Travelogue_tz
JF-Expert Member
- Sep 28, 2010
- 855
- 1,224
Na Mwanahalisi
Masalia ya Zitto yapukutishwa CHADEMA
Na Alfred Lucas - Imechapwa 01 June 2011
Printer-friendly version
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ililazimika kujigeuza mahakama ili kusikiliza malalamiko dhidi ya wagombea nafasi ya uenyekiti wa baraza la vijana la chama hicho (BAVICHA).
Katika kusikiliza malalamiko hayo, Kamati Kuu iliwateua wanasheria wake mashuhuri, Mabere Marando na Profesa Abdallah Safari kuwa majaji wa kuendesha kesi ya Habibu Mchange aliyekuwa anawania nafasi ya mwenyekiti.
Mchange ambaye anajitambulisha kuwa ni mfuasi wa naibu katibu mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe lilalamikiwa na mwenyekiti wa BAVICHA mkoani Mwanza, Liberatus Mlebele kukiuka maadili ya uchaguzi, ikiwamo kusafirisha wajumbe wa mkutano wa uchaguzi kutoka mikoani hadi Dar es Salaam.
Ndani ya CC, Mchange alilazimika kujibu tuhuma moja baada ya nyingine ikiwamo malalamiko ya kushindwa kuwajibika yaliyofunguliwa na katibu wa BAVICHA jimbo la Kigamboni.
Katibu huyo alimtuhumu Mchange kushindwa kutimiza wajibu wake kwa kile alichoeleza, "Tangu achaguliwe kushika nafasi ya mwenyekiti wa BAVICHA wilayani humo hajahudhuria vikao."
Mjumbe mmoja wa CC amedokeza gazeti hili kuwa Mchange ambaye alionekana kuwa na wafuasi wengi, alikatwa kwa kuwa alishindwa kujitetea mbele ya mahakama ya CHADEMA.
Kwa mfano, kati ya 20 Mei na 25 mwaka huu, Mchange alituma zaidi ya Sh. 2, 561,000 kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa vijana kutoka katika mikoa mbalimbali nchini. Fedha hizo zilitumwa na Mchange mwenyewe kupitia mtandao wa M-Pesa na Tigo Pesa.
Namba ya Mchange iliyotumika kusambaza fedha hizo, ni 0658 178678. Alianza kutapakanya fedha kwa wajumbe 11 Mei 2011 saa 10:44.58 ambapo kiasi cha Sh. 28,500 zilitumwa kwa mmoja wa wajumbe wenye simu Na. 0659 374206.
Baadaye saa 11:04.24 alituma Sh. 15,500 kwenda Na. 0659 374206 na kisha 20 Mei 2011 saa 14:03.04 alituma Sh. 19,000 kwa mwenye Na. 0713 866650.
Tarehe 23 Mei 2011 saa 10:56.06, nyaraka zinaonyesa Mchange alituma Sh. 50,000 kwenda kwa mwenye Na. 0713 867745; tarehe 21Mei 2011 saa 11:54.47 alituma Sh. 40,000 kwenda kwa mwenye Na. 0717 268576 na saa 12:41.48 alituma Sh. 81,000 kwa mwenue Na. 0714 038536.
Wengine waliotumiwa fedha na Mchange; ni wenye Na. 0712 511508 aliyetumiwa Sh. 26,000 na mwenye Na. 0713 606169 aliyetumiwa Sh. 10,000 ambaye alitumiwa fedha hizo, saa 22:24.31.
Nyaraka za M-PESA zinamuonyesha Mchange akimtumia Peter Shiyo, mwenyekiti wa BAVICHA wilayani Maswa Sh. 50,000. Fedha hizo zilitumwa 23 Mei 2011 saa 16:39.
Tarehe hiyo 23 Mei 2011 saa 18:48, Mchange alituma kiasi cha Sh. 30,000 mwenyekiti wa vijana wilaya ya Singida Mjini, Wilfred Kitundu.
Aidha, siku hihiyo Mchange akitenda kama karani wa benki alituma Sh. 150,000 kwa mwenyekiti wa baraza hilo mkoani Mwanza, Liberatus Mlebele.
Mara baada ya kupokea fedha hizo, Mlebele aliwasilisha malalamiko kwa katibu mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa akimtuhumu Mchange kumshawishi kwa njia ya rushwa ili amchague kuwa mwenyekiti.
Katika barua yake hiyo, Mlebele pamoja na mambo mengine alisema, "Ninakuandikia kwa nia njema kabisa ya kulinda hadhi ya chama chetu nikiomba maelekezo yako kama mtendaji mkuu wa chama."
Anasema, "Tarehe 28 Mei 2011 Baraza la Vijana wa chama chetu litafanya uchaguzi wa viongozi wake wa kitaifa. Je, sisi wajumbe tumegharamiwa na chama ama wagombea kufika Dar es Salaam kwa ajili ya uchaguzi huu?
Alisema, "Ninauliza hivi kwa sababu tayari mmoja wa wagombea ameshaniagiza kufika Dar es Salaam kwa gharama zake ili kukagua hoteli ambayo wajumbe wa mkoa wangu na kwingineko watafikia hali ambayo ninaihesabu kama rushwa."
Mlebele alisema katika barua yake, "Niko tayari kutoa vielelezo sahihi juu ya kitendo hiki kama itabidi, ili kulinda hadhi ya chama chetu dhidi ya watu hatari kama hawa."
Alisema, "Kwa kuwa mimi binafsi sipendi rushwa na siwezi kuvumilia vitendo vya rushwa na kwa kuwa natambua chama chetu kimekuwa kinara wa kupambana na rushwa nchini, ninaomba kamati kuu ichukue hatua stahiki dhidi ya mtu huyu ili kulinda hadhi ya baraza na chama chetu mbele ya wananchi."
Ni maelezo hayo ya Mlebele yaliyozika ndoto za Mchange kuwa mwenyekiti wa BAVICHA. Taarifa zinasema Dk. Slaa aliwasilisha malalamiko yote mbele ya wajumbe wa CC. Barua ya Mabele iliwasilishwa kwa Dk. Slaa, 26 Mei 2011.
Taarifa zinasema kabla ya CC kujigeuza mahakama ya kusikiliza shauri hilo, mjumbe mmoja alinukuliwa akimtetea Mchange. Hata hivyo, alizimwa na Dk. Slaa aliyesimama kidete kutaka chama chake kichunguze suala hilo na kichukue hatua.
Katika barua yake, Mlebele anasema alifikia katika hoteli ya Bondeni One iliyoko Magomeni. Anamtaja Mchange kuwa ndiye aliyelipa fedha hizo. Alitoa nakala ya kitabu cha wageni kuthibitisha kuwa fedha hizo zililipwa na aliyemteja.
Mchange alikiri mbele ya wajumbe wa CC kuwa ni kweli kwamba simu iliyotajwa kupeleka fedha ni yake; alimhonga Mlebele kiasi kilichotajwa, alilipia sehemu ya gharama za hoteli na alikiri kumuagiza akusanye wajumbe wa mkutano wa uchaguzi.
Kamati kuu ya CHADEMA ilipitisha majina ya wagombea tisa katika nafasi ya mwenyekiti na kisha kukasimu madaraka yake kwa kamati ya wazee kwa hatua nyingine inazoona zinafaa.
Ni kupitia kamati hiyo, ndiko wagombea wengine watatu walifyekwa. Waliopatwa na panga la kamati hiyo iliyokuwa chini ya Edwin Mtei, Bob Makani na mwanasheria wa chama hicho, Mabere Marando, ni Mtela Mwampamba, Bernard Saanane na Grayson Nyakarugu, huku John Heche akionywa na na kuelezwa ikibainika alifanya vitendo kinyume cha maandili, atavuliwa madaraka.
