Huu ni uchochezi wa kidini!

Huu ni uchochezi wa kidini!

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
25,950
Reaction score
25,327
Tangu zamani waislamu na wakristo tumekuwa tukiishi kama ndugu huku tukishirikiana katika mambo mbali mbali ya kimaisha lakini kuna baadhi ya watu ambao wanataka kutugombanisha kwa maslahi yao binafsi.

Kuna waziri mwandamizi ambaye amesikika hivi karibuni akiwabagua waislamu akiwa ndani ya kanisa na amerudia uchochezi wake akiwa bungeni Dodoma.

Kitendo cha kudai kwamba wazanzibar wanataka kujitenga ili kuifanya Zanzibar kuwa nchi ya kiislamu ikiwa serikali 3 zitapita, ni uchochezi unaolenga kuwadhalilisha, kuwachafua na kuwashushia hadhi waislamu mbele ya jamii. Aidha, kuwahusisha uamsho na chama cha siasa sio jambo la kulifumbia macho hata kidogo. Lengo lake ni kutaka kuwagombanisha waislamu na jamii. Na ni bahati mbaya maneno haya yametamkiwa ndani ya kanisa, kitendo ambacho kinalenga kujenga chuki kati ya waislamu na wakristo.

Jamani, tuwapuuze hawa wabaguzi kwani hawana nia njema na amani na mshikamano wetu tuliojijengea kwa muda mrefu sasa. Nawasihi pia viongozi wa dini waache kutumiwa vibaya.
 
Na muache kutukana dini humu jf kwani uchochezi ni mbaya na inatuuma sana, alilosema waziri si haki kabisa anajua fika yakitokea machafuko yeye na familia watakuwa wa kwanza kuikimbia nchi na kuaacha watu wafe nyuma,vita sio kitu cha kuomba, hivi wakijitenga wakawa na nchi atawabadilisha wawe wakristo? Hoja ya msingi ni kuwa bora suluhu ya hali ya juu kuliko kuchochea vita asiyoiweza, God help us
 
Hiyo ndiyo nyia ya mwongo ! Wamedanganya wananchi mwishowe wanaropoka yasiyoropokeka!!!
 
Hiyo ndiyo nyia ya mwongo ! Wamedanganya wananchi mwishowe wanaropoka yasiyoropokeka!!!

hawa wachochezi ni wa kuwaogopa kama ukoma. wanataka kuitumbukiza nchi kwenye mauaji ya kimbari.
 
ccm ndio wanafikiri hivyo ndio maana hadi leo kauli yake imeendelea kusimama kwa kuwa ni sawa alichokisema machoni pao na ndio msimamo wa ccm.
 
Kaka tatizo waislamu hamjazoea kuambiwa ukweli. Maelezo ya Lukuvi wote tumeyasikia bungeni na hayana tatizo lolote. Kwani nani haoni au hajui ubaguzi wa wazi unaofanywa na waislamu hapa Tanzania. Zipo nyumba za waislamu hawapangishi wakristo, baadhi ya mashirika ya uma kama NSSF sasa hivi kupata kazi kama sio muislamu ni tatizo...kisa Dau na Chiku Matesa. Ipo mifano mingi...achilia mbali kuhujumu ukristo huko Zanzibar ambapo wote sisi ni mashahidi. Mikutano ya waislamu kutukana ukristo hadharani tunaishuhudi kila uchao. Leo Lukuvi ana ubaya gani???? Tutoleeni ushenzi hapa!!!
 
