Huu unyama utaisha lini?

Huu unyama utaisha lini?

Geza Ulole

Platinum Member
Joined
Oct 31, 2009
Posts
72,763
Reaction score
103,609
20th February 13
Mwigulu: How chopped off my arm
mwigulu-albino-feb20-2013(1).jpg

Mwigulu Matonange (10), a Standard I pupil at Msia Primary School in Sumbawanga District, nurses wounds at Mtowisa Health Centre after an attack on February 15 in which his left arm was chopped off. (Photo: Correspondent Emmanuel Kwitema, UTSS Sumbawanga)

Correspondent
Mwigulu Gimbishi Matonange (10) a standard One pupil with albinism at Msia Primary School in Sumbawanga Rural District, 117 kilometres from the town, is now admitted at Mtowisa Health Centre nursing wounds after criminals cut off his left arm.
Narrating the ordeal in his native language of Sukuma, which was then translated into Swahili by his father, Gimbishi Lugwisha Magesse Matonange; the humble, but courageous boy said on February 15, he was literally kidnapped by two strangers who took him to a hill and hacked off his arm.

"I was held down like a goat about to be slaughtered. One of them covered my eyes with his hat apparently to stop me from watching what they were about to embark on. I then felt a sharp pain in my arm as a machete cut through the flesh and bone. They dismembered my left arm from the rest of my body," Mwigulu tells a team of Under The Same Sun (UTSS) who visited him at the hospital in Rukwa last Sunday.

The team was also visiting a woman with albinism, Maria Chambanenge (39) of Mkowe village in Miangalua who is admitted at the Regional Hospital after unknown criminals invaded her house while she was asleep and chopped off her left arm on February 11, this year.
Rukwa Regional Crimes Officer (RCO), Peter Ngussa told UTSS in his office that his force has arrested five people in connection with the incident and that Maria's arm was recovered where the goons had left it, somewhere in a bush between Miangalua and Mkowe.
It was at this time that young Mwigulu suffered the horrible experience.

Mwigulu told the UTSS team that after cutting off his arm, the two men disappeared into the thick forest with his arm wrapped in the dirty clothes they had, leaving him helpless and bleeding profusely. "I did not lose hope," said Mwigulu, adding that he struggled to move from where he was left and started to climb down the hill hoping to reach home, but he was bleeding profusely and losing strength.

"I felt weak and decided to rest a little," he said. While he was still figuring out how he could reach home alive, he heard some people calling out his name. "They were calling my name." He used his remaining strength to respond, shouting: "I am here! I am here! Come and help me! They have cut off my arm."

His elder cousin, Mwigulu Chilomwa was the one who reached him first. They covered the wound with clothes to stop the bleeding before taking him home and later to a nearby dispensary at Msia village where the nurses disinfected the wound and dressed it. He was later taken on a motorcycle to Mtowisa Health Centre, 32 kilometres from their home village, where he is currently admitted for treatment. According to the Centre's doctor Frednand Yunga, Mwigulu's condition is improving.

When asked what should be done to the criminals if they are caught, the confident Mwigulu did not hesitate to state clearly: "They should be beheaded because they had planned to kill me."

His father Matonange says he becomes confused when his son Mwigulu M reminds him that he would like to go back to school as soon as he is discharged and the money donated by the Good Samaritans for his treatment should be used to buy him a pair of socks as part of school uniform. Matonange says however that his boy does not want to go back home and to the same school in Msia because he is afraid the same men would come back to hack off his remaining arm.

Recounting what had happened before the thugs captured him on the fateful day, Mwigulu says he remembers to have left the school a bit earlier because his neighbour 17-year old Mwigulu (Standard VI) was not feeling well. Normally his brother Didi would escort him to and from the school. But he had not finished his assignment in school. So when neighbour Mwigulu offered to go home with Mwigulu, Didi allowed him to. Their home is in an isolated area near a forest, three kilometers from the Msia centre.

On their way home, Mwigulu says they saw two unidentified men who were walking fast trying to catch up with them. As they approached home just near a bridge they saw them "closely watching where we were heading," narrates Mwigulu.

