Hukumu ya bomoabomoa kutolewa saa nane

Hukumu ya bomoabomoa kutolewa saa nane

Status
Not open for further replies.
Bomoabomoa iwaguse wote,hata matajir walionan ya mita 60


Well said! Muhimu tuone kweli utekelezaji haubagui masskini na matajiri. Vinginevyo pamoja na kuwa zoezi zima ni halali, tutakuwa tumelenga kusomeshana namba tu!
 
Hii tabia ya kuona sisi tuliokwenda kujenga kilungule, kajiungeni, makabe n.k kuwa ni washamba na wao ni wajanja wa mjini ndo wakome kabisa. Si kweli kuwa uhaba wa viwanja ulisababisha watu kujenga kwenye mito, bali ni kutopenda kukaa pembeni mwa mji. Mtu unasema umekuwepo jangwani karibu miaka 20 iliyoppita, wakati kipindi hicho kulikuwa na maeneo mengi nje kidogo ya mji kama vile Mbezi, Segerea, Bunju n.k ambayo ni salama. Na kwa ushahidi wengi waliopata viwanja mabwepande na Mbweni (eneo la Ubungo) waliishia kuviuza au kuvitelekeza.
 
Mpango miji itakuja mpaka huku kwenu kilungule, kajiungeni, makabe,...... Na kwengine kote ambapo bado tunajenga kwa kukomoana
 
Kutokana na kuwepo baadhi ya nyumba ambazo zimejengwa kwenye maeneo hatarishi yakiwemo ya kwenye kingo za mito pamoja na bahari hususani kwenye eneo la mto msimbazi nyumba ambazo zipo pembezoni mwa mto msimbazi kwa umbali wa Mita 60; Kwa muda mrefu serikali ikitoa fidia na hifadhi kwa watu wa mabondeni kutokana kusombwa na mafuriko.

Na hali hiyo ilisababisha serikali kutoa viwanja katika eneo la Mabwepande kwa wakazi waliokuwa mabondeni. Na baadhi yao walihama lakini wengine waliendelea kusalia kwenye maeneo hayo ambapo wiki mbili zilizopita serikali ilianza zoezi la bomoa-bomoa katika maeneo hayo ambayo watu wanaishi Mita 60 ndani ya mto msimbazi.

Na bomoa-bomoa hiyo ilianzia kwenye eneo la Mkwajuni na baada ya siku kadhaa Waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi William Lukuvi akawa amesitisha zoezi hilo mpaka Janauri 5 ambayo ni leo.

Lakini kabla ya kufika kwa siku ya Januari 5, wakazi wa Kinondoni wakiongozwa na Mbunge wa Jimbo hilo walikwenda kufungua kesi kwenye mahakama ya ardhi wakipinga kufanyika kwa hilo zoezi la bomoa-bomoa. Na kesi yao jana kwa mara ya kwanza imekuja kusikilizwa hapa kwenye mahakama kuu ya ardhi ambapo Jaji wa Mahakama hiyo Kuu ya Ardhi, Mh. Panterine Kente alisikiliza pande zote kwa maana ya waleta maombi pamoja na upande wa watetezi kwa upande wa serikali na mjadala ulikwenda kwa muda kidogo ikawa wamezungumza kila mtu akitoa hoja zake kutetea upande aliopo.

Lakini baada ya majadiliano ya muda mrefu ya kisheria Jaji Pente akawa ameamua kwamba leo majira ya saa tano angeweza kutoa maamuzi kwamba nini kitafuata kama ni kusitisha hiyo bomoa bomoa au kuendelea na taratibu zipi.

Sasa kilichotokea leo katika eneo la mahakama ambayo ipo katikati ya Jiji hapa kwenye mtaa wa Samora, nimefika majira ya asubuhi kshuhudia kesi hiyo ifanyiwe hukumu kwa maana ya kutolewa uamuzi majira ya saa tano lakini hilo halikuweza kufanyika.

Taarifa imetolewa mahakamani kwamba hukumu ya kesi hiyo itatolewa majira ya saa nane mchana. Wakazi zaidi ya mia sita wa kinondoni wako nje pembezoni mwa barabara ya Samora wakisubiri maamuzi ya kesi yao. Jeshi la Polisi linaonekana kuimarisha ulinzi katika eneo hili kuna magari ya doria ya polisi ambapo tayari wameshatoa tangazo kwa wananchi hao kwamba waondoke katika eneo hili.

Kwahiyo maamuzi ya bomoa inaendelea au inasitishwa ni saa nane leo mchana.
haya nchi ya watu hii ss wengine wasindikizaji tuu
 
Duuuuh hii bomoa hata siielewi... leo wapo tabata nasikia.
 
Bomoabomoa kwa Dar es salaam mwisho wake ni leo,kwasababu nyumba za maskini(Wananchi wa kawaida) zitakuwa zmekaribia kuisha zote hivyo kubaki za Vigogo ambazo haziwezi kuguswa..labda tusubiri tena sehem ambazo CCM ilipata resistance kipindi Cha Uchaguzi.
 
SHERIA INASEMAJE?
--->tanesco ni mfanyabiashara anahitaji fedha yako na huduma atakuletea
---->>dawasco ni mfanyabiashara utakapo huduma utaletewa!
---->>watu wa ardhi endapo walikuwa wanachukua kodi / ni kimakosa.
----->>vibendera vya chama chochote aviwezi kuwa msaada!
SHERIA IZINGATIWE!!!!!!!!
 
SHERIA INASEMAJE?
--->tanesco ni mfanyabiashara anahitaji fedha yako na huduma atakuletea
---->>dawasco ni mfanyabiashara utakapo huduma utaletewa!
---->>watu wa ardhi endapo walikuwa wanachukua kodi / ni kimakosa.
----->>vibendera vya chama chochote aviwezi kuwa msaada!
SHERIA IZINGATIWE!!!!!!!!
 
Wakome na ssm yao wale wamama wajingawajinga wanyoookeee ...!
 
Shukrani, ikifika hiyo saa 8 tafadhali tupe ripoti, kwa ufupi!
nashangaa upande wa pili zanzibar Bahressa anajenga apartment baharini na ameruhusiwa kusogeza maji ya baharini ili kuongeza eneo lake la ujenzi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom