Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 71,270
- 105,441
Hujathibitisha nina chuki binafsi.
Sio wewe uliyesema JPM alikuuzia nyumba? Sasa leo unasema unafuata principle kwa nini huendi kumshauri rafiki yako kama ni kweli? Nafahamu hapo unajibinafsi tu huna lolote. Wivu tu unakusumbua.
Hujathibitisha serikali iliuza korosho nje.
Hujakanusha kwamba serikali imetuingiza katika hasara kubwa kwa kuingilia biashara ya korosho.
Hujakanusha kwamba mauzo ya mazao ya kilimo yameanguka kwa zaidi ya nusu ya mapato kwa mwaka mmoja uliopita, kwa asilimia 55.
Hujatuonesha mkakati wa serikali kujihimu kukabiliana na muanguko huu.
Benki Kuu ya Tanzania yenyewe imetuambia habari hizi.
Unamtetea JPM kwa mahaba tu, wakati data zinaonesha anaangusha exports za kilimo.