He said as soon as they reached home, they had their lunch before he and his younger cousin Luwilimila Mashala (12), a standard II pupil of the same school left for a nearby seasonal stream, a kilometre away from their home to bathe. As they approached the tributary they saw a herd of cattle grazing near their farms.

They decided to move the cows far away towards a nearby forest to prevent them from destroying their crops. They saw the two strangers they had earlier seen by the roadside. The two unidentified men asked them if they happened to have seen their red cow. They boys told them that they had not come across the cow in question.

Mwigulu said that one of the two assailants snatched his hand, while the other was chasing his cousin with an intention of abducting him as well. Luwilimila was helpless as he witnessed his cousin Mwigulu being dragged up the hill into the forest. It was then that he decided to run as fast as he could to the village to seek help.

He met his brother Mwigulu Chilomwa weeding his farm and he broke news that strangers had abducted Mwingulu and that they were heading towards the top of a nearby hill. Mwigulu Chilomwa and a group of villagers managed to find him lying down in the bush, very tired and still bleeding.

Speaking to UTSS on the two events Rukwa Regional Commissioner, Engineer Stella Manyanya said the regional administration was taking the incidents very seriously and that police have confirmed that they have made arrests in connection with Maria's and Mwigulu's attackers. "Let us give them time to finish the investigations so that the criminals would be brought to the court of law for justice to take its course," she told UTSS team.

However, Manyanya said she that does not expect the office of government attorneys in the region to dilly- dally in bringing the case to court when they have all the necessary evidence.

She said, "It is true there are legal and human rights implications in these cases. But what human rights issues are there to be discussed when one person cuts another's hand with a machete without mercy and the evidence is right there?"

THE GUARDIAN
Mwigulu: How chopped off my arm

MY TAKE
Ina maana Kikwete anafurahia haya au? Je Kikwete ni mshirikina au? Na kama sio kwa nini wale waliokamatwa mwanzo na kupatikana na hatia na kuhukumiwa adhabu ya kifo suala lao limenyamazishwa? Hivi Kikwete anajua majukumu yake kikatiba kama Rais wa nchi? Au mpaka aone Riziwani amenyofolewa mkono ndo ataamka usingizini? Mwenzenu machozi yananitoka nikiona katoto cha miaka mikumi kakifanyiwa unyama wa kutisha uliokosa chembe ya utu!
 
Pole sana Mwigulu, inasikitisha sana hadi leo eti kuna watu wanaamini viungo vya binadamu wenzao vinasaidia kupata utajiri.
 
Dawa yake ni SHARIA LAW tu, Ukingoa jicho, unangolewa jicho. Mnaleta siasa katika Sheria Za Mungu! Hayo ndio matokeo yake.
 
20th February 13
Mwigulu: How chopped off my arm
mwigulu-albino-feb20-2013(1).jpg

Mwigulu Matonange (10), a Standard I pupil at Msia Primary School in Sumbawanga District, nurses wounds at Mtowisa Health Centre after an attack on February 15 in which his left arm was chopped off. (Photo: Correspondent Emmanuel Kwitema, UTSS Sumbawanga)

Correspondent
Mwigulu Gimbishi Matonange (10) a standard One pupil with albinism at Msia Primary School in Sumbawanga Rural District, 117 kilometres from the town, is now admitted at Mtowisa Health Centre nursing wounds after criminals cut off his left arm.
Narrating the ordeal in his native language of Sukuma, which was then translated into Swahili by his father, Gimbishi Lugwisha Magesse Matonange; the humble, but courageous boy said on February 15, he was literally kidnapped by two strangers who took him to a hill and hacked off his arm.

"I was held down like a goat about to be slaughtered. One of them covered my eyes with his hat apparently to stop me from watching what they were about to embark on. I then felt a sharp pain in my arm as a machete cut through the flesh and bone. They dismembered my left arm from the rest of my body," Mwigulu tells a team of Under The Same Sun (UTSS) who visited him at the hospital in Rukwa last Sunday.

