mayenga
JF-Expert Member
- Sep 6, 2009
- 4,118
- 1,966
Jana nilikuwa naangalia kipindi cha usiku wa habari TBC1.Kilichonistua si kingine ni huyu mgombea ubunge wa jimbo la Mtera kupitia CCM,aliyemwangusha Mzee Malecela(TingaTinga) katika kura za maoni.Dogo alikuwa akiwahutubia wananchi ila sehemu ifuatayo ya maneno yake iliniacha hoi:
"Walikuja wanaume wagombea udiwani wakapita,wakaja wanaume wagombea ubunge wakapita,wakaja wanaume wagombea urais wakapita,lakini mimi ndo mwanaume kamili"
Imekaaje Hii.
"Walikuja wanaume wagombea udiwani wakapita,wakaja wanaume wagombea ubunge wakapita,wakaja wanaume wagombea urais wakapita,lakini mimi ndo mwanaume kamili"
Imekaaje Hii.