Umeshawahi kujiuliza hivi ubongo wa binadamu na computer kipi kina uwezo Zaidi?, basi hili swali ni moja ya swali maarufu sana ambalo wanazuoni wengi wamekuwa wakijiuliza na kulifanyia utafiti, kwa miaka mingi.
Wengine wamejaribu kulimit comparison katika Nyanja nne ambazo ni ,
- Energy efficiency
- Storage
- Memory
- And processing speed.
- Lakini leo tutaenda Zaidi ya hapo.
Umeshawahi kujipima uwezo wako wa akili na computer? Inawezekana jibu ni ndio, labda ulijaribu kujipa hesabu ndogo ili uone wewe na computer nani atatoa jibu haraka na computer ikakushinda, (hahaha), Ukichukua computer na ubongo wa bunadamu kwa haraka, utaona computer ni smart na inaspeed Zaidi ya ubongo, naam hii huifanya computer ionekane inauwezo Zaidi, lakini kuna mengi Zaidi nyuma ya stori hii, na ukweli ni kwamba ubongo wa binadamu unauwezo maradufu ya “ large contemporary super computer’’
Chukua porpcorn zako weka pozi zuri.
Kiwango cha nishati kinachoweza kukotolewa kutoka kwenye “fastest super computer” inayofanyakazi, kinaweza kutumika kuwasha jingo zima la kawaida, lakini ubongo unaweza kufanya kazi sawa na hiyo computer kwa kutumia nishati kidogo tu inayoweza kuwasha balbu inayofifia.
Kompyuta ya kawaida hutumia takriban wati 100 za nguvu. Ubongo wa binadamu, kwa upande mwingine, unahitaji takriban wati 10. Hivyo ni kweli, ubongo wako unatumia nishati mara kumi zaidi ya kompyuta. Ubongo unahitaji nguvu kidogo kuliko balbu.
Na tofauti kubwa ya kwanza kati ya ubongo na computer ni kwamba, ubongo unatumia glucose lakini computer inatumia umeme kwa upande wa nishati ( energy)
Makadirio hutofautiana kulingana na seli ngapi za neva, au niuroni, ziko katika ubongo wa kawaida. Tafiti nyingi zimekadiria ubongo unaweza kuwa na niuroni bilioni 100, wakati utafiti wa Chuo Kikuu cha Stanford unakadiria kuwa ubongo kweli una niuroni bilioni 200.
Unaweza kuwa unafikiria, "hapa utalinganisha vipi?, kompyuta ina byte na ubongo una niuroni. Tunawezaje kulinganisha hizi mbili?"
Twende sasa.
Tofauti moja kubwa kati ya ubongo wa binadamu na flash memory ya kompyuta ni uwezo wa niuroni kuchanganyikana yaani (storage na memory vimeungana). Kila neuroni ina takribani miunganisho elfu moja kwa niuroni zingine. Kwa miunganisho zaidi ya trilioni katika ubongo wa wastani wa binadamu, athari hii ya mwingiliano huunda uwezo mkubwa zaidi wa kuhifadhi.
Kulingana na uelewa wetu wa niuroni leo, ambao ni mdogo sana, tunaweza kukadiria uwezo wa kuhifadhi wa ubongo katika petabyte 1, ambayo inaweza kuwa sawa na zaidi ya SSD 1TB elfu, yaani kwa lugha nyingine GB million.
Tumalizie uzi huu, kwenye hii site hapa
HUMAN BRAIN VS COMPUTER