Huyu dada anaomba ushauri

Huyu dada anadate na wanaume 2 tofauti.Mmoja ana hela afu mwingine naye kapuku Hana mafaranga Ni wa kuunga unga tu.
Sasa huyu dada alijichanganya akastukia ameukwaa ujauzito wa huyu mwana kapuku.Akaamua kumbambikizia mimba jamaa wake mwenye pesa.Jamaa akaridhiria kulea mimba kwa bidii Sana akijua mimba Ni ya kwake kumbe hola anamlelea mwanaume mwenzie.
Miezi 8 ikapita Mambo yakabadilika ghafla,aliyekuwa kapuku akastawi kiuchumi Mambo yakabadilika nywee,na huyu jamaa aliyekuwa na pesa mwanzo akafulia mazima.

Sasa dada wa watu amechanganyikiwa kbsa hajui Nini Cha kufanya.Yuko njia panda ameshindwa awaite wanaume wake wote awaambie ukweli ama afanyaje.Anatamani kuirudisha mimba kwa mwanaume halali( aliyekuwa kapuku mwanzo) ila anashindwa ataanza vipi coz mimba imelelewa na mwanaume mwingine.
Naamini ushauri wenu utamfaa zaidi.

Nawasilisha.
Dah eti mwana kapuku
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom