Huyu bwana kaumia sana mimi kuolewaa

Huyu bwana kaumia sana mimi kuolewaa

Me nilishakuwa na mwanaume wa hivi anafanya vituko vyote anavyovijua yeye..akadai anaoa mm namchelewesha ..yaan n manyanyaso mwanzo mwisho... Nilikaa mwaka nikiwa single ..baadaye nkapata mwanaume mwingine..sasa baada ya kuona Niko na mwanaume mwingine hataki kuamin kama Niko na mwanaume mwingine anajishaua kunilalamikia na kuomba msamaha..

Mumy huu n unafiki na ushamba achana naye halafu hakikisha hakufuatilii kwenye mtandao maana atakuharibia ndoa muda si mrefu..unaweza kumblock ili asione picha wala statuses wala video zako. Watu wa hivi wanaboa siyo siri.
Afadhali wew umenielewa,nashukuru kwa ushauri wako
 
Mamboz?
Jamn kuna watu hata sijui niwaweke kwenye kundi gani,sawa aliwahi kuwa wangu wa "moyo" ila ghafla akabadilika.Mawasiliano akakata na baada ya muda akanitangazia anaoa,basi kwa uhakika akanitumia mipicha ya harusi yake mpk memory ikajaa.ukweli niliumia ila Mungu si Jf namimi nikabarikiwa mume .

Miez miwil iliyopita ndio nilifunga ndoa takatifu, ukweli sikumjulisha coz sikuona sababu ya kufanya hvyo.Ila dunia haina siri taarifa ikamfikia akanipigia cm kunipa hongera basi, kuolewa ni baraka jmn nikawa najikuta tu napost picha na video za harus yngu kwenye status yangu wasap nikimshukuru Mungu. Sasa tangu huyu bwana kajua nimeolewa imekua kero kutwa ananipigia cm eti ananipenda,ooo mara harus yako ilinoga sana ,we mzuri aisee huyu mke niliemuoa hatuendan ,natamn turudiane na uchafu mwingi mwingi.
Sasa juzi kapost Instagram video yngu fupi niliyokua nikimuimbia mume wangu nyimbo ya Ed sheeran "perfect duet" half chini akaandika " I was d only one deserve this n not that ass" . kaniudh saaaana ,nmfanyej?? Nimwambie my lovely haya makaraha au ninyamaze tu??
Hamkumalizana vizuri, itakuharibia ndoa
 
Kuna mambo mengine hata hayahitaji ushauri.

we endelea na hayo mawasiliano upasue ndoa yako
 
.............Hii ndiyo aina ya wanawake wanandoa tuliokuwa nao!Sasa wewe dada yangu,unamshukuruje Mungu kupitia status zako w'app Mungu unaemwamini wewe unadhani huwa anapata muda kupita kwenye profile yako kuziangalia?

Ningetegemea useme ulikuwa unaenda kufanya ibada kwenye nyumba ya imani unayoiamini ila unatuma shukurani zako status,kesho na kesho kutwa ndoa yako ikiingia msala usianze kulia Mungu wangu kwanini umeniacha maana ni uzembe wako.

Niishie hapa usije ukasema na mimi inaniuma wewe kuolewa.
 
Back
Top Bottom