Jukwaa hili lililenga zaidi kuiimarisha jamii kwenye masuala ya ndoa, uchumba au mahusiano. Rakini ukisoma asilimia zaidi ya 90 ya thread humu zianachochea, zinashawishi na kusifia uzinzi, uasherati, usaliti katika mahusiano na kadharika kinyume na lengo la kuanzishwa kwake.
Sidhani kama kuna mtu kati yetu humu ambaye anaweza kumkubalia mke, mume, mchumba au mpenzi wake ajiunge na jukwaa hili kirahisi kutokana na mambo yalivyo humu. Humu hakumjengi mtu kuwa mke, au mume bora.
Tumeliharibu jukwaa limekuwa kitu kingine kabisaa, mambo mengi humu ni ya kijinga kuliko ya kujenga.
Naomba kuwasilisha
Sidhani kama kuna mtu kati yetu humu ambaye anaweza kumkubalia mke, mume, mchumba au mpenzi wake ajiunge na jukwaa hili kirahisi kutokana na mambo yalivyo humu. Humu hakumjengi mtu kuwa mke, au mume bora.
Tumeliharibu jukwaa limekuwa kitu kingine kabisaa, mambo mengi humu ni ya kijinga kuliko ya kujenga.
Naomba kuwasilisha