The team was also visiting a woman with albinism, Maria Chambanenge (39) of Mkowe village in Miangalua who is admitted at the Regional Hospital after unknown criminals invaded her house while she was asleep and chopped off her left arm on February 11, this year.
Rukwa Regional Crimes Officer (RCO), Peter Ngussa told UTSS in his office that his force has arrested five people in connection with the incident and that Maria's arm was recovered where the goons had left it, somewhere in a bush between Miangalua and Mkowe.
It was at this time that young Mwigulu suffered the horrible experience.

Mwigulu told the UTSS team that after cutting off his arm, the two men disappeared into the thick forest with his arm wrapped in the dirty clothes they had, leaving him helpless and bleeding profusely. "I did not lose hope," said Mwigulu, adding that he struggled to move from where he was left and started to climb down the hill hoping to reach home, but he was bleeding profusely and losing strength.

"I felt weak and decided to rest a little," he said. While he was still figuring out how he could reach home alive, he heard some people calling out his name. "They were calling my name." He used his remaining strength to respond, shouting: "I am here! I am here! Come and help me! They have cut off my arm."

His elder cousin, Mwigulu Chilomwa was the one who reached him first. They covered the wound with clothes to stop the bleeding before taking him home and later to a nearby dispensary at Msia village where the nurses disinfected the wound and dressed it. He was later taken on a motorcycle to Mtowisa Health Centre, 32 kilometres from their home village, where he is currently admitted for treatment. According to the Centre's doctor Frednand Yunga, Mwigulu's condition is improving.

When asked what should be done to the criminals if they are caught, the confident Mwigulu did not hesitate to state clearly: "They should be beheaded because they had planned to kill me."

His father Matonange says he becomes confused when his son Mwigulu M reminds him that he would like to go back to school as soon as he is discharged and the money donated by the Good Samaritans for his treatment should be used to buy him a pair of socks as part of school uniform. Matonange says however that his boy does not want to go back home and to the same school in Msia because he is afraid the same men would come back to hack off his remaining arm.

Recounting what had happened before the thugs captured him on the fateful day, Mwigulu says he remembers to have left the school a bit earlier because his neighbour 17-year old Mwigulu (Standard VI) was not feeling well. Normally his brother Didi would escort him to and from the school. But he had not finished his assignment in school. So when neighbour Mwigulu offered to go home with Mwigulu, Didi allowed him to. Their home is in an isolated area near a forest, three kilometers from the Msia centre.

On their way home, Mwigulu says they saw two unidentified men who were walking fast trying to catch up with them. As they approached home just near a bridge they saw them "closely watching where we were heading," narrates Mwigulu.

He said as soon as they reached home, they had their lunch before he and his younger cousin Luwilimila Mashala (12), a standard II pupil of the same school left for a nearby seasonal stream, a kilometre away from their home to bathe. As they approached the tributary they saw a herd of cattle grazing near their farms.

They decided to move the cows far away towards a nearby forest to prevent them from destroying their crops. They saw the two strangers they had earlier seen by the roadside. The two unidentified men asked them if they happened to have seen their red cow. They boys told them that they had not come across the cow in question.

Mwigulu said that one of the two assailants snatched his hand, while the other was chasing his cousin with an intention of abducting him as well. Luwilimila was helpless as he witnessed his cousin Mwigulu being dragged up the hill into the forest. It was then that he decided to run as fast as he could to the village to seek help.

He met his brother Mwigulu Chilomwa weeding his farm and he broke news that strangers had abducted Mwingulu and that they were heading towards the top of a nearby hill. Mwigulu Chilomwa and a group of villagers managed to find him lying down in the bush, very tired and still bleeding.

Speaking to UTSS on the two events Rukwa Regional Commissioner, Engineer Stella Manyanya said the regional administration was taking the incidents very seriously and that police have confirmed that they have made arrests in connection with Maria's and Mwigulu's attackers. "Let us give them time to finish the investigations so that the criminals would be brought to the court of law for justice to take its course," she told UTSS team.

