Huu ndio ubabaishaji wa G4S (Kampuni ya Ulinzi)

frontpage

Member
Feb 26, 2017
71
113
G4S SECURE SOLUTION ni kampuni kubwa inayojishughulisha na shughuli mbalimbali za kiulinzi, Ndiyo kampuni inayolinda ubalozi wa U.S.A kwa hapa Tanzania, ndiyo inayolinda mgodi wa ACACIA geita na Nyamongo, mbali na maeneo niliyoyataja kuna mengine mengi.
.
Kampuni hii imekuwa ikiendeshwa kihuni sana, mikataba yao kwa wateja wao ni ya kiubabaishaji sana ukizingatia na gharama kubwa wanazozitoza kwa wanaoingia mikataba nao.
.
Nianze na mikataba:-
G4S SECURE SOLUTION wamekuwa wakiwatoza wateja wao gharama kubwa ukiliganisha na huduma wanazozitoa ni za kibabaishaji. Unakuta mteja anailipa kampuni hiyo milioni 2 kwa askari mmoja kwa mwezi lakini wao wanamlipa laki moja na nusu mfanyakazi anayefanya kazi hiyo ukijumuisha na over time inafika laki mbili na nusu, hivi kwa malipo hayo unadhani kuna kazi ama mzaha?, mteja hana usalama wowote maana mfanyakazi anakuwa hajalipwa inavyostahili hivyo ufanisi wa kazi haupo.
.
Pili wafanyakazi wanadhulumiwa pasipo kuwa na mahala pa kuzungumzia:-
Katika hili niseme limekuwa sugu sana, wao wanalipa kwa mfumo wa masaa, lakini masaa yao hufikia wakati hayako sawa kama mfanyakazi alivyofanya kazi zake kwa mwezi mzima, wanachokifanya ni kuiba masaa 20 hadi 30 kwa kila mfanyakazi na kuyaingiza mfuko wa wajanja kwa manufaa yao walio na jukumu la masaa na kulipa pesa za mishahara..... ushahidi upo maana ni malalamiko mengi yametolewa kwao na wafanyakazi kuahidiwa kuingiziwa kiasi hicho mwezi utakaofuata na hakuna litakalofanyiwa kazi.
.
Wafanyakazi wamekuwa wakifukuzwa kiholela pasipo utaratibu wa kisheria kwa kujivunia kwamba walimnunua mwanasheria aliyekuwa akifanya kazi mahakama ya kazi aitwa NEEMA, hivyo hata kama utaenda kuishtaki kampuni hutoweza kusimama na kumshinda mwanasheria huyo maana anafahamiana na idara nzima pale mahakama ya kazi, kesi nyingi za kampuni hiyo zimeishia kuwekwa kapuni na kupigwa kalenda.
.
Unyanyasaji wa kingono:-
Kampuni hii imekuwa chanzo cha kuvuruga ndoto za mabinti wengi kwa kupewa mimba na viongozi wao kwa kigezo cha kupangiwa mahala pasipo na usumbufu wa kazi nyingi, RUSHWA YA NGONO imepelekea mabinti wengi karibu 80% ya wanaofanya kazi kampuni hiyo ya G4S SECURE SOLUTION kuzalishwa na kutelekezewa watoto.
.
Kupitia uzi huu wahusika wa haki za wafanyakazi na haki na kibinadamu walifanyie kazi jambo hili linaloendelea ndani ya kampuni hii, Ubabaishaji kama huu umepelekea kampuni hii kuvunjiwa mikataba katika maeneo mengi waliyokuwa wakifanya kazi, hii ni pamoja na:-
.
*DANGOTE CEMENT MTWARA Hapa ulifanyika wizi mkubwa wa mashine ya karibu milioni 200 na wakasitishiwa mkataba kwa kushindwa kudhibiti usalama maana ulifanyika ushirikiano wao kutekeleza jambo hilo.
.
*HOTELI ZA KITALII ZANZIBAR hapa walitakiwa wawaongezee wafanyakazi mishahara kwa kanuni za zanzibar na matakwa ya mteja lakini wao waligomea wakitaka ongezeko la pesa kutoka kwa mteja.Malipo ya mteja ni milioni moja na nusu, mfanyakazi alilipwa laki na nusu, hebu angalia tofauti iliyopo hapo.
.
*MGODI WA ACACIA hawa waliwataka G4S waongeze mshahara wafanyakazi hadi laki 8 kutoka laki 4 maana wao ACACIA hulipa milioni mbili na nusu 2,500,000 kwa askari mmoja mshika bunduki, wao G4S waligomea na kuona ni hasara kutekeleza hilo na mkataba hautoendelea baada ya mwezi huu wa April maana ACACIA waiona ni upuuzi. Huwezi kulipwa malipo makubwa na anayehusika na kazi ukambinya kiasi hicho.
.
Kiujumla kampuni hii imekuwa ikinyonya na kukandamiza maslahi ya wafanyakazi pasipo na woga wala hofu ya kuiogopa serikali ya Jamuhuri ya Tanzania.
.
Endapo watashindwa kuyafanyia kazi haya ndani ya muda mfupi swala hili litazidi kuanikwa katika taswira za kimataifa zaidi.
 
