Sijali
JF-Expert Member
- Sep 30, 2010
- 2,589
- 1,679
Dunia nzima, sidhani kama kuna nchi inatumia jina la 'Dkt, Dokta, Dr. Daktari, kama Tanzania! Tena pasi na udhibiti. Hii ni dalili ya 'Educational inferiority complex' (mfundo wa moyoni wa uduni wa taaluma) waliyo nayo hao wanaojiita hivyo, au wanaokubali kuitwa.
Maana ndani ya nyoyo zao wanaamini kuwa wao ni mapepe tu kielimu, na ili kuwa aminisha wengine kuwa wao pia ni wana 'taaluma' katika hilo wanalolifanya, basi huweka/huwekewa hicho kibwagizo.
Tuliishi na Kambarage hapa miaka nenda miaka rudi, kwa kweli wachache sana walijua alikuwa Dokta, tena wa kusoma, si wa 'kutuzwa'. Kila mtu alijua Kambarage ni msomi pale tu alipofungua mdomo kuzungumza, hakuhitajia kibwagizo cha "Daktari'. Hivyo ndivyo usomi unavyotakiwa.
Kwa kweli viongozi wengi duniani ni 'Madokta', ila hadi ufanye utafiti ndiyo utajua hivyo.
Xi Jinping wa China ni Dokta wa Sheria, Narendra Modi wa India ni Dokta wa Elimu, Angela Merkel aliyekuwa Chancellor wa Ujerumani ni Daktari wa Physics, halkadhalika Hassan Rohani wa Iran alikuwa Dokta wa Sheria.
Ukija Afrika: Rais Ameena Gurib wa Mauritius ni Dokta wa Organic Chemistry, Mulatu Teshone wa Ethiopia: Sheria, Alassane Watara wa Cote d'Ivoire: Uchumi, Peter Mutharika, Malawi: Sheria, Mfalme Hassan, Morocco: Sheria na hata jrani Wlliam Ruto wa Kenya, tena Udokta wake wa aina yake, Plants Ecology (Wajua hiyo?) lakni kamwe hajiwekei au kuwekewa.
Sasa ingia Tanzania! Ndiyo nikasema hii yaonesha 'Educational inferiority Complex' kwa wataalamu wa maradhi ya nafsi watakwambia!
Ni aibu kujiita Dokta katika nchi ambayo hatutengenezi hata shazia, umeme unakatika kutwa, tukitaka barabara twamwita uncle wetu Mchina! Wakati huo huo eti tuna Vyuo Vikuu vinavyototoa madaktari hata wa Nanotechnology, Biotechnology, Physics. Ifike mahala tuone haya kuchekwa na walimwengu!
Tuacheni ushamba huu tukidhani kuwa ni 'ujanja' mwingine kutoka Tanzania. La, ni ujinga!
Maana ndani ya nyoyo zao wanaamini kuwa wao ni mapepe tu kielimu, na ili kuwa aminisha wengine kuwa wao pia ni wana 'taaluma' katika hilo wanalolifanya, basi huweka/huwekewa hicho kibwagizo.
Tuliishi na Kambarage hapa miaka nenda miaka rudi, kwa kweli wachache sana walijua alikuwa Dokta, tena wa kusoma, si wa 'kutuzwa'. Kila mtu alijua Kambarage ni msomi pale tu alipofungua mdomo kuzungumza, hakuhitajia kibwagizo cha "Daktari'. Hivyo ndivyo usomi unavyotakiwa.
Kwa kweli viongozi wengi duniani ni 'Madokta', ila hadi ufanye utafiti ndiyo utajua hivyo.
Xi Jinping wa China ni Dokta wa Sheria, Narendra Modi wa India ni Dokta wa Elimu, Angela Merkel aliyekuwa Chancellor wa Ujerumani ni Daktari wa Physics, halkadhalika Hassan Rohani wa Iran alikuwa Dokta wa Sheria.
Ukija Afrika: Rais Ameena Gurib wa Mauritius ni Dokta wa Organic Chemistry, Mulatu Teshone wa Ethiopia: Sheria, Alassane Watara wa Cote d'Ivoire: Uchumi, Peter Mutharika, Malawi: Sheria, Mfalme Hassan, Morocco: Sheria na hata jrani Wlliam Ruto wa Kenya, tena Udokta wake wa aina yake, Plants Ecology (Wajua hiyo?) lakni kamwe hajiwekei au kuwekewa.
Sasa ingia Tanzania! Ndiyo nikasema hii yaonesha 'Educational inferiority Complex' kwa wataalamu wa maradhi ya nafsi watakwambia!
Ni aibu kujiita Dokta katika nchi ambayo hatutengenezi hata shazia, umeme unakatika kutwa, tukitaka barabara twamwita uncle wetu Mchina! Wakati huo huo eti tuna Vyuo Vikuu vinavyototoa madaktari hata wa Nanotechnology, Biotechnology, Physics. Ifike mahala tuone haya kuchekwa na walimwengu!
Tuacheni ushamba huu tukidhani kuwa ni 'ujanja' mwingine kutoka Tanzania. La, ni ujinga!