However, Manyanya said she that does not expect the office of government attorneys in the region to dilly- dally in bringing the case to court when they have all the necessary evidence.

She said, "It is true there are legal and human rights implications in these cases. But what human rights issues are there to be discussed when one person cuts another's hand with a machete without mercy and the evidence is right there?"

THE GUARDIAN
Mwigulu: How chopped off my arm

MY TAKE
Ina maana Kikwete anafurahia haya au? Je Kikwete ni mshirikina au? Na kama sio kwa nini wale waliokamatwa mwanzo na kupatikana na hatia na kuhukumiwa adhabu ya kifo suala lao limenyamazishwa? Hivi Kikwete anajua majukumu yake kikatiba kama Rais wa nchi? Au mpaka aone Riziwani amenyofolewa mkono ndo ataamka usingizini? Mwenzenu machozi yananitoka nikiona katoto cha miaka mikumi kakifanyiwa unyama wa kutisha uliokosa chembe ya utu!

Nawe usiwe kama mpumbavu asiyetaka kutumikia akili yake kutafakari. Haya mauji yameanzia kwa kikwete au kabla yake? Unataka yeye ndo aende kuzuia? wewe umefanya nini? Mbona hujasema pinda ambaye mahaya yametokea anakotoka? Au ni wale wale wa udini? Hebu tuwe realistic, tuchambue mambo kwa mtazamo chanya uenda tukapata majibu sahihi. Lakini kwa mwendo wa ndugu yangu huyu hatutafika>
Sina hakikia kama umesoma hata civics -je, hujui hata mgawanyo wa madaraka ya mihimili ya dola? Unataka kikwete akakamate, ashitaki, ahukumu na asimamie magereza? Hebu kuwa mfikiriaji huru na chanya, usipendelee kulishwa maneno ya kusema, iko siku huyo unayemtaka atakuwa madarakani, vipi kama haya yataendelea utasema kama hivi?
JAribu kidogo tu kujiheshimu na kujieklewa uenda ikawa heri kwako kuliko kukurupuka
 
Nawe usiwe kama mpumbavu asiyetaka kutumikia akili yake kutafakari. Haya mauji yameanzia kwa kikwete au kabla yake? Unataka yeye ndo aende kuzuia? wewe umefanya nini? Mbona hujasema pinda ambaye mahaya yametokea anakotoka? Au ni wale wale wa udini? Hebu tuwe realistic, tuchambue mambo kwa mtazamo chanya uenda tukapata majibu sahihi. Lakini kwa mwendo wa ndugu yangu huyu hatutafika>
Sina hakikia kama umesoma hata civics -je, hujui hata mgawanyo wa madaraka ya mihimili ya dola? Unataka kikwete akakamate, ashitaki, ahukumu na asimamie magereza? Hebu kuwa mfikiriaji huru na chanya, usipendelee kulishwa maneno ya kusema, iko siku huyo unayemtaka atakuwa madarakani, vipi kama haya yataendelea utasema kama hivi?
JAribu kidogo tu kujiheshimu na kujieklewa uenda ikawa heri kwako kuliko kukurupuka
wamekufa 72 kiasi kikubwa zaidi ya wakati wote na nina uhakika uuaji wa albino umeanza kipindi cha Kikwete huko nyuma vikongwe walikuwa wanauwawa ila si kwa kiasi hiki! Kiufupi moja na moja ni mbili huwezi sema kwa vile amuaji yalikuwapo basi Kikwete afumbe macho majukumu yake ya kikatiba kama Rais hayamruhusu kufanya hivyo ndo maana anaitwa dhaifu kwa vile kuna waliokutwa na hatia na mahakama na kupewa adhabu ya kifo lakini Kikwete amekalia mafaili hataki kuidhinisha adhabu kutekelezwa! Huwezi jua labda walikuwa wateja wake hao waliohukumiwa maana naskia Kikwete ni mtu wa Mlingotini!
 
Pole sana sana Mwigulu,Mwenyezi Mungu atakuongoza katika maisha yako.
 
