Huduma ya cheka ni dar es salaam tu

Gokona

Member
Feb 16, 2010
62
9
Wadau kwanza naomba samahani kwa hawa jamaa wenye mtandao ambao wameweka huduma ya cheka maana baada ya faraja inakuwa kero na karaha,mimi ni mtu wa safari safari za mikoani sana sasa nikiwa huku unaweza ukakesha usiku kucha hupati huduma ya cheka ya 500 unaambiwa jaribu ya 2000 au cheka ya 5000 lakini nikiwa dar es salaam kila siku na wakati mwingine hata saa moja asubuhi,saa mbili na hata saa tatu ukigusa tu cheka ya 500 hiyo sasa biashara mnafanyia dar lakini mnatutia mchanga wa macho sisi wa mikoani maana server zimekuwa saved out of dar cheche sasa mkitoa matangazo mseme kwamba hii ni kwa Dar tu tusisumbuane watu hatulali acheni usanii,imeniuma sana na sio kama nashindwa kununua airtime kwani kabla ya huduma hii nilikuwa sipigi simu? ila kama kuna cost cutting sio mbaya .jirekebisheni sisi wote ni watanzania watoto wa baba mmoja.
 
mana ake nini hiyo mkuu maana umeniacha na sijaelewa au niko nyuma na mambo ya Bongo jamani?hiyo cheka ndo huduma gani na hutolewa na kampuni gani kwa ajili gani?au kwa watu wanaopenda kucheka?
 
:D:eek:hahaha Mkubwa naona upo kwenye financial crisis..ila nikweli nimesikia complains hizo especially kwenye minara very remote area...Naona nguzo inazidiwa uwezo kama cheka ya 500 ikiwa available all ze time..huenda inakuwepo kwa muda mfupi then wanaclose band yake,Kwa sasa wamebadilisha utaratibu unajiunga kuanzia saa alfajiri mpaka kesho yake saa9.59 alfajiri kwa mkubwa re set alarm time yako na sio saa sita tena kama ulivyosea....Gud nite
 
mana ake nini hiyo mkuu maana umeniacha na sijaelewa au niko nyuma na mambo ya Bongo jamani?hiyo cheka ndo huduma gani na hutolewa na kampuni gani kwa ajili gani?au kwa watu wanaopenda kucheka?

Kampuni karibu zote za simu zimeanzisha huduma za kupiga simu kwa gharama nafuu sana kwa kipindi flani cha muda.Vodacom wao wanahuduma ya CHEKA TIME..unajiunga kwa Tsh 500 unapata muda wa maongezi dak 60 ambazo unazitumia kwa kipindi flani cha siku, vivyo hivyo kwa Tsh 2000 unapata dak 100 za maongezi kwa siku mbili na Tsh 5000 unapata dak 300 za maongezi kwa siku 5.Sasa huduma hii ya Tsh 500 kwa dar nadhan kutokana na mitambo ya Voda kuwa bomba na yenye uwezo huduma hupatikana hata saa4 asubuh kulingana na eneo uliopo..ila kwa upcountry huduma ya Tsh 500 ni ngumu sana kupatikana..only ths2000 na 5000 ndo unawezakujiunga at anytime of ze day.natumai umenipata mdau magulamangu
 
Hata mimi niko Arusha sasa najaribu sana kujiunga na hiyo cheka naambiwa jiunge na cheka ya 2000 lakini nikiwa dar ni bwerere tu. inaudhi
 
Back
Top Bottom