Tangu dunia iumbwe ukweli haujawahi kuwa na sifa ya uongo,ukweli hauwezi kuwa uongo wala uongi haujawahi kuwa ukweli,sababu uongo ni kinyume cha ukweli.
Ni makosa ukweli kuupa au kuuarifisha kwa tamko "dhana" sababu ukweli ni hali halisi.
Nilichokiona kwako na ndio ukweli wenyewe ni kushindwa kwako kuonyesha ukweli wa hizo habari. Sifa moja miongoni mwa sifa za ukweli ni kuwa unamea popote,hauhitajiki kuwa smart sana kama unavyodai ili kuzielewa habari hizo. Habari kwa zenyewe zina ukakasi seuze kueleweka ?
Huu nakupa mfano rahisi sana,ukweli kuhusu uwepo wako kamwe hauwezi kuwa uongo wa kutokuwepo maadamu ni kweli wewe upo,unaishi.
Lakini swali langu rahisi sana,nililo uliza ni kupata uhakika wa ukweli juu ya habari hizi,hili halihitaji nguvu hata kidogo.
Nipo .....