Hukumu ya bomoabomoa kutolewa saa nane

Hukumu ya bomoabomoa kutolewa saa nane

Status
Not open for further replies.
Chipolopolo 2 naona unatimiza usemi usemao aliyeshiba hamjui mwenye njaa.
Naunga mkono bomoabomoa lakini serikali mpya ingetoa angalau miezi mitatu kwa kuzingatia yafuatayo;
Kipato cha wakaazi, watoto,wazee,wagonjwa na elimu ya wanafunzi kushindwa kuhudhuriwa shule iwapo watakosa makazi
 
Hivi kati ya mafuriko na kubomolewa kipi chenye athari kubwa
Mafuriko huja bila taaarifa na hayana muda yaweza tokea usiku watu wamelala na bomao inakuarifu na unaona mwenziao kinamemkuta
Saaa katika hali hii kipi kinanafuu kiliko kingine
Tuone jibu la mahakama
 
Tangu uchaguzi uishe hakuna lolote lililofanyika zaidi ya fukuzafukuza,ziara za kushtukiza,matamko na bomoabomoa!
 
Hukumu itende haki wananchi wapewe haki zao hii nchi lazima iendeshwe kwa sheria na taratibu nasi kuendesha nchi kwa kaulimbiu ya chama.
 
Wanao bomolewa sio wote waliojenga mabondeni hata wale waliojenga kwenye open space nawenyewe wanabomolewa tatizo city plan map ilikuwa haitolewi hivyo mtu akinunua kiwanja nafatilia ardhi na ramani na title ya kiwanja chake anapewa ss hapo mwenye kosa ni nani mnunuzi au mtoa title ya kiwanja??

Pale salender kwa nyuma ilipokuwa ubalozi wa marekani wa muda baada ya kulipuliwa ule wa zamani zile nyumba ziko kwenye mkondo wa maji nazenyewe nimeona baadhi zimepigwa X kwa mbele anakaa Mzee Mengi na jirani yake alikuwaga ni Azim Dewji sijui kma bado anaishi pale ila kuna mahekalu kule ya kufa mtu na kipindi cha mvua ni kweli huwa maji yanajaa haswa. Wakitaka tuone haki inatendeka wasitishe kule kwa walalahoi waanze haya mahekalu ya vibopa wakisha maliza kuzibomoa warudi kwa walalahoi tujue haki imetendeka na msumeno unakata kotekote
 
Kwa majira ya Tanzania hivi sasa ni saa 9 na dk 25 , bado hukumu haijatolewa ?
 
Watanzania tuache kulalamika kwa kila jambo jamani hawa watu wamejenga mabondeni na ndo wanasababisha mafuriko kila siku. Na hao matajiri kumbukeni wengi wao sio kwamba wamejenga mabondeni wengi wao ni kwamba kwenye viwanja vyao ni kwamba wakuta wameongeza uwanja so at the end of the day wakuta ukuta tu ndo wavunjwa. Watanzania mnaomba mvua mkipewa mvua mwataka jua.
 
Siogopi ila siielewi.....mie nilipo hainikuti,ila nyumba yetu ya magomeni sijui kama itapona.
Magomeni kwa upande gani? Ni kama washapita.. ila kama ni huu upande unaopakana na Kigogo bado hawajapiga X
 
Magari ya Bomoa Bomoa toka Mawili (2) Hadi Manne (4), Yanaendelea Kupiga kazi Mkwajuni tena Chini ya Ulinzi wa Kutosha...Ndg zangu Amenii tu.
 
Uwe unatumia akili kabla ya kulinganisha mambo.
Utofauti upo wapi hapo? Au bahari ya zanzibari na pwani zake hazipati athari kama hizi zilizoko huku Tanganyika? Akili za watu wa CCM zingekuwepo wakati mji wa Venice unajengwa wala usingejengwa!!
 
Waondolewe tu make hao hao kila mwaka utangaziwa wahame na hawataki alafu leo eti wanaomba waongezewe muda, ni muda kiasi wanataka miaka yote wanaambiwa hawataki kuhama wanajifanya ndo wajanja wa mjini? waandolewe tu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom