Huyu demu kanitosa kisa elf 3000

Huyu demu kanitosa kisa elf 3000

pesa ipo, ila kulipa limtu ambalo halijafanya kazi yeyote hapana,
 
Wazazi wenye watoto wa kiume, tangu wakiwa wadogo wafunzeni namna ya kuhudumia na kuwa Mwanaume.
 
Kuna Dada aliniambia nimkopeshe 10k angenilipa mwisho wa mwezi, ilikuwa 2016 mpaka keshokutwa nikimdai ananiambia hana, mbaya zaidi ni MKE WA MTU SUMU
 
Hivi wanawake mmekuwaje siku hizi mbona mnapenda hela hivyo? daah siamini huyu binti mwenye mtoto mmoja amenichunia kisa nimekataa kumpa elf 3000, wakati yeye anafanya biashara yake huu ni ungwana kweli ? hapa mimi siwezi mizinga isiokuwa na maana.
Wacha utoswe tu, kwa sababu hakuna namna. Kwa kulilia huku nano atakuvumilia? Any way wewe ni dar au mkoani?
 
Hivi wanawake mmekuwaje siku hizi mbona mnapenda hela hivyo? daah siamini huyu binti mwenye mtoto mmoja amenichunia kisa nimekataa kumpa elf 3000, wakati yeye anafanya biashara yake huu ni ungwana kweli ? hapa mimi siwezi mizinga isiokuwa na maana.
kama buku 3 ndio umeanzisha thread nashauri moderator akufutie usajili humu huna maana yoyote
 
Mfuuuuuu elf tatu si ushukuru jamn hata ulipata dem wa kukuomba buku tatu halafu biashara yake yakuhusu nn
 
ELFU TATU? Duh hauko siliazi aise na watoto wa kike basi baki na elfu tatu yako maana nakuona una safari ndefu kama vile hautafika kabisa
 
Nina jirani yangu mwenyeji wa mkoa mmoja wa kaskazini alikuwa na mbwa anayemsaidia kwenye ulinzi usiku.
Kwa sababu ya ubahili ikawa anajaza maji kwenye ndoo halafu anatupia mfupa wenye nyama kidogo. Anamuita mbwa wake na kumuonyesha mfupa. Mbwa katika jitihada ya kufikia mfupa anashiba kwa kufakamia maji.Jamaa anatoa mfupa na kuanika.
Ubahili wa kushindwa kutoa 3000 umenikumbusha jirani yangu.
 
Hivi wanawake mmekuwaje siku hizi mbona mnapenda hela hivyo? daah siamini huyu binti mwenye mtoto mmoja amenichunia kisa nimekataa kumpa elf 3000, wakati yeye anafanya biashara yake huu ni ungwana kweli ? hapa mimi siwezi mizinga isiokuwa na maana.
sasa jamani buku 3 ndio inakuongelesha namna hii.. angekuomba hata buku kumi si ingekua balaa😀 wanaume wa Dar banah
 
Hata mim ningechuna. Ubahili gani huo?! Muda mwingine m'mke anapokuomba ela anakupima tu! Siyo kuwa kakosa kabisa! Au kakosa wa kumpa! Ila anapima moyo wako wa kujitolea kwake.. Kwahyo jitafakari vizur
 
Hivi wanawake mmekuwaje siku hizi mbona mnapenda hela hivyo? daah siamini huyu binti mwenye mtoto mmoja amenichunia kisa nimekataa kumpa elf 3000, wakati yeye anafanya biashara yake huu ni ungwana kweli ? hapa mimi siwezi mizinga isiokuwa na maana.
Kakukataa kisa 3000 ndio mana mimi nilivyo mzalisha nikakataa kumuoa kwa tamaa zake
 
unadhani angekuomba sh ngapi ungetoa na usingekuja kundika huku JF?
 
Back
Top Bottom