Safi sana Mkuu, siku hizi umekuja na mtindo wa kujiamini 'tusiwape credit' wawe CCM, TISS, Polisi nk. Miaka ya 70, 80 mabalozi wa nyumba kumi walikuwa wakiheshimika sana, ilikuwa huwezi kununua gari kama hujapata baraka zao. Lakini taratibu walikuja kudharaulika, lakini pamoja na kudharaulika kwao kuna watu bado wanawapa credit. Hii ni kwa level ya vijijini na mitaani.
Kwa level ya watu wanaoonekana wameelimika hata humu JF bado wana mentality hiyo ya kuhusudu(kutoa credit) kwa vitu au watu, utasiki aa yule TISS bwana, lolote linaweza kutokea, NEC ni kila kitu nk. Binafsi nakiona kitendo hiki kama weakness fulani, kwa vile kadri unavyoonyesha kumuhusudu ndivyo opponent wako anavyozidi kukudharau. Mfano mzuri ukikutana uso kwa uso na simba lazima simba atastuka kwanza halafu atakuangalia kama utakimbia au miguu inatetemeka. Please guys be strong kama tunahitaji CCM ni wepesi sana, tumeona uchaguzi uliopita ni determination ya timu ndiyo iliyoshinda, lakini kama CDM wangesema tupige kura tusipige lazima CCM washinde na kweli CDM isingeshinda.