Ubaguzi wa waislamu umeendekezwa na serikali sikivu ya ccm
 
Kaka tatizo waislamu hamjazoea kuambiwa ukweli. Maelezo ya Lukuvi wote tumeyasikia bungeni na hayana tatizo lolote. Kwani nani haoni au hajui ubaguzi wa wazi unaofanywa na waislamu hapa Tanzania. Zipo nyumba za waislamu hawapangishi wakristo, baadhi ya mashirika ya uma kama NSSF sasa hivi kupata kazi kama sio muislamu ni tatizo...kisa Dau na Chiku Matesa. Ipo mifano mingi...achilia mbali kuhujumu ukristo huko Zanzibar ambapo wote sisi ni mashahidi. Mikutano ya waislamu kutukana ukristo hadharani tunaishuhudi kila uchao. Leo Lukuvi ana ubaya gani???? Tutoleeni ushenzi hapa!!!

mkuu, unamaanisha kwamba lukuvi amewatukana waislamu kwa ajili ya kulipiza kisasi? unafurahia uchochezi huu wa lukuvi? think twice!
 
Kaka tatizo waislamu hamjazoea kuambiwa ukweli. Maelezo ya Lukuvi wote tumeyasikia bungeni na hayana tatizo lolote. Kwani nani haoni au hajui ubaguzi wa wazi unaofanywa na waislamu hapa Tanzania. Zipo nyumba za waislamu hawapangishi wakristo, baadhi ya mashirika ya uma kama NSSF sasa hivi kupata kazi kama sio muislamu ni tatizo...kisa Dau na Chiku Matesa. Ipo mifano mingi...achilia mbali kuhujumu ukristo huko Zanzibar ambapo wote sisi ni mashahidi. Mikutano ya waislamu kutukana ukristo hadharani tunaishuhudi kila uchao. Leo Lukuvi ana ubaya gani???? Tutoleeni ushenzi hapa!!!
Hayo unayoyasema ndo ticket ya ccm kutumia udini kuwavuruga watanzania????
 
Tangu zamani waislamu na wakristo tumekuwa tukiishi kama ndugu huku tukishirikiana katika mambo mbali mbali ya kimaisha lakini kuna baadhi ya watu ambao wanataka kutugombanisha kwa maslahi yao binafsi.

Kuna waziri mwandamizi ambaye amesikika hivi karibuni akiwabagua waislamu akiwa ndani ya kanisa na amerudia uchochezi wake akiwa bungeni Dodoma.

Kitendo cha kudai kwamba wazanzibar wanataka kujitenga ili kuifanya Zanzibar kuwa nchi ya kiislamu ikiwa serikali 3 zitapita, ni uchochezi unaolenga kuwadhalilisha, kuwachafua na kuwashushia hadhi waislamu mbele ya jamii. Aidha, kuwahusisha uamsho na chama cha siasa sio jambo la kulifumbia macho hata kidogo. Lengo lake ni kutaka kuwagombanisha waislamu na jamii. Na ni bahati mbaya maneno haya yametamkiwa ndani ya kanisa, kitendo ambacho kinalenga kujenga chuki kati ya waislamu na wakristo.

Jamani, tuwapuuze hawa wabaguzi kwani hawana nia njema na amani na mshikamano wetu tuliojijengea kwa muda mrefu sasa. Nawasihi pia viongozi wa dini waache kutumiwa vibaya.

fanya uchunguzi kwanza sio unatupa lawama tu bila kuchunguza kinachoongelewa kipo

-tafuta video pamoja na audio za hao unaowatetea usikie wanacho waubiria waumini wao
- tafuta maazimio waliyo yafikia miaka za themanini pale Khartoum Sudan naona utashawishika na kinacho endelea
- Najiulize kwa nini mmarekani anamwandama mwarabu sana utapata majibu ya huyu unaemwita mropokaji wa office ya raisi
-then jiulize kwa nini waislam walikataa kuesabiwa na kama tume wakitaka kuwaesabu wawaesabu wao na wakristo wenyewe jiuleze nini malengo yao
- kwanini kipindi kile cha buguruni vugu za kidini walitaka palipo na waislam wengi wakristo waame na wakakae palipo na wakristo wengi je? hauoni kunaukweli na akichokiongea
-hapo huyu mweshimiwa alikosea kufikisha ujumbe alikuwa hashi sana but ule ndio ulikuwa ukweli
 
