Huu ni urafiki wa mashaka! USA na Cuba?

Huu ni urafiki wa mashaka! USA na Cuba?

Mbavu mbili

JF-Expert Member
Joined
Apr 25, 2011
Posts
1,457
Reaction score
874
Ni miongo takribani mitano imepita tangu uhasama baina ya mataifa haya yajiingize ktk mzozo mzito wa Kidiplomasia. Hali hii ilipelekea Cuba kuwekewa vikwazo vikubwa vya kiuchumi hadi Leo.
Napata shaka urafiki huu unaorejea kwa kasi kadri Siku zinavyozidi kwenda.
Najiuliza maswali yafuatayo, ningali sipati majibu.
1: Ni kwa nini uhusiano huu wa Cuba na Usa unarejeshwa kipindi hiki?
2: Kama Fidel Castro angekuwa madarakani je uhusiano baina ya Cuba na Usa ungerejea kwa kasi namna Hii?
3: Je ni kwa nini uhusiano baina ya Cuba na Usa unaimarika zama hizi ambazo uhusiano baina ya Urusi na Marekani unazidi kuzorota?
4: Je huu ndio mwanzo wa kuanguka kwa Sera za ujamaa ktk nchi ya Cuba ?.
NB:
NIONAVYO MIMI NI KAMA KUNA URAFIKI WA MASHAKA KAMA ULE WA PAKA NA PANYA.

KARIBUNI KWA MJADALA
 
Back
Top Bottom