Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 762
- 6,980
Chama Cha mapinduzi ni chama kikubwa barani Afrika, kilianzishwa kikiwa na misingi yake na kililelewa katika misingi ambayo baadhi ililenga kukiweka kuwa Chama Cha kizalendo.
Kufikia Sasa chama Cha mapinduzi kinazidi kukosa dira kwa sababu kimeshindwa kutofautisha Mambo ya kitaifa na maslahi ya chama, kimeshindwa kutofautisha asset and liability, kimeshindwa kuwatofautisha wasaka madaraka na viongozi wa wananchi, kimeshindwa kutofautisha uimara wa chama na uimara wa serikali, kimashindwa kujinasua kwenye serikali na kusimama Kama chama Cha siasa kinachoweza kupambana na kushinda uchaguzi.
Chama cha mapinduzi kwa uimara wa Mwenyekiti wa Sasa hakipaswi kumpokea Mhe. Sumaye wala Lowasa kwa sababu Hawa watu walishaiambia dunia wazi kwamba CCM siyo baba yao wala Mama yao. Walitamka adharani kwamba hawatarejea ccm kwa sababu ya MAPUNGUFU yaliyopo huko. Leo wamepokelewa na Kama ccm wanaweza kupima upepo watagundua hakuna mwananchi aliyeonyesha kuunga mkono kurejea kwao ccm kwa sababu siyo watu wetu kujua wanaamini Nini.
Leo Ccm inazoa viongoz kutoka upinzani lakini naamini Kati yao hakuna anayekwenda ccm kwa sababu anapenda tanzania, wanakwenda kwa sababu wanataka kula na kulishwa. Kesho njaa ikiwakaba wakapata wakuwalisha wataondoka tu.
Lakini kibaya zaidi ni kwamba CCM kwa hii miaka mitano wamewavunja moyo Wana ccm nakuwapa thamani wapinzani, vijana kwa wazee wamepokelewa ccm na kupewa madaraka huku vijana waliokuwa watiifu kwa ccm wakiwa hawana ajira. Imagine mtu anatokoa upinzani na uwezo wake mdogo anafika anapewa uwaziri, hao aliowakuta watafurahi?
CHADEMA wanayo historia nzuri ya kukabidhi watu wasio na uchungu na chama madaraka , waliwakaribisha 2015 Leo wapo wapi, walikuwa wanatafuta kula.
Kuelekea 2020 napenda kuwakumbusha ccm kuwa uongozi wa Dr.Bashiru umeongeza wasiojulikana kiitikadi kwenye chama jambo ambalo litakipa chama wakati mgumu sana kuchagua Nani awe Nani, mmewanunua watu ambao kwa fedha walizopata