SAGAI GALGANO
JF-Expert Member
- Nov 13, 2009
- 50,081
- 75,445
CCM bila msaada wa polisi hawana chao, si mnaona wanaomba msaada wa polisi wawazuie Chadema wasidhibiti wizi wa kuara.
Haya ni Matokeo Chana ya Kutotatua changamoto, zingine za makusudi zinazo Tokea Kwenye Chaguzi zetu Itafika Mahala Watu Wataitafuta Haki kwa Mtutu Wa Bunduki ama kwa Mapanga Shaaa! Hivi Hatujifunzi Kwa Yanayo Tokea DRC ? We Need a Free and Fair Elections, 'Say No For Greedy Leadership'Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amefunguka na kulitaka jeshi la polisi kuhakikisha Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hakilindi kura kwani hilo si jukumu lao.
![]()
Polepole amesema hayo leo Februari 15, 2018 wakati akiongea na waandishi wa habari kuelekea uchaguzi mdogo wa Ubunge na nafasi za udiwani ambao unatarajia kufanyika Februari 17 2018 na kudai kuwa mpaka sasa wamepata taarifa kuwa CHADEMA wanachukua watu kutoka mikoani kuja kulinda kura kitu ambacho hakikubaliki.
"Zipo nyumba kadhaa hapa Dar es Salaam ambazo zimehifadhi watu wasio wakazi wametoka mikoa mbalimbali kuja hapa kwa kigezo cha kulinda kura, sisi hatufanyi siasa za matukio wala kutafuta kiki baada ya kujua hili tumewajulisha jeshi la polisi juu ya nyumba hizo na watu hao, kitakachofuata ni kushugulika na watu hao ambao hawapendi utaratibu mzuri na desturi yetu nzuri ya uchaguzi"
Polepole aliendelea kusema kuwa
"Kura hazilindwi na watu wanaoletwa kwa makundi bali kura kwa mujibu wa Katiba, Sheria ya uchaguzi na kanuni mbalimbali za uchaguzi zimewekewa utaratibu wa kisheria kuhakikisha mwenye yake na anaipata hiyo, upo utaratibu wa mawakala kila chama kina wakala huyo ndiye atakayeshiriki kuhesabu, kujua hii kura yangu au si yangu sasa unapoanza kuandaa watu wasiojulikana na kuwaleta Dar es Salaam ni kuleta taharuki na mpango huo msingi wake ni kutisha wakina mama, vijana na wazee wasijitokeze kwenda kupiga kura, tumesema jeshi la polisi tafadhali tena tafadhali sana watu wasiohusika na usimamizi wa zoezi la uchaguzi ni sheria hawapaswi kuwepo wanatakiwa kuwepo kwenye maeneo yao wakafanye kazi zao za kujiletea kipato, uchaguzi haulindwi na mabaunsa, kura hailindwi bali dola ina vyombo vyake ambavyo sisi wote vyama vya siasa tumekubaliana" alisisitiza Polepole
My take:
Hapa naona polepole kaanza kucheza na akili za chadema huu uchaguzi hauko vizur kwa upande wa ccm wanahangaika sana washakabwa.
Kisheria Kazi ya kulinda kura ni ya wakala aliye chumba cha kura huko nje wanalinda nini? Hizo ni kazi za mawakala wa chadema au hawawaamiini?
Ushindi ni ushindi uwe goli la mkono wote ushindiTuliwaambia kwamba hamkubaliki mnalazimisha, sijui mnataja miradi ya maendeleo mkidhani watu watawakubali. Mkajifanya kununua viongozi ili muonekane mnakubalika, lakini saa hii kila mtu anawaona mnavyolazimisha kushinda uchaguzi kwa mauaji na ukatili wa kila aina. Zile kelele za kutamba kwa ushindi wakati cdm wamesusia uchaguzi ndio niliwapuuza kishenzi, toka lini ufunge goli lililowazi kisha ushangalie kama sio mwendawazimu.
Umma uliokuwa hauamini kwamba ccm huwa wanashinda kimizengwe na ukatili saa hii wanashuhudia kila mnachokifanya.
Ushindi ni ushindi uwe goli la mkono wote ushindi
Polepole na chama chenu acheni wananchi wa Kinondoni waamue ya nini kusumbukaaa?!
Karibu sanduku la kura karibu sana tukutane kesho kutwa uone mziki wa CCM baada ya matokeo nakungoja hapa jamii forums ila ushauri wa bure uwe na namba karibu ya daktari wako wa magonjwa ya presha usije kutufia tukakosa mchangia mada jamii forums kwa kufariki kwa presha baada ya mshituko wa tangazo la matokeo ya uchaguziNimeshukuru cdm wameamua kushiriki na kudhibitishia umma kwamba ndio chama kinachokubalika. Sasa ni dhahiri ccm inang'ang'ania madaraka na wala haikubaliki. Lengo kubwa la kushiriki cdm kwa sasa ilikuwa ni kuweka rekodi sawa kwamba ccm haikubaliki. Jengeni SGR, sambazeni maji, jengeni barabara, nunueni viongozi wa upinzani lakin umma hauwakubali. Hamna kitu kigumu kama kulamisha kuvuta riziki kwa kamba.
Mkwala kokoNyie magamba leteni uduwanzi wenu, safari hii mtaonana na muumba kwa njia rahisi sana.
Karibu sanduku la kura karibu sana tukutane kesho kutwa uone mziki wa CCM baada ya matokeo nakungoja hapa jamii forums ila ushauri wa bure uwe na namba karibu ya daktari wako wa magonjwa ya presha usije kutufia tukakosa mchangia mada jamii forums kwa kufariki kwa presha baada ya mshituko wa tangazo la matokeo ya uchaguzi