Wadau kwanza naomba samahani kwa hawa jamaa wenye mtandao ambao wameweka huduma ya cheka maana baada ya faraja inakuwa kero na karaha,mimi ni mtu wa safari safari za mikoani sana sasa nikiwa huku unaweza ukakesha usiku kucha hupati huduma ya cheka ya 500 unaambiwa jaribu ya 2000 au cheka ya 5000 lakini nikiwa dar es salaam kila siku na wakati mwingine hata saa moja asubuhi,saa mbili na hata saa tatu ukigusa tu cheka ya 500 hiyo sasa biashara mnafanyia dar lakini mnatutia mchanga wa macho sisi wa mikoani maana server zimekuwa saved out of dar cheche sasa mkitoa matangazo mseme kwamba hii ni kwa Dar tu tusisumbuane watu hatulali acheni usanii,imeniuma sana na sio kama nashindwa kununua airtime kwani kabla ya huduma hii nilikuwa sipigi simu? ila kama kuna cost cutting sio mbaya .jirekebisheni sisi wote ni watanzania watoto wa baba mmoja.