena Dar es Salaam International hiyo ilikuwa 1978 inaenda 1979, yule hasimu wake bwana Abel Baltazar alitimka na baadhi ya waimbaji wenzake na kwenda kuanzisha bendi ya Ochestra MLlimani Park.
☆ Hama hama ile ya waimbaji kama walivyo pendwa kuitwa na siyo (wasanii), Marijani alikutana na watu wapya kabisa katika bendi baada ya ujio wake mara ya pili, wakongwe kama, Chistopher Kasongo, Mohammed Tungwa, Hamis Milambo, Athumani Momba na Alex Kanyimbo.
☆ Ni katika kipindi hiki hiki baada ya ujio huu Marijani aliweza pia kushika mkono wasanii waliokuwa wachanga ambao baadae wakaja kuwa wakubwa sana katika uwanda huu. Wasanii kama Fresh Jumbe ambaye kwa sasa makazi yake ni Japan Tokyo, akiendelea na shughuli za muziki katika kumbi.
☆ Alifanikisha pia kutoa album iliyokuwa na vibao kama Zuena na Mwanameka, vibao vilivyokuwa gumzo na vingine vikifanyiwa sample mpaka leo hii na wasanii wa Bongo Fleva, lakini katika kazi kubwa yote hiyo pesa aliyo ambulia ilikuwa ni 2500/= Th toka RTD
☆ Radio Tanzania Dar es Salaam (RTD), ambao ndiyo walihusika na recording nzima hiyo ilikuwa ni mwaka 1983 na ilipofika mwaka 1987. Bend ya Dar International ilikufa na hii ni kutokana na sababu za uchakavu wa vyombo na malipo yasiyoridhisha.
☆ Nyota wetu wa mchezo wa leo anaingia katika kundi lile lile la masikini wenye majina makubwa mpaka pale umauti ulipo mfika. Na kwa ushahidi wa wazi kabisa Marijani alianza kutembeza kanda za nyimbo zake mitaani ili kujipatia chochote kutokana na ugumu wa maisha.
☆ Zipo bendi kadhaa ambazo gwiji huyu alipita japo siyo kwa mafanikio makubwa kama;
● Arusha jazz
● Mwenge Jazz
Pia akiambatana na Muhidin Maalim Ngurumo, mwaka huo wa 1987 katika kuhadhimisha miaka 20 ya azimio la arusha la 1967, waliongoza jopo la waimbaji zaidi ya 50 na kuunda Tanzania All Stars kwa mara ya kwanza (huu umekuwa utamaduni ambapo kila maadhimisho).
Basi waimbaji wa aina tofauti za muziki hujumuika pamoja na kuhamasisha uzalendo kupitia uimbaji.
Huyo ndiyo MARIJANI RAJABU (marijani wa zuwena)
Imeandikwa na ChizzoDrama ✍
Attachments
-
images - 2023-05-24T013802.624.jpeg21.8 KB · Views: 7
-
Screenshot_20230524-020639_Chrome.jpg100.3 KB · Views: 14
-
Marijani_Rajabu (1).jpg10.3 KB · Views: 12
-
images - 2023-05-24T022621.785.jpeg9.6 KB · Views: 13
-
David_Mussa_na_Marijani.jpg24.2 KB · Views: 11
-
images - 2023-05-24T022616.128.jpeg10.1 KB · Views: 9
-
images - 2023-05-24T025337.542.jpeg11.3 KB · Views: 9
-
images - 2023-05-24T031541.927.jpeg10.3 KB · Views: 12
-
440px-Fresh_Jumbe.jpg21.7 KB · Views: 13
-
images - 2023-05-24T031415.262.jpeg37.2 KB · Views: 9
-
images - 2023-05-24T013222.179.jpeg31.9 KB · Views: 11