Wote waliokatwa walipatikana na makosa ya rushwa, kutoaminika, kupanga matokeo, makundi na kutumiwa na watu wa kutoka nje ya baraza la vijana.
Akifanya marejeo ya kilichofanyika Jumamosi katika uchaguzi huo uliofanyika ukumbi wa PTA Sabasaba, Temeke, jijini Dar es Salaam, Dk. Slaa alisema chama chake kimeweza kunasua mitego yote ya rushwa iliyopandikizwa na CCM.
UPDATE; Majibu ya Mchange.
Masalia ya Zitto yapukutishwa CHADEMA
Na Alfred Lucas - Imechapwa 01 June 2011
Printer-friendly version
KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ililazimika kujigeuza mahakama ili kusikiliza malalamiko dhidi ya wagombea nafasi ya uenyekiti wa baraza la vijana la chama hicho (BAVICHA).
Katika kusikiliza malalamiko hayo, Kamati Kuu iliwateua wanasheria wake mashuhuri, Mabere Marando na Profesa Abdallah Safari kuwa majaji wa kuendesha kesi ya Habibu Mchange aliyekuwa anawania nafasi ya mwenyekiti.
Mchange ambaye anajitambulisha kuwa ni mfuasi wa naibu katibu mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe lilalamikiwa na mwenyekiti wa BAVICHA mkoani Mwanza, Liberatus Mlebele kukiuka maadili ya uchaguzi, ikiwamo kusafirisha wajumbe wa mkutano wa uchaguzi kutoka mikoani hadi Dar es Salaam.
Ndani ya CC, Mchange alilazimika kujibu tuhuma moja baada ya nyingine ikiwamo malalamiko ya kushindwa kuwajibika yaliyofunguliwa na katibu wa BAVICHA jimbo la Kigamboni.
Katibu huyo alimtuhumu Mchange kushindwa kutimiza wajibu wake kwa kile alichoeleza, "Tangu achaguliwe kushika nafasi ya mwenyekiti wa BAVICHA wilayani humo hajahudhuria vikao."
Mjumbe mmoja wa CC amedokeza gazeti hili kuwa Mchange ambaye alionekana kuwa na wafuasi wengi, alikatwa kwa kuwa alishindwa kujitetea mbele ya mahakama ya CHADEMA.
Kwa mfano, kati ya 20 Mei na 25 mwaka huu, Mchange alituma zaidi ya Sh. 2, 561,000 kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa vijana kutoka katika mikoa mbalimbali nchini. Fedha hizo zilitumwa na Mchange mwenyewe kupitia mtandao wa M-Pesa na Tigo Pesa.
Namba ya Mchange iliyotumika kusambaza fedha hizo, ni 0658 178678. Alianza kutapakanya fedha kwa wajumbe 11 Mei 2011 saa 10:44.58 ambapo kiasi cha Sh. 28,500 zilitumwa kwa mmoja wa wajumbe wenye simu Na. 0659 374206.
Baadaye saa 11:04.24 alituma Sh. 15,500 kwenda Na. 0659 374206 na kisha 20 Mei 2011 saa 14:03.04 alituma Sh. 19,000 kwa mwenye Na. 0713 866650.
Tarehe 23 Mei 2011 saa 10:56.06, nyaraka zinaonyesa Mchange alituma Sh. 50,000 kwenda kwa mwenye Na. 0713 867745; tarehe 21Mei 2011 saa 11:54.47 alituma Sh. 40,000 kwenda kwa mwenye Na. 0717 268576 na saa 12:41.48 alituma Sh. 81,000 kwa mwenue Na. 0714 038536.
Wengine waliotumiwa fedha na Mchange; ni wenye Na. 0712 511508 aliyetumiwa Sh. 26,000 na mwenye Na. 0713 606169 aliyetumiwa Sh. 10,000 ambaye alitumiwa fedha hizo, saa 22:24.31.
Nyaraka za M-PESA zinamuonyesha Mchange akimtumia Peter Shiyo, mwenyekiti wa BAVICHA wilayani Maswa Sh. 50,000. Fedha hizo zilitumwa 23 Mei 2011 saa 16:39.