[h=1]Albino auawa, wawili wakatwa viungo[/h]KWA UFUPI
Katika matukio hayo, mtoto mwenye umri wa miezi saba alinusurika kuuawa baada ya watu wasiojulikana kuvamia nyumba ya mama yake usiku katika eneo la Lamadi, Wilaya ya Busega, Mwanza siku moja baada ya kupokea ujumbe mfupi wa simu kwamba mtoto wake anawindwa.


Vicky Ntetema
HALI ya wasiwasi imetanda miongoni mwa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) nchini, baada ya watu watatu kukatwa viungo na mmoja wao kuuawa mwezi huu.

Katika miaka ya hivi karibuni, jumla ya albino 72 wameuawa, 34 wamenusurika, wengi wao kwa kukatwa viungo au kuumizwa. Makaburi 15 yamefukuliwa na viungo kuchukuliwa na kumekuwa na majaribio manne ya kufukua makaburi.
Katika matukio ya hivi karibuni, walemavu hao wakazi wa Tabora na Sumbawanga wamekatwa mikono ya kushoto. Ukatili huo safari hii umekwenda kinyume na ilivyokuwa mwaka 2010-2011 wakati mikono ya kuume ndiyo iliyokuwa inakisiwa.
Aliyeuawa ni
Lugolola Bunzari (7) na waliojeruhiwa ni Mwigulu Matonange (10) na Maria Chambanenge (39).

Katika matukio hayo, mtoto mwenye umri wa miezi saba alinusurika kuuawa baada ya watu wasiojulikana kuvamia nyumba ya mama yake usiku katika eneo la Lamadi, Wilaya ya Busega, Mwanza siku moja baada ya kupokea ujumbe mfupi wa simu kwamba mtoto wake anawindwa.

Marehemu Lugolola
Kijiji cha Kanoge kina umbali wa takriban kilomita 75 kutoka Tabora Mjini, barabara iendayo Ulyankulu kwenye machimbo ya dhahabu.
Imenichukua saa mbili na nusu kufika huko. Saa moja na nusu kati ya hizo, nilizitumia katika safari ya kilomita 15 tu kutoka Kanoge makao makuu ya kijiji hadi Kitongoji cha Kinondoni alikouawa mtoto Lugolola.

Nyumbani kwa Bunzari niliwakuta ndugu na jamaa kutoka vijiji vya jirani vya Wilaya hiyo ya Kaliua, Tabora. Bibi mzaa baba wa Lugolola, Gama Zengabuyanda (60), ndiyo kwanza alikuwa amerejea kutoka Hospitali ya Mkoa ya Kitete alikokuwa akitibiwa baada ya kushambuliwa na majambazi alipotaka kumwokoa mjukuu wake.

Huku akilia kwa huzuni, Zengabuyanda alinisimulia jinsi mjukuu wake na baba yake mzazi, Zengabuyanda Meli (95) walivyouawa kikatili.

Katika muda wa kati ya saa 10 na 11 alfajiri ya kuamkia Februari Mosi mwaka huu, Lugolola aliuawa kikatili baada ya kukatwa mkono kwa panga, kukwanguliwa nywele, kujeruhiwa mkono wa kulia na sikioni na kuondolewa ngozi kwenye sehemu ya paji la uso.

Katika mashambulizi hayo, babu yake Meli pia aliuawa alipojaribu kumwokoa mjukuu wake. Vilevile baba yake mzazi, Bunzari Shinga alijeruhiwa wakati alipojaribu kumlinda mwanaye.
Nilimkuta mama mzazi wa Lugolola aitwaye Kulwa akisaidiana na ndugu zake kumenya maharage mabichi waliyoyatoa shambani mwao muda mfupi tu uliopita.

Yeye ni mke mkubwa wa Bunzari Shinga (35). Walibahatika kupata watoto sita, wawili kati yao ni albino. Lugolola na marehemu mdogo wake aitwaye Maganga aliyefariki kwa malaria mwaka 2011.

