Komeo Lachuma
JF-Expert Member
- Oct 31, 2014
- 5,375
- 11,524
Wewe kafanye tofauti Fatwah ikukamate, tunakuomba Mufti wetu uharakishe hii kitu na hapa kwetu.anacholenga kuzuia ni simu isisomwe au uovu usionekane? Kama simu ina mazuri tu, anazuia ya kazi gani? Badala awaambie wanaume wasifanye mabaya anawaambia wanawake wasisome simu? Mbona fatwa imekaa kushoto kushoto?
hata mkawekeana kukatana vichwa, wekeni tuSheikh mkuu wa Dubai ametangaza kuwa ni Haram kwa mwanamke Kupekua pekua kwenye Simu ya Mumewe bila Idhaa yake. Hii Fatwa ameitangaza na tayari imeshakuwa sharia.
Mwanamke hutakiwi kuangalia simu ya mumeo bila idhaa yake. Labda tu kama unaangalia ikiwa imezimwa unaangalia kava lake likoje au yenyewe inapendezaje mkononi.IKIWA IMEZIMWA LAKINI.
Tunaomba na sheikh wetu huku uangalie jambo hili jema kabisa katika kudumisha mahusiano.akina mama watuachie simu zetu.siyo tunalazimika kwenda kuoga na simu hata kwenye swimming pool.maana ukiacha inchi kavu inakuwa issue. Kwa sasa simu za wanaume wengi inasemakana zimekuwa na password zaidi ya 5 mpaka kuja kufikia kwenye sms,calls,photos,whatsapp app n.k
Jambo hili limesababisha wakati mwingine tuwe tunasahau hata hizo password na kulazimika kuwa consult wataalam wa IT watusaidie.
Tupate Taarifa Kamili.
View attachment 992289
Eti simu ya mumeo usiguse kabisa na uiogope kama ukoma duuhSijawahi kupata jibu sahihi hasa kwanini mke wangu ninae-share nae kitanda kimoja na kunipikia chakula asishike simu yangu,ni sababu gani itakayonisukuma kufanya hivi!
Simu zangu zote mama anazijua password zake,hata mimi naijua password ya simu yake kwanini muishi mkijengeana mashaka?
Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
Kama unapendwa unapendwa tu not otherwise...Eti nisisome?? No thank you
Mkuu Simu ni Kama Ubongo kila mtu ana wake!Sijawahi kupata jibu sahihi hasa kwanini mke wangu ninae-share nae kitanda kimoja na kunipikia chakula asishike simu yangu,ni sababu gani itakayonisukuma kufanya hivi!
Simu zangu zote mama anazijua password zake,hata mimi naijua password ya simu yake kwanini muishi mkijengeana mashaka?
Sent from my Redmi Note 5 using Tapatalk
πππππImeshapita, tumelobia vizuri
Hivi mkuu ulishawahi kujiuliza kama mpo ndani usiku wa manane ghafla ukapata tatizo kubwa la kiafya ambalo inabidi watafutwe watu kuja kukupa msaada halafu simu ya mkeo haina credit ila simu yako ina salio la kutosha na huwezi kufanya lolote so itambidi mkeo akahangaike kugonga milango ya majirani kuomba msaada wakati simu yako ina salio tatizo ni hajui password zake?Mkuu Simu ni Kama Ubongo kila mtu ana wake!
Ni kutokujitambua tu,mkishakuwa ndani ya ndoa kila kitu ni chenu wote siyo kuanza kubaguana na wengi hawajui mkishaanza kuzuiyana baadhi ya vitu ndo mwanzo wa nyumba kuwa na vurugu zisizokuwa na mashiko.