Ukisema ukweli unaonekana mchochezi. Ukifuatilia mihadhara ya UHAMSHO ndio utajua Lukuvi anamaanisha nini. Nchi yoyote ikisha kuwa na waislam ni tatizo, ni wauwaji waliovaa koti la dini, mwamedi alikosea sana kuingiza mistari ya kuripiza visasi, chuki dhidi ya wasio wa imani yake, sijui aliemtuma ni nani
 
fanya uchunguzi kwanza sio unatupa lawama tu bila kuchunguza kinachoongelewa kipo

-tafuta video pamoja na audio za hao unaowatetea usikie wanacho waubiria waumini wao
- tafuta maazimio waliyo yafikia miaka za themanini pale Khartoum Sudan naona utashawishika na kinacho endelea
- Najiulize kwa nini mmarekani anamwandama mwarabu sana utapata majibu ya huyu unaemwita mropokaji wa office ya raisi
-then jiulize kwa nini waislam walikataa kuesabiwa na kama tume wakitaka kuwaesabu wawaesabu wao na wakristo wenyewe jiuleze nini malengo yao
- kwanini kipindi kile cha buguruni vugu za kidini walitaka palipo na waislam wengi wakristo waame na wakakae palipo na wakristo wengi je? hauoni kunaukweli na akichokiongea
-hapo huyu mweshimiwa alikosea kufikisha ujumbe alikuwa hashi sana but ule ndio ulikuwa ukweli

mkuu, bado sijakuelewa kabisa. ina maana wewe unamtetea lukuvi kwa kuwatukana waislamu akiwa ndani ya kanisa? wewe ni mchochezi, huna tofauti na lukuvi.
 
Likuvi ni Intarahamwe mwenye udini fasaha

ccm wako tayari kuwagawa watanzania kwa itikadi za kidini na ikibidi kuingia msituni ilmradi tu malengo yao yatimie. hao ndiyo intarahamwe na hizo ndizo tabia za kiintarahamwe---roho ya kumwaga damu, kuchinja na kula nyama za watu!
 
Nina mashaka kama kweli umemuelewa mwanzilishi wa huu uzi.

Anachocholalamikia yeye ni uchochezi wa wanasiasa kwa Watanzania wa kawaida.

Angalia sasa unavyotokwa na mapovu na ndio nyienyie mtakao kuja kushika mapanga baadaye wakati mwenzako Lukuvi yuko kwenye VX lenye kiyoyozi.
Na hapo mtakapo kuja kuchinjana mwenzenu analikwea pipa na kwenda kula bata nje.

Mungemwambia Lukuvi kuwa kama ana tatizo na Waislamu wa Zanzibar basi anajua wanapopatikana ataandaliwa mhadhara wa Waislamu watupu halafu yeye azungumze hayo maneno yake badala ya kauli zake za kichochezi bungeni za kuwaingiza waliomo na wasio kuwemo.
 
Nina mashaka kama kweli umemuelewa mwanzilishi wa huu uzi.

Anachocholalamikia yeye ni uchochezi wa wanasiasa kwa Watanzania wa kawaida.

Angalia sasa unavyotokwa na mapovu na ndio nyienyie mtakao kuja kushika mapanga baadaye wakati mwenzako Lukuvi yuko kwenye VX lenye kiyoyozi.
Na hapo mtakapo kuja kuchinjana mwenzenu analikwea pipa na kwenda kula bata nje.

Mungemwambia Lukuvi kuwa kama ana tatizo na Waislamu wa Zanzibar basi anajua wanapopatikana ataandaliwa mhadhara wa Waislamu watupu halafu yeye azungumze hayo maneno yake badala ya kauli zake za kichochezi bungeni za kuwaingiza waliomo na wasio kuwemo.