Usiku wa mashambulizi hayo, Kulwa anasema alikuwa amelala na watoto wake wadogo wa kike (mmoja, Shija mkubwa) na Lugolola kwenye nyumba yake inayotazamana na ile ya mke mwenzake Pili, umbali wa takriban mita 20. Bunzari alikuwa amelala kwa mke huyo mdogo na binti yao mwenye umri wa mwaka mmoja hivi.

Mzee Meli alikuwa amelala na watoto wa kiume upande wa kulia wa nyumba ya Kulwa.
"Aliamshwa usingizini na kelele za watoto waliokuwa wakilalamika kwamba wanapigwa na fimbo. Alipotaka kwenda chumbani kwa watoto alishambuliwa kwa mapanga kichwani, usoni, mgongoni, mikononi na miguuni," Gama anaelezea huku akilia.

"Pamoja na hayo yote, Baba alijikongoja kuelekea kwenye nyumba alimolala mjukuu wangu, Lugolola huku akipiga mayowe, Tumevamiwa! Nani anataka kuwadhuru watoto wangu."
Majangili hayo yakamshambulia zaidi kwa mapanga na marungu na huo ndiyo ulikuwa mwisho wake. Jamani Baba yangu!"
Gama anasema alikuwa amelala kwenye banda lake lililopo kati ya nyumba ya pili na ile ya babu.

Banda hilo la nyasi na kuta za udongo na miti lilikuwa limepambwa kwa vibuyu vya aina mbalimbali, tunguri, vyungu vilivyohifadhi mizizi, magamba ya miti, kauri (nyumba za konokono), hirizi, nywele za binadamu, taya za wanyama, vipande vya mifupa mbalimbali, fuvu la mnyama na gamba la kobe. Katika mazungumzo yetu niligundua kwamba Mzee Meli alikuwa mganga wa kienyeji.

Gama aliposikia vilio vya watoto alitoka nyumbani mwake na kukimbilia kwenye nyumba ya babu ili kujua kilichowatokea wajukuu wake na sababu iliyomfanya baba yake apige mayowe.

Akiwa nje alimwona baba yake akishambuliwa na watu watatu. Watu wengine wanne walikuwa wamesimama nje ya nyumba ya Kulwa wakiwa wameshika silaha mbalimbali ikiwa ni pamoja na magobole, mapanga na marungu. Gama alipiga kelele, ‘Tumevamiwa!' na mmoja kati ya watu hao alimshambulia kwa panga kichwani, miguuni na mikononi.
Alianguka na akapata mwanya wa kutambaa chini kwa chini kama nyoka hadi akafika kwenye shamba la mahindi na kupotelea kwenye vichaka.
Hata hivyo, alizimia na alipozinduka alijikuta akiwa Wodi ya Wanawake ya Hospitali ya Kitete.

Gama alikuwa amefiwa na mjukuu wake na baba yake mzazi. Kinachomsikitisha zaidi ni kwamba waliuawa bila ya hatia na hakupata hata fursa ya kuwaaga na kuwazika.
Itaendelea kesho...



http://www.mwananchi.co.tz/habari/Kitaifa/-/1597296/1705706/-/view/printVersion/-/14nnixj/-/index.html

Kwako Kikwete hapo Magogoni....:yo:
 
Na hii nchi mambo ya kishirikina watu wanayapenda sana, sijui tutabadilika lini.
 
[h=1]Albino auawa, wawili wakatwa viungo (2)[/h]
baba_albino.jpg
Baba mzazi wa marehemu Lugolola (7), Bunzari Shinga akiwa na majeraha aliyopata wakati akijaribu kumwokoa mtoto wake alipovamiwa na majambazi.
KWA UFUPI
"Ile kutoka tu, nilikumbana na risasi tatu tumboni na moja ilinipitia mguu wa kulia na kunitengua nguvu za kuendelea kusimama. Nilianguka na kulala kwenye vumbi kwa muda. Walipoona sitikisiki waliniacha palepale na kuendelea na uovu wao,"