Tarehe hiyo 23 Mei 2011 saa 18:48, Mchange alituma kiasi cha Sh. 30,000 mwenyekiti wa vijana wilaya ya Singida Mjini, Wilfred Kitundu.
Aidha, siku hihiyo Mchange akitenda kama karani wa benki alituma Sh. 150,000 kwa mwenyekiti wa baraza hilo mkoani Mwanza, Liberatus Mlebele.
Mara baada ya kupokea fedha hizo, Mlebele aliwasilisha malalamiko kwa katibu mkuu wa chama hicho, Dk. Willibrod Slaa akimtuhumu Mchange kumshawishi kwa njia ya rushwa ili amchague kuwa mwenyekiti.
Katika barua yake hiyo, Mlebele pamoja na mambo mengine alisema, "Ninakuandikia kwa nia njema kabisa ya kulinda hadhi ya chama chetu nikiomba maelekezo yako kama mtendaji mkuu wa chama."
Anasema, "Tarehe 28 Mei 2011 Baraza la Vijana wa chama chetu litafanya uchaguzi wa viongozi wake wa kitaifa. Je, sisi wajumbe tumegharamiwa na chama ama wagombea kufika Dar es Salaam kwa ajili ya uchaguzi huu?
Alisema, "Ninauliza hivi kwa sababu tayari mmoja wa wagombea ameshaniagiza kufika Dar es Salaam kwa gharama zake ili kukagua hoteli ambayo wajumbe wa mkoa wangu na kwingineko watafikia hali ambayo ninaihesabu kama rushwa."
Mlebele alisema katika barua yake, "Niko tayari kutoa vielelezo sahihi juu ya kitendo hiki kama itabidi, ili kulinda hadhi ya chama chetu dhidi ya watu hatari kama hawa."
Alisema, "Kwa kuwa mimi binafsi sipendi rushwa na siwezi kuvumilia vitendo vya rushwa na kwa kuwa natambua chama chetu kimekuwa kinara wa kupambana na rushwa nchini, ninaomba kamati kuu ichukue hatua stahiki dhidi ya mtu huyu ili kulinda hadhi ya baraza na chama chetu mbele ya wananchi."
Ni maelezo hayo ya Mlebele yaliyozika ndoto za Mchange kuwa mwenyekiti wa BAVICHA. Taarifa zinasema Dk. Slaa aliwasilisha malalamiko yote mbele ya wajumbe wa CC. Barua ya Mabele iliwasilishwa kwa Dk. Slaa, 26 Mei 2011.
Taarifa zinasema kabla ya CC kujigeuza mahakama ya kusikiliza shauri hilo, mjumbe mmoja alinukuliwa akimtetea Mchange. Hata hivyo, alizimwa na Dk. Slaa aliyesimama kidete kutaka chama chake kichunguze suala hilo na kichukue hatua.
Katika barua yake, Mlebele anasema alifikia katika hoteli ya Bondeni One iliyoko Magomeni. Anamtaja Mchange kuwa ndiye aliyelipa fedha hizo. Alitoa nakala ya kitabu cha wageni kuthibitisha kuwa fedha hizo zililipwa na aliyemteja.
Mchange alikiri mbele ya wajumbe wa CC kuwa ni kweli kwamba simu iliyotajwa kupeleka fedha ni yake; alimhonga Mlebele kiasi kilichotajwa, alilipia sehemu ya gharama za hoteli na alikiri kumuagiza akusanye wajumbe wa mkutano wa uchaguzi.
Kamati kuu ya CHADEMA ilipitisha majina ya wagombea tisa katika nafasi ya mwenyekiti na kisha kukasimu madaraka yake kwa kamati ya wazee kwa hatua nyingine inazoona zinafaa.
