Huduma mbovu kituo cha afya Sinza Palestina

Umkondo wa Swize

JF-Expert Member
Dec 29, 2012
282
89
attachment.php


Jana mwanangu alizidiwa usiku alikuwa anatapika nikamwahisha kituo cha afya cha serikali Sinza Palestina, kufika pale nikapata huduma kama kawaida kwa daktari akaniambia nimpeleke mwanangu maabara akachukuliwe vipimo ili wajue tatizo ni nini.

Kufika maabara nikakuta watu wengi wanamsubiri mtaalamu wa maabara ilikuwa mishare ya saa 4.30 usiku basi tulisota kwenye benchi pale mpaka saa 5;45 usiku jamaa hajatokea huyu wa maabara.

attachment.php

Hili Tray kama linavyo onekana ndipo unapaswa kuweka form au daftari kwa ajili ya kuchukuliwa vipimo tulikaa pale mpaka saa 6.00 huyo jamaa wa maabara alikuwa hajatokea na mimi mwanangu alikuwa anatapika bado kumuuliza mlinzi akasema alikuwepo atakuwa katoka kidogo, fikiria toka saa 4.30 mpaka saa 6.00 usiku mtu wa kuchukua vipimo hayupo na haijulikani alienda kufanya zinaa au kulewa na kuacha kazi pasipo taarifa yoyote kwa wenzie, kuona hivyo mi nikaamua kuondoka na kumpeleka mwanangu kituo binafsi pale Manzese darajani St. monica na tukapatiwa matibabu. Serikali inabidi ianzishe patrol kwenye vituo vya afya kusudi kuwabana wale wafanyakazi wenye mtindo wa kusign na kuondoka kwenda kuendelea na shughuli zao binafsi. Usipo kuwa makini unaweza poteza mwanao/mgonjwa wako hivi hivi.

Sijui hao wenzangu nilio waacha walipata muda gani huduma. Wizara ya Afya liangalieni hilo.
 
Mkuu pole sana kwa kuua mbu toka saa 4.30 mpaka saa 6.00 usiku si mchezo.
 
Uongozi wa hospitali husika wanapaswa kulifuatilia kwa makini.
 
Back
Top Bottom