Jana tuliishia pale Gama alipo zinduka na kujikuta akiwa katika Wodi ya Wanawake ya Hospitali ya Kitete na kueleza masikitiko yake ya kufiwa na mjukuu wake na baba yake mzazi ambao licha ya kuuawa bila ya hatia, hakupata hata fursa ya kuwaaga na kuwazika.
GAMA anaeleza kwamba miezi michache iliyopita, familia ilikuwa imepanga kumpeleka Lugolola kwenye Shule ya bweni baada ya kusikia taarifa za kuuawa na kukatwa viungo kwa watu wenye ulemavu wa ngozi.
"Lakini tukaambiwa kwamba umri wake ni mdogo kwa shule ya bweni. Hivi hawa watu walikuwa wanasubiri hadi mwana ngu auawe? Hii ni kazi ya ndani tu. Hakuna mtu wa nje ambaye angeweza kujua mahali aliko Lugolola, ambaye alikuwa amelala kama siyo jirani au ndugu wa familia hii," anasema mmoja wa ndugu wa familia aliyejitambulisha kwa jina la John.
Usiku ule wa mauaji Bunzari, aliposikia vilio vya watoto alitoka nje ya nyumba ya pili na kuelekea kwenye nyumba ya Babu Zengabuyanda.
"Ile kutoka tu, nilikumbana na risasi tatu tumboni na moja ilinipitia mguu wa kulia na kunitengua nguvu za kuendelea kusimama. Nilianguka na kulala kwenye vumbi kwa muda. Walipoona sitikisiki waliniacha palepale na kuendelea na uovu wao," anasimulia Bunzari akiwa katika Wodi ya Wanaume katika Hospitali ya Kitete.
"Nilipoona kuwa wameniacha, nilitambaa hadi kwenye shamba la mahindi na kuelekea msituni. Wakati nilipokuwa kule nikasikia sauti ya babu akitutahadharisha kwamba kaya yetu imevamiwa."
"Watoto waliendelea kulia na huku nikisikia jinsi majambazi hao yalivyokuwa yakiwachapa watoto kwa fimbo. Baadaye nilisikia sauti ya mwanangu mpenzi Lugolola."
"Alilia kwa uchungu na kutoa sauti kubwa mara moja tu na kisha sikumsikia tena. Ilikuwa kama uwanja wa vita. Hawa wali dhamiria kuua kila mtu ili wapate mkono wa mwanangu! Hivi amewakosea nini?" alisema Bunzari huku akilia... na kuongeza: "Babu yangu mpenzi amewakosea nini watu hawa?"
Muuguzi alisema risasi tatu zilitolewa kwenye nyonga na kwamba hali yake ilikuwa inaendelea vizuri.
Mke mdogo wa Bunzari, Pili, aliniambia kuwa aliposikia risasi zikirindima na nyingine kupiga ukutani, alijificha chumbani mwao hadi alipohisi kuwa majambazi yameondoka.
"Nilimbeba mwanangu na kukimbilia msituni nikimwita mume wangu kwa jina. Nilimkuta mtoto mmoja amekaa karibu naye. "Akamwambia kuwa ati akifariki dunia kwa kuwa alikuwa anatoka damu nyingi, basi yule mtoto awaelekeze watu kule msituni ili wamuokote na kumzika asiozee msituni. Nilimsaidia Bunzari hadi kwa jirani umbali wa kilomita moja hivi," anasema Pili.
Bunzari alipakiwa kwenye pikipiki na kupelekwa Zahanati ya Kanoge, kilomita 15 hivi kutoka nyumbani kwake ambako alipatiwa huduma ya kwanza na baadaye alipelekwa Tabora kwa gari la polisi.
Mtu ambaye hakuguswa na silaha hata kidogo ni Kulwa, mke wa kwanza wa Bunzari na ambaye ni mama mzazi wa Lugolola.
Huku akiendelea kumenya maharage mabichi alinisimulia jinsi alivyowatoa watoto wake aliokuwa nao usiku huo wakati wauaji hao wakiwa nje ya nyumba yake.