Ni kupitia kamati hiyo, ndiko wagombea wengine watatu walifyekwa. Waliopatwa na panga la kamati hiyo iliyokuwa chini ya Edwin Mtei, Bob Makani na mwanasheria wa chama hicho, Mabere Marando, ni Mtela Mwampamba, Bernard Saanane na Grayson Nyakarugu, huku John Heche akionywa na na kuelezwa ikibainika alifanya vitendo kinyume cha maandili, atavuliwa madaraka.
Wote waliokatwa walipatikana na makosa ya rushwa, kutoaminika, kupanga matokeo, makundi na kutumiwa na watu wa kutoka nje ya baraza la vijana.
Akifanya marejeo ya kilichofanyika Jumamosi katika uchaguzi huo uliofanyika ukumbi wa PTA Sabasaba, Temeke, jijini Dar es Salaam, Dk. Slaa alisema chama chake kimeweza kunasua mitego yote ya rushwa iliyopandikizwa na CCM.
UPDATE; Majibu ya Mchange.
thread hii imeletwa hapa kimkakati,
kwa kuwa walioleta wanawajua waliowatuma, na kwa kuwa wao kwa ufupi wao wa kufikiri wanaamini kuwa hii ndio silaha yao kwangu, leo nasema ukweli kuhusu hili humu jamvini, tena nasema ukweli bila hata kumung'unya neno hata moja, na wakati nasema ukweli najua kuna watu watasema nilikuwa wapi siku zote.
ndugu zangu, mimi ni muumini mzuri sana wa siasa za kweli na haki, mimininaamini katika mtu kuwa awarded kulingana na nafasi na ushiriki wake, lakini kikubwa mimi ni muumini mzuri wa kuhakikisha chama changu kinaendelea kuwa imara.
NASEMA HIVI.
1. sijakatwa na kuenguliwa BAVICHA kwa sababu ya rushwa, nimekatwa kwa sababu za siasa zenu hizi cha chuki, unafiki na majungu majungu ziizotawaliwa na WOGA...msimamo wangu wa kutokubali kumezeshwa ujinga kichwani mwangu ndio kinachoniponza zaidi.
2. waliokuwepo kwenye kikao wakati nakatwa wanaweza kuthibitisha. alitafutwa hadi GIRLFRIEND wangu aandike mashtaka kuwa mimi sio mstaarabu ili nienguliwe lakini akakataa...wakatafutwa hadi watu wa VCOBA wakasema nimewadhurumu wakatafutwa hadi viongozi wanafiki wakasema nimewatukana..nafahamu moyoni kwanini nilienguliwa BAVICHA na hata HECHE anafahamu kwanini ALIPEWA KITI cha dezo''...hakuna kesi ya rushwa duniani kote yenye adhabu ya kumuengua mtu kwenye uchaguzi na kesi kuishia hapo hapo.. mwanahalisi wao walijikuta wakinitumia kutimiza malengo yao kumshambulia Zitto, in any how kama niliyekatwa ni mimi kulikuwa na haja gani ya kumuhusisha zitto kwenye ukatwaji wangu?.
3. hakuna kesi ya rushwa duniani kote ambayo mwendesha mashtaka ndio huyo huyo mshitaki, ndio huyo huyo shahidi na ndio huyo huyo hakimu....na kama mimi nilienguliwa kwa rushwa MWAMPAMBA alienguliwa kwa kosa gani?...NYAKARUNGU alienguliwa kwa sababu ipi?.
sisi tunaokipenda chama tuliamua kukaa kimya tuendelee kukuza chama, kukaa kwetu kimya hakukumaanisha kuwa ni wajinga. ukwatwaji wangu unahusika moja kwa moja mikakati ya baadhi ya viongozi wa kichama kuhakikisha sishindi, mwanzo walizani nacheza walipoona nguvu yangu wakaungana na kuamua kunikata. nasisitiza tena rushwa ilikuwa ni shitaka moja kati ya mashitaka zaidi ya nane niliyosomewa kwenye hicho kikao.
katika kuwathibitishia kuwa mwanahalisi ilifanya kazi ya kuhalalisha ukatwaji wangu ili kujihami kuwa nilitoa rushwa kwa madai eti chama chetu ni mpiganaji mkuu wa rushwa, naomba nisisitize yafuatayo.
