Ndugu wana JF, ni mejitahidi sana kunyamaza lakini sasa naona niongee maana najisikia kama vile moyo wangu unataka kuripuka kwa jinsi hali inavyoonekana. Kwanza kabisa napenda kutoa pole kwa wana-Arusha kwa tukio baya hili lililowapata. Pili nawapa pole CHADEMA kwa hili lililotokea katika mkutano wenu. Tatu natoa pole kwa watanzania makini ambao nia yao ni kuona Tanzania yenye amani ambayo inatoa haki kwa watu wote na wanaofaidi matunda ya uhuru wa Nchi yao.
Ndugu zangu, yapo mambo kadhaa ambayo inabidi wewe na mimi tujiulize. Hivi ni nani aliyepanga mpango wa Kurusha bomu katika mkutano waCHADEMA, na je ? Kunauhusiano wowote katika ya bomu la mkutano wa CHADEMA na lile la OLASITI? je CCM inahusika na jmabo hili au la?
Ndugu zangu, naomba nianzie kwenye hili la uhusiano wa bomu la mkutano wa CHADEMA na la OLASITI. Napenda watanzania niwafungue macho juu ya jambo hili. Kwanza mjue kuwa uchaguzi huu ulishapangiwa tarehe za kufanywa mapema hata kabla ya mlipuko wa pale Olasiti. Huku ikijulikana wazi kuwa Arusha ni ngome Kongwe ya CHADEMA na CCM inapahitaji sana , kumekuwa na mbinu za kila namna za chama Tawala CCM kuhakikisha inaimarisha hadhi yake katika jiji hili la Kitalii.
Kama ilivyo kawaida CCM inatabia ya kufanya tathimini ya mapema katika maeneo inahofia hata pale ambapo hakuna upinzani mkali maana haijiamini sana baada ya watu kuongezeka uelewa. Mahesabu yote yamekuwa yakionyesha wazi kuwa katika kata za Arusha CCM haina chake kabisa. Swali walilokuwa wanajiuliza ni namna gani CCM ishinde kata za ARUSHA?
Jibu lilipatikana: MBINU ILIYOTUMIKA MWAKA 1995 kwenye uchaguzi mkuu kwa JIJI LA DAR ES SALAAM lazima itumike kuhakikisha kuwa uchaguzi unahairishwa Arusha huku ikijiaminisha kushinda katika maeneo mengine. Hii ilipangwa kuwa baada ya matokeo ya maeneo mengine kutangazwa huku CCM ikijihakikishia Ushindi basi itawakatisha tamaa wakazi wa Arusha kwa kuona kuwa CHADEMA si kama walivyokuwa wanadhani kuwa inakubalika. Hii mbinu ilisaidia CCM kuchukua majimbo ya DAR baada ya watu kukatishwa tamaa na matokeo ya mikoa mingine. WENYE AKILI MNAELEWA.
Swali liliofuata ni je? tutafanyaje ili uchaguzi uhairishwe? Jibu lilipatikana kuwa ni kwa njia ya kuandaa mtadao utakao vaa sura ya ugaidi kwa kufanya mashambulizi ya mapema kabla ya uchaguzi ili litakapotokea ionekane kuwa ni mwendelezo wa matukio ya kigaidi katika jiji la Arusha. Mpango ulisukwa ukasukika, ndipo bomu la Olasiti lilionekana kuwa ndilo jibu huku wakijua kuwa yuko wa kubebeshwa lawama za awali yaani waislamu kutokana na matukio yaliyokwisha tangulia. Hii ndiyo maana mrusha bomu pamoja na kuwepo Polisi hakuweza kukamatwa. Ni mpango shirikishi wa CCM na POLISI.
Bomu la jumamosi lilikuwa nilakumamilisha mpango uliokusudiwa pale Arusha, ndiyo maana uchaguzi ulihairishwa kwa malengo maalum.
kwa wafuatiliaji wa mambo mtakubaliana na mimi kuwa mazingira ya bomu la Olasiti na la jumamosi kwenye mkutano wa CHADEMA yanafanana kabisa hasa kuhusu namna polisi kwa maana ya serikali inavyoshindwa kukamata mrushaji wa bomu. Hebu jiulize, kulikuwa na sababu gani Polisi kurusha mabomu ya machozi na hata kutumia risasi za moto zilizosababisha kifo badala ya kumkamata mhalifu.
WATANZANIA NAPENDA NIJIWEKE WAZI KUWA MIMI NI MWANA CCM KABISA ila naomba niwaweke wazi kuwa adui wa wawatanzania siyo chama kingine bali ni CCM yenyewe. Je ulishajiuliza swali hili? Hivi kwanini fujo utokea katika maeneo ambayo CCM inakozidiwa na siyo wapinzani wanakozidiwa? Itakuwa ajabu washabiki wa timu inayoongoza kwa mabao kurusha chupa au mawe uwanjani huku wakijua ushindi ni wao. Itakuwa ni jambo la ajabu watu wenye matumaini kuvuruga uchaguzi CCM ndiye mwanzirishi wa vurugu zote katika chaguzi.
CCM inahitaji kuadhibiwa kwa gharama zozote lakini si kwa kumwaga damu, kwanza ni kuhakikisha uchaguzi wa Arusha ukifanyika isipate kiti hata kimoja nawaomba na wana CCM mlioko Arusha msiichague CCM maana ni maadui wa maslahi ya watu na ustawi wao. Huu siyo wakati wa kufurahia vi t-shirt na vikofia na vilemba huku ndugu zetu wanakufa.
Baada ya Arusha, watanzania wote tujipange CCM iondoke madarakani ili wananchi wapate radha mpya ya utawala wenye malengo ya kuwakomboa watu na kujali maslahi ya watu.