"Niliposikia kelele za watoto kutoka nyumbani kwa babu niliamka na kutoka nje. Nilipofika mlangoni nikawaona watu wanne wenye silaha za mapanga, magobole na marungu nje ya nyumba yangu."
"Mbele ya mlango wa babu niliwaona watu watatu pia wakiwa na silaha. Mtu mwingine mwenye silaha ikiwamo gobole alisimama mbele ya nyumba ya pili. Nilirudi ndani na kumchukua Shija, dada yake Lugolola na huyu wa mgo ngoni nikawapeleka vichakani. Nikarudi nikamchukua mdogo wake Lugolola mwenye miaka mitatu na kumpeleka vichakani."
"Nilipokuwa huko nikasikia sauti ya Lugolola ikilia mara moja tu. Kisha kukawa na kimya kikuu. Niliporudi nyumbani ndipo nikamkuta mwanangu ame nyofolewa mkono na amekufa."
Hakuonyesha simanzi wala hakuzungumza kwa uchungu. Kwangu mimi kama mzazi, iliniwia vigumu kumwelewa Kulwa. Kwanza nikiiangalia hali nzima ya mashambulizi katika kaya hiyo nikagundua kwamba yeye peke yake kati ya watu wote wazima hakuguswa hata kidogo na wauaji hao.
Amekutana nao ana kwa ana mara tatu na hakuna kilichomtokea. Kisha aliingia mara mbili ndani ya nyumba yake na kuwachukua watoto wale wengine wasio na albino na kuwaficha vichakani bila kukumbana na hasira za wauaji.
Swali nililomwuliza na ambalo hakulijibu ni kwa nini mara ya kwanza alipoingia ndani haku mchukua Lugolola mwenye umri wa miaka saba na ambaye anatembea mwenyewe bila kubebwa?
Iweje alimwacha mwanaye mwenye matatizo ya albino chumbani wakati anaingia na kutoka kuwasalimisha wengine?
Zengabuyanda Meli alishambuliwa na kuuawa mara tu alipotoka nyumbani kwake kwa lengo la kumwokoa Lugolola. Naye Gama Zengabuyanda alishambuliwa kwa mapanga alipojaribu kwenda walikolala watoto aliposikia vilio vyao. Bunzari alipigwa risasi nne na nyingine nne zikafikia ukutani alipotoka tu ndani ya nyumba yake.
"Mama Lugolola, imekuwaje wewe hukuguswa? Nilimwuliza Kulwa. "Sijui sasa!" lilikuwa jibu lake.
Bado nikiwa katika kaya hiyo ya Bunzari, maofisa wa polisi baadhi yao wakiwa na silaha waliwasili. Tulisalimiana na kujitambulisha na kisha walitaka niwapishe waendelee na uchunguzi wao.
Nilitumia muda huo kuzungumza na baadhi ya ndugu na jamaa waliokuwa pale. Karibu wote walisisitiza kwamba lazima kuna mtu wa karibu sana na familia au mwana familia ambaye alifanya njama hizo za kuuawa kwa Lugolola. Niliwasihi watoe taarifa hizo kwa siri kwa polisi ili wahusika wakamatwe.
Nilifika kwenye kaburi la Lugolola lililokuwa pembeni mwa zizi lakini mbali na lile la ndugu yake Maganga. Yote mawili yalikuwa ni ya udongo tu. Nilimwuliza Kulwa kwa nini Lugolola hakuzikwa karibu na mdogo wake aliyefariki kwa malaria.
"Familia imeamua hivyo!" ndilo lilikuwa jibu lake. Nilitaka kujua kama watalijengea kwa kutumia nondo, matofali na zege ili kuzuia watu wasije wakachukua viungo vilivyobaki. Makaburi mengi ya albino huimarishwa hivyo ili viungo vyao visitolewe na kupelekwa kwa waganga wa kienyeji.
Itaendelea kesho...

Albino auawa, wawili wakatwa viungo (2) - Kitaifa - mwananchi.co.tz

 
Back
Top Bottom