Huku Mkoani tuna balance hivi

Huku Mkoani tuna balance hivi

Norshad

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2013
Posts
5,216
Reaction score
12,604
unga nusu -500
bamia na majani ya maboga -300
Nyanya,hoho bilinganya -600
uduvi- 500
mafuta -200

Huku kuna Mgomo wa Chipsi yai...
317617705cef884ea08a48b69b70be6e.jpg
 
Umeharibu hapo Kwenye ugali naona ni sembe.. Dona ingekua ni bora zaidi
 
Screenshot_2016-11-12-11-00-59-1-1.png

Hii kitu hatari najua mnapenda ila ndio mtafanyaje sasa tuacheni na misosi yetu.
 
mzigo dona ule sema halina ile rangi tu.
 
Toa hivyo vingine niachie hiyo rost ya bilinganya na ugali tu dah....
 
Lile bakuli si mlenda ule?hako kangumi katateleza fasta.
 
Mnapikia kuni eehh? Maji ya kunywa hamna? Unakula milo mingapi? Hapo kwa siku lazima ilale 10,000 ambapo ni sawa na 300,000 kwa mwezi. Usafiri, kuvaa, sabuni, umeme, ada za watoto, pango, vocha za simu, michango ya harusi na msiba, sadaka, kunyoa nywele, soda japo moja kwa wiki, azamtv, sukari, tunda japo mara moja kwa wiki, upo hapo?
 
sijasema kwamba tunayafurahia haya maisha, lakini ni rahisi tofauti na kwenda kula vibandani hapo 10 lazma ikate, huku 10 tunatumia siku mbili...jiko la gesi na maji ya Bomba, maji huku ni 2500 kwa mwezi, kwa yule aliyeuliza, na Usafiri cjui kwa wengine mm natumia miguu maana kazini na ninapoishi ni kama km1 hivyo hiyo ni nauli ya Muwa tunatembea tu...Mimi Mzaliwa wa Dar ila pamenishinda, kwanza Joto, pili Foleni. tatu vyakula ninavyovipenda Dar kuvipata ni mtihani naukivipata ghalama iko juu, nne dar mna mazoea sana, kujuana kwingi, huku kila mtu na zake...na la mwisho nahisi huku kunafaa kutafuta zaidi,
 
Back
Top Bottom