ANAYEPINGA NA APINGE LAKINI NAWAACHIA SWALI HILI: KAMA UPINZANI ULIOPO SASA USINGE KUWEPO HALI YA TAIFA INGEKUWAJE?
Ndugu zangu, yapo mambo kadhaa ambayo inabidi wewe na mimi tujiulize. Hivi ni nani aliyepanga mpango wa Kurusha bomu katika mkutano waCHADEMA, na je ? Kunauhusiano wowote katika ya bomu la mkutano wa CHADEMA na lile la OLASITI? je CCM inahusika na jmabo hili au la?
Ndugu zangu, naomba nianzie kwenye hili la uhusiano wa bomu la mkutano wa CHADEMA na la OLASITI. Napenda watanzania niwafungue macho juu ya jambo hili. Kwanza mjue kuwa uchaguzi huu ulishapangiwa tarehe za kufanywa mapema hata kabla ya mlipuko wa pale Olasiti. Huku ikijulikana wazi kuwa Arusha ni ngome Kongwe ya CHADEMA na CCM inapahitaji sana , kumekuwa na mbinu za kila namna za chama Tawala CCM kuhakikisha inaimarisha hadhi yake katika jiji hili la Kitalii.
Kama ilivyo kawaida CCM inatabia ya kufanya tathimini ya mapema katika maeneo inahofia hata pale ambapo hakuna upinzani mkali maana haijiamini sana baada ya watu kuongezeka uelewa. Mahesabu yote yamekuwa yakionyesha wazi kuwa katika kata za Arusha CCM haina chake kabisa. Swali walilokuwa wanajiuliza ni namna gani CCM ishinde kata za ARUSHA?
Jibu lilipatikana: MBINU ILIYOTUMIKA MWAKA 1995 kwenye uchaguzi mkuu kwa JIJI LA DAR ES SALAAM lazima itumike kuhakikisha kuwa uchaguzi unahairishwa Arusha huku ikijiaminisha kushinda katika maeneo mengine. Hii ilipangwa kuwa baada ya matokeo ya maeneo mengine kutangazwa huku CCM ikijihakikishia Ushindi basi itawakatisha tamaa wakazi wa Arusha kwa kuona kuwa CHADEMA si kama walivyokuwa wanadhani kuwa inakubalika. Hii mbinu ilisaidia CCM kuchukua majimbo ya DAR baada ya watu kukatishwa tamaa na matokeo ya mikoa mingine. WENYE AKILI MNAELEWA.
Swali liliofuata ni je? tutafanyaje ili uchaguzi uhairishwe? Jibu lilipatikana kuwa ni kwa njia ya kuandaa mtadao utakao vaa sura ya ugaidi kwa kufanya mashambulizi ya mapema kabla ya uchaguzi ili litakapotokea ionekane kuwa ni mwendelezo wa matukio ya kigaidi katika jiji la Arusha. Mpango ulisukwa ukasukika, ndipo bomu la Olasiti lilionekana kuwa ndilo jibu huku wakijua kuwa yuko wa kubebeshwa lawama za awali yaani waislamu kutokana na matukio yaliyokwisha tangulia. Hii ndiyo maana mrusha bomu pamoja na kuwepo Polisi hakuweza kukamatwa. Ni mpango shirikishi wa CCM na POLISI.
Bomu la jumamosi lilikuwa nilakumamilisha mpango uliokusudiwa pale Arusha, ndiyo maana uchaguzi ulihairishwa kwa malengo maalum.
kwa wafuatiliaji wa mambo mtakubaliana na mimi kuwa mazingira ya bomu la Olasiti na la jumamosi kwenye mkutano wa CHADEMA yanafanana kabisa hasa kuhusu namna polisi kwa maana ya serikali inavyoshindwa kukamata mrushaji wa bomu. Hebu jiulize, kulikuwa na sababu gani Polisi kurusha mabomu ya machozi na hata kutumia risasi za moto zilizosababisha kifo badala ya kumkamata mhalifu.
WATANZANIA NAPENDA NIJIWEKE WAZI KUWA MIMI NI MWANA CCM KABISA ila naomba niwaweke wazi kuwa adui wa wawatanzania siyo chama kingine bali ni CCM yenyewe. Je ulishajiuliza swali hili? Hivi kwanini fujo utokea katika maeneo ambayo CCM inakozidiwa na siyo wapinzani wanakozidiwa? Itakuwa ajabu washabiki wa timu inayoongoza kwa mabao kurusha chupa au mawe uwanjani huku wakijua ushindi ni wao. Itakuwa ni jambo la ajabu watu wenye matumaini kuvuruga uchaguzi CCM ndiye mwanzirishi wa vurugu zote katika chaguzi.
CCM inahitaji kuadhibiwa kwa gharama zozote lakini si kwa kumwaga damu, kwanza ni kuhakikisha uchaguzi wa Arusha ukifanyika isipate kiti hata kimoja nawaomba na wana CCM mlioko Arusha msiichague CCM maana ni maadui wa maslahi ya watu na ustawi wao. Huu siyo wakati wa kufurahia vi t-shirt na vikofia na vilemba huku ndugu zetu wanakufa.
Baada ya Arusha, watanzania wote tujipange CCM iondoke madarakani ili wananchi wapate radha mpya ya utawala wenye malengo ya kuwakomboa watu na kujali maslahi ya watu.
ANAYEPINGA NA APINGE LAKINI NAWAACHIA SWALI HILI: KAMA UPINZANI ULIOPO SASA USINGE KUWEPO HALI YA TAIFA INGEKUWAJE?