1. Mwanahalisi ambalo ndio linatumiwa kama kielelezo kikuu cha mashtaka yangu imeongopa kama alivyofanya ndugu ben saa nane hii leo.
A. ukijumlisha jumla ya pesa ambazo wanadai nilizituma haziwezi kufika hata laki tano wao wamesema nimetuma jumla ya shilingi milioni 2.5 huu ni uwongo nilioudharau kuupinga lakini sasa lazima niweke kumbukumbu sawa.
B. Mtitiriko wa mashtaka hayo umekaa kiujanja ujanja kiasi kwamba hakukuwa hata na namba moja ya kweli niliyoirushia pesa, leo nitazielezea namba zote zilizoorodheshwa hapo kwenye gazeti hilo.
(i) mwanahalisi wanasema '' Alianza kutapakanya fedha kwa wajumbe 11 Mei 2011 saa 10:44.58 ambapo kiasi cha Sh. 28,500 zilitumwa kwa mmoja wa wajumbe wenye simu Na. 0659 374206''. ukweli ni kwamba mwenye namba 0659374206 hajawahi wala sio mjumbe wa BAVICHA..mwenye namba hiyo kipindi hicho ni mzee hamis lichonyo ambaye umri wake unazidi miaka 63 kwa sasa, huyu ni mzee wangu katika siasa na ni mwenyeji wa mkoa wa lindi, tumefundishwa vijana kuishi vizuri na wazee wetu, hivyo mzee wako anapokuomba msaada si vibaya kumsaidia, nilimsaidia mzee wangu..
(ii) mwanahalisi waliendelea kuongopa ''Mchange alituma Sh. 50,000 kwenda kwa mwenye Na. 0713 867745'' ukweli ni kwamba mmiliki wa namba hii ni ndugu fikirini rajabu, huyu wakati namtumia pesa alikuwa ni mwanafunzi wa mwaka wa pili wa chuo kikuu cha dodoma akisoma project planning and community development-hajawahi hata kuwa kiongozi wa kata wa chadema wala BAVICHA.
(iii). wakaendelea kudanganya kuwa mchange ''alituma Sh. 19,000 kwa mwenye Na. 0713 866650''. ukweli ni kwamba mmiliki wa namba hii ni NDUGU NKYA ambaye ni mfanya kazi wa kampuni ya simu ya tigo tawi la mlimani city nilipompigia simu baada ya gazeti hili kuchapishwa akacheka sana na kuahidi kutokuwa mwanachama wa chama chochote cha siasa.
(iv) mwanahalisi likaendelea kudanganya watanzania kuwa Wengine waliotumiwa fedha na Mchange; ni wenye Na. 0712 511508 aliyetumiwa Sh. 26,000.....oooh my God MWANAHALISI WALIENDELEA kudanganya, mmiliki wa namba hii anaitwa ALLY MCHANGE, ni kaka yangu wa kuzaliwa, yeye ni mtaalamu wa hotelians na mechanical engineer, hajui lolote kuhusu siasa na wala hana kadi ya chama chochote cha siasa, tukio pekee la kisiasa alilowahi kushiriki ni kunisaidia kwenye kampeni zangu za ubunge wa kibaha. mwanahalisi ni WANAFIKI NA WAONGO KAMA BEN SAA NANE.
(iv) mwanahalisi waliendelea kubwabwaja kuwa saa 12:41.48 alituma Sh. 81,000 kwa mwenue Na. 0714 038536. hapa waliendelea kudanganya sana, mwenye namba hii anaitwa NYEMBO M. TEMBA huyu hajawahi kuwa mjumbe waBAVICHA HATA SIKU MOJA, yeye ni msaidizi wa mweshimiwa zitto kabwe tena jimboni kigoma kaskazini tena wa kijijini mwandiga.
(V) Uwongo mwingine wa MWANAHALISI NI HUU kuwa niliendelea kutuma pesa kwenda kwa mjumbe mwenye mwenye Na. 0713 606169 aliyetumiwa Sh. 10,000 ambaye alitumiwa fedha hizo, saa 22:24.31. --hapa pia walidanganya kikamilifu, mmiliki wa namba hii anaitwa EDWARD KINABO (naye ni mwana JF), na kipindi hicho naye alikuwa anagombea ujumbe wa BARAZA KUU KUPITIA BAVICHA huku akiwa ni mwandishi wa habari wa GAZETI LA TANZANIA DAIMA na makala zake maarufu za WARAKA WA KINABO, ni rafiki yangu sana sana siku hiyo nilikutana naye sinza, WHITE INN BAR akaniambia ndugu yangu nataka kwenda sehemu lakini sina pesa, mimi nikamwambia sina CASH naweza kukurushia kwenye TIGO PESA tukakubaliana nikamrushia tukaachana akaenda na zake. gazeti lilipotoka hakuwa ameiona namba yake, akanipigia simu kunipa pole, nikamwambia sijawahi kutoa rushwa kwenye maisha yangu, na sitakuja kutoa rushwa mpaka naingia kaburini, akabisha nikamwonyesha namba yake, nikamuuliza nawewe nilikupa rushwa?. akasikitika tukaendelea na mishe nyingine...
namba pekee ya mjumbe wa bavicha bwana liberatus dotto ambaye nilimtumia jumla ya shilingi 40 elf (mwanahalisi wao wamedanganya kuwa nilimrushia laki moja na nusu-150,000/=) ambazo yeye mwenyewe aliniomba mara nne tofauti, mara ni 0717 268576 AMBAYE KUMBE ALITUMWA NA WAPINZANI WANGU ASEME NIMEMPA RUSHWA, Mungu ni mkubwa kwani wakati anatoa ushuhuda wa mimi kumrushia yeye rushwa ya nauli tayari nilishapata nakala ya ticket yake ya ndege ya shirika la precision air yenye namba E-TICKET NUMBER 03144109725678 ya ndege aina PW411 ya kwenda Dar tarehe 25.05.2012 na kurudi mwanza tarehe 02.07.2012 AMBAPO ALIWASILI JKN AIRPORT SAA 10:00AM na kurudi mwanza kwa ndege ya saa 18:00 jioni kwa tarehe hisika. ticketi hizi zililipiwa na kiongozi mmoja wa chama ambaye kwa kipindi hicho alikuwa mbunge na taarifa zinasema alirudishiwa pesa zake na chama baada ya kutimiza kazi zake ipasavyo---hapa walidhihirisha ujinga wao na nikazidi kuwadharau..maana wamenishtaki kwa kutoa rushwa ya kutengeneza huku wao wakitoa rushwa ya zaidi ya laki 3.7 kwa ticket....
MWANAHALISI walishindwa kuthibitisha kuonyesha Transactions za watu waliowataja kama Wlfred kitundu wa singida na mwengine yeyote, badala yake wakachukua print out zangu za tigo na mpesa na kuzihusianisha na rushwa, hii ni lugha ile ile aliyoionyesha saa nane humu jamvini..
siku katibu mkuu ananisomea haya mashtaka sikuamini macho na masikio yamgu, sikuamini kama kiongozi niliyekuwa nataraji angekuwa rais miezi sita nyuma angeweza kushiriki kwenye uwongo wa namna ile..
narudia sikutaka kuweka hadharani haya kwa sababu yanawahusu moja kwa moja viongozi wangu wa chama..
nasema tena kwa msisitizo, SIJAENGULIWA BAVICHA KWA SABABU YA RUSHWA, NIMEENGULIWA KWA SABABU YA SIASA ZA WOGA DHIDI YA MAHUSIANO YANGU NA ZITTO.
nitaendelea kufichua kila unafiki dhidi yangu mpaka hapo jamii itakapoelewa na kuziona true colours za baadhi ya wiongozi wetu.