Kwaio wale jamaa wanao escort madini toka Mwanza mpaka Dar kwa ndege wanalipwa 400k
 
Wakati naingia dar rasmi kwa kusaka tonge 2014 Agosti nikajikuta naingia kwenye kampuni hii ya kimataifa iliyojaa unyonyaji.
Nilipangiwa Bulyanhulu baada ya kozi fupi.
Niliacha baada ya muda mfupi.
Ukiwa una roho ya utawala(Kifalme) huwezi kukubali kunyonywa na wapuuzi.
Kampuni zote za ulinzi Tz na zile zote zinazoact kama agents au zile ambazo clients walipe then wamlipe mfanyakazi wao ni upuuuuuuuzi mtupu.
 
Naskia G4S wanalipa wafanyakazi wao kwa M-Pesa sababu hawajawasainisha mkataba ni kweli?
Zinalipwa kupitia akauti za bank na hata mapungufu utakayo yabaini usiulize, maana hata uulize utapewa karatasi uandike malalamiko yako ya mapungufu kuligana na masaa yako ya kazi, lakini yote hayo itaishia mezani kupigwa vumbi na hakuna utakachoambulia.
 
Ila mkuu mimi huwa nawalaumu sana wa Tz wezangu maana unakuta mtu anamfundisha mgeni namna ya kutunyonya ndugu zake kwasababu anajua fika wengi wetu hatuzijui haki zetu, Badala awatetee watanzania yeye yupo bize kuona unakandamizwa tu tubadilike kwanza sisi wenyewe tuwe wazalendo.
 
Kifupi tuachane na hii dhana ya kuajiriwa. Tujikite zaidi na tujiongeze tujiajiri wenyewe. Chukua hatua inawezekana
 
Kumbe Mola alininusuru maana kidogo waniajiri sema tukashindwana kitu kidogo sana na aliyeniunganisha nikasitisha zoezi
 
Wakati naingia dar rasmi kwa kusaka tonge 2014 Agosti nikajikuta naingia kwenye kampuni hii ya kimataifa iliyojaa unyonyaji.
Nilipangiwa Bulyanhulu baada ya kozi fupi.
Niliacha baada ya muda mfupi.
Ukiwa una roho ya utawala(Kifalme) huwezi kukubali kunyonywa na wapuuzi.
Kampuni zote za ulinzi Tz na zile zote zinazoact kama agents au zile ambazo clients walipe then wamlipe mfanyakazi wao ni upuuuuuuuzi mtupu.
Wakati mwingine mnaweza mkawa mnalaumu hizo kampuni za ulinzi wakati tatizo ni serikali/CCM yenu !
- PoliCCM wanalipwa kiasi gani, je Mlinzi unaweza kulipwa kuliko polisi ?
 
Pata suluhisho LA ulinzi fika suma jkt upate ufumbuzi
Nyie Suma mnawatesa vijana, hata basic ya serikali hamuizingatii kwa wafanyakazi wenu.
Mnamlipa kijana fedha ambayo kijana ataendelea kuwa maskini kila leo.
Pia vijana wenu hamuwapi masomo ya costomer care. Wako sharrow sana, wanajisahau kuwa wao ni watoa huduma badala yake wanajiona wako vitani kila muda.
 
