Hili ni zuri sana ila biashara yenyewe haipo very certain i.e. hujui madini utapata au utakosa. Idara ya madini ingefanya good exploration na kuona kama kweli ni viable kumlazimisha mchimbaji mdogo kuinvest for a very long time without getting stones. Hii itawaondoa wachimbaji wote wadogo na watabaki wakubwa wenye mitaji mikubwa labda ndio lengu la serikali.
Nakuhakikishia hata hao wawekezaji wakubwa watakimbia au watapunguza wafanyakazi, maana hapo kwenye kutaja mshahara + idadi ya wafanyakazi wako ni mtego mkubwa sana kwao.
Hapo kutakuwa na makato mengi ambayo ni kodi ya serikali, mchango wa NSSF, chama cha wafanyakazi bima ya afya, na mishahara yao lazima uipitishie benk. Kwahiyo hutaweza kudanganya, pia kumbuka hapo mambo ya mshahara ishakuwa sheria, usipowalipa miezi kadhaa wanakushitaki.
Kwa pale ndani ya ukuta hakuna kampuni kubwa na lenye eneokubwa la uchimbani kama Tanzanite One Mining Limited, lakini nao wameshindwa kuwalipa wafanyakazi wao wote tokea mwezi wa 12 mwaka jana, mapaka leo hii mwezi wa 7/2018 ni takilibani miezi 9 wafanyakazi hawajapata chochote, alafu unatakiwa uwe unaenda kazini hivyo hivyo.
Lakini baada ya kuona maji yamewafika shingoni, Tanzanite One wanamadeni kila kona ya Nchi, kampuni ipo gizani hawana umeme kama miezi 4 sasa, wameamua kufunga kampuni kwa muda.
Hii sheria ya mikataba + mishahara ni vicheko kwa wafanyakazi, ila kwa yale mazingira ya wachimbaji wadogo wadogo navyowajua, watapata tabu sana. Wengi watafunga migodi yao, walishazoea kuchimba kwa ghalama nafuu, yaani wachimbaji unawanunulia chakula tu.