Lakini sio tu kwamba Lukuvi amewatukana waislamu per se bali anapowatukana waislamu akiwa ndani ya kanisa maana yake ni kwamba anajenga bifu kati ya wakristo na waislamu. waislamu watawachukia wakristo kwa kuwaruhusu wanasiasa kutumia makanisa kuukashfu uislamu. hapa ndipo vita ya kimbari itakapoanzia. lukuvi hapendi kuona watanzania tukiishi kwa amani ktk nchi hii
 
tangu zamani waislamu na wakristo tumekuwa tukiishi kama ndugu huku tukishirikiana katika mambo mbali mbali ya kimaisha lakini kuna baadhi ya watu ambao wanataka kutugombanisha kwa maslahi yao binafsi.

Kuna waziri mwandamizi ambaye amesikika hivi karibuni akiwabagua waislamu akiwa ndani ya kanisa na amerudia uchochezi wake akiwa bungeni dodoma.

Kitendo cha kudai kwamba wazanzibar wanataka kujitenga ili kuifanya zanzibar kuwa nchi ya kiislamu ikiwa serikali 3 zitapita, ni uchochezi unaolenga kuwadhalilisha, kuwachafua na kuwashushia hadhi waislamu mbele ya jamii. Aidha, kuwahusisha uamsho na chama cha siasa sio jambo la kulifumbia macho hata kidogo. Lengo lake ni kutaka kuwagombanisha waislamu na jamii. Na ni bahati mbaya maneno haya yametamkiwa ndani ya kanisa, kitendo ambacho kinalenga kujenga chuki kati ya waislamu na wakristo.

Jamani, tuwapuuze hawa wabaguzi kwani hawana nia njema na amani na mshikamano wetu tuliojijengea kwa muda mrefu sasa. Nawasihi pia viongozi wa dini waache kutumiwa vibaya.
lMh Lukuvi amekosea kusema aliyosema na mahali alipoyasemea.angeyasemea ndani ya bunge mjadala ungekuwa tofauti.hata hivyo katika hali ya sasa ni muhimu kuonyesha kwa vitendo kwamba hakuna sababu za raia yeyote kuwa na wasiwasi kwa tunaelekea kwenye sintofahamu.ili kufuta hali za wasiwasi ni muhimu kusema yafuatayo kwa wazi.
1)hakuna sababu yeyote ya kuingiza vifungu vyenye muelekeo wa kidini katika katiba ya muungano au ya washirika
2)jamhuri au nchi shirika zipinge kwa wazi matumizi au promotion ya sheria za kidini
3)siasa zifanywe na vyama vya kisiasa.ni vigumu kuelewa hali ambayo ngo ya kidini inaweza kujiingiza kwenye siasa moja kwa moja
4)haleweki kwa taasisi ya kijamii kupigia debe vitu kama kupinga sensa,upande mmoja ni koloni la uapande mwingine wa muungano,mwaasisi mmjawapo alihujumu imani fulani, upande mmoja wa muungano upate autonomy nk

mambo ya aina hii yasipopata nafasi na yakapingwa kwa nguvu na wazi mazingira ya hali ya wasiwasi yatatoweka yenyewe
 
mkuu, bado sijakuelewa kabisa. ina maana wewe unamtetea lukuvi kwa kuwatukana waislamu akiwa ndani ya kanisa? wewe ni mchochezi, huna tofauti na lukuvi.

Uchochezi uko wapi?mtu kuonyesha hofu yake ndio uchochezi?acheni kujidanganya kabisa kwani hiyo hofu ipo miongoni mwa watu wengi.Na hofu hiyo kwangu ndio inanifanya niamini kuwa serikali tatu ndo suluhisho pekee.Zanzibar wafanye watakavyotaka,wakiamua kuwahamisha watu wenye imani tofauti na yao basi wawahamishe.
 
Tatizo la watanzania huwa tuna kumbukumbu za kuchagua.
Mtoa mada aliwahi kulalamikia maneno ya jussa waliposhindwa uchaguzi uzini? au maneno ya Lipumba msikitini akiongelea gesi ya mtwara?
 
Watanzania hupenda kujiburudisha kwa maneno maneno ya mtaani.ukitaka ukweli google SIASA ZA UDINI TANZANIA usome mwenyewe
 
Back
Top Bottom