G4S SECURE SOLUTION ni kampuni kubwa inayojishughulisha na shughuli mbalimbali za kiulinzi, Ndiyo kampuni inayolinda ubalozi wa U.S.A kwa hapa Tanzania, ndiyo inayolinda mgodi wa ACACIA geita na Nyamongo, mbali na maeneo niliyoyataja kuna mengine mengi.
.
Kampuni hii imekuwa ikiendeshwa kihuni sana, mikataba yao kwa wateja wao ni ya kiubabaishaji sana ukizingatia na gharama kubwa wanazozitoza kwa wanaoingia mikataba nao.
.
Nianze na mikataba:-
G4S SECURE SOLUTION wamekuwa wakiwatoza wateja wao gharama kubwa ukiliganisha na huduma wanazozitoa ni za kibabaishaji. Unakuta mteja anailipa kampuni hiyo milioni 2 kwa askari mmoja kwa mwezi lakini wao wanamlipa laki moja na nusu mfanyakazi anayefanya kazi hiyo ukijumuisha na over time inafika laki mbili na nusu, hivi kwa malipo hayo unadhani kuna kazi ama mzaha?, mteja hana usalama wowote maana mfanyakazi anakuwa hajalipwa inavyostahili hivyo ufanisi wa kazi haupo.
.
Pili wafanyakazi wanadhulumiwa pasipo kuwa na mahala pa kuzungumzia:-
Katika hili niseme limekuwa sugu sana, wao wanalipa kwa mfumo wa masaa, lakini masaa yao hufikia wakati hayako sawa kama mfanyakazi alivyofanya kazi zake kwa mwezi mzima, wanachokifanya ni kuiba masaa 20 hadi 30 kwa kila mfanyakazi na kuyaingiza mfuko wa wajanja kwa manufaa yao walio na jukumu la masaa na kulipa pesa za mishahara..... ushahidi upo maana ni malalamiko mengi yametolewa kwao na wafanyakazi kuahidiwa kuingiziwa kiasi hicho mwezi utakaofuata na hakuna litakalofanyiwa kazi.
.
Wafanyakazi wamekuwa wakifukuzwa kiholela pasipo utaratibu wa kisheria kwa kujivunia kwamba walimnunua mwanasheria aliyekuwa akifanya kazi mahakama ya kazi aitwa NEEMA, hivyo hata kama utaenda kuishtaki kampuni hutoweza kusimama na kumshinda mwanasheria huyo maana anafahamiana na idara nzima pale mahakama ya kazi, kesi nyingi za kampuni hiyo zimeishia kuwekwa kapuni na kupigwa kalenda.
.
Unyanyasaji wa kingono:-
Kampuni hii imekuwa chanzo cha kuvuruga ndoto za mabinti wengi kwa kupewa mimba na viongozi wao kwa kigezo cha kupangiwa mahala pasipo na usumbufu wa kazi nyingi, RUSHWA YA NGONO imepelekea mabinti wengi karibu 80% ya wanaofanya kazi kampuni hiyo ya G4S SECURE SOLUTION kuzalishwa na kutelekezewa watoto.
.
Kupitia uzi huu wahusika wa haki za wafanyakazi na haki na kibinadamu walifanyie kazi jambo hili linaloendelea ndani ya kampuni hii, Ubabaishaji kama huu umepelekea kampuni hii kuvunjiwa mikataba katika maeneo mengi waliyokuwa wakifanya kazi, hii ni pamoja na:-
.
*DANGOTE CEMENT MTWARA Hapa ulifanyika wizi mkubwa wa mashine ya karibu milioni 200 na wakasitishiwa mkataba kwa kushindwa kudhibiti usalama maana ulifanyika ushirikiano wao kutekeleza jambo hilo.
.
*HOTELI ZA KITALII ZANZIBAR hapa walitakiwa wawaongezee wafanyakazi mishahara kwa kanuni za zanzibar na matakwa ya mteja lakini wao waligomea wakitaka ongezeko la pesa kutoka kwa mteja.Malipo ya mteja ni milioni moja na nusu, mfanyakazi alilipwa laki na nusu, hebu angalia tofauti iliyopo hapo.
.
*MGODI WA ACACIA hawa waliwataka G4S waongeze mshahara wafanyakazi hadi laki 8 kutoka laki 4 maana wao ACACIA hulipa milioni mbili na nusu 2,500,000 kwa askari mmoja mshika bunduki, wao G4S waligomea na kuona ni hasara kutekeleza hilo na mkataba hautoendelea baada ya mwezi huu wa April maana ACACIA waiona ni upuuzi. Huwezi kulipwa malipo makubwa na anayehusika na kazi ukambinya kiasi hicho.
.
Kiujumla kampuni hii imekuwa ikinyonya na kukandamiza maslahi ya wafanyakazi pasipo na woga wala hofu ya kuiogopa serikali ya Jamuhuri ya Tanzania.
.
Endapo watashindwa kuyafanyia kazi haya ndani ya muda mfupi swala hili litazidi kuanikwa katika taswira za kimataifa zaidi.
Njoo DM mkuu,tuongezee nyama jambo lifike kwenyewe
 
Wahanga WaPo wengi wanaokimbizana na masaaa kwa kweli usipojua haki yako utanyonywa mpaka kufa na ujue hiii ni Kampuni hovyo Kabisa haiwajali wafanyakazi wake....
Ila kila kitu kina mwisho , Ukilinganisha na Kenya South Africa na Nigeria kiukweli utaona tofauti kubwa kwa watu wake kiuchumi.
 
Hilo kampuni la G4S mmiliki wake ni mzawa?
Nauliza tu!
Lakini ndugu zangu wana JF njaa haivumiliki. Katika nyakati kama hizi Kijana unapata kazi hapo G4S ati watakulipa laki 4 utakataaa?
Ni ngumu kukataa kwasababu una shida.
Wanafanya unyonyaji wote huo kwasababu Wewe ni mnyonge, na wanajua huna namna ya Kufanya kukuwezesha uishi; Isipokuwa kwa kibarua chao.
Pamoja na Changamoto zote hizo ambazo umeweka wazi, bado kuna watu wengi wanapeleka barua za maombi ya kazi.
Tumeambiwa tufanye kazi.
 
Back
Top Bottom