wa stendi
JF-Expert Member
- Jul 7, 2016
- 24,796
- 26,964
Kama mnavyokumbuka kipindi cha nyuma awamu ya 4 chini ya Jakaya Kikwete iliwahi tokea sintofahamu kati ya Rais Kikwete wa Tanzania na Rais wa Rwanda, Paul Kagame.
Na wakati huo yale malumbano yalimalizwa kidiplomasia/kimazungumzo mambo yakaisha, lakini kuna baadhi hadi walimuona JK kipindi hicho kwa nini anakuwa mpole, wakati jeshi na nguvu na uwezo anao, kwanini anakubali kudharauliwa kiasi hicho.
Hivi kwa dharau zile za Kagame kipindi hicho Kikwete angelikuwa na maamuzi magumu kama ya Magufuli, mpaka sasa hii nchi ingekuwa kwenye wakati gani? Je, Magufuli angepeleka jeshi msituni au angekuwa mkimya kukubali yaishe kama Kikwete?
Karibuni kwa hoja.
Na wakati huo yale malumbano yalimalizwa kidiplomasia/kimazungumzo mambo yakaisha, lakini kuna baadhi hadi walimuona JK kipindi hicho kwa nini anakuwa mpole, wakati jeshi na nguvu na uwezo anao, kwanini anakubali kudharauliwa kiasi hicho.
Hivi kwa dharau zile za Kagame kipindi hicho Kikwete angelikuwa na maamuzi magumu kama ya Magufuli, mpaka sasa hii nchi ingekuwa kwenye wakati gani? Je, Magufuli angepeleka jeshi msituni au angekuwa mkimya kukubali yaishe kama Kikwete?
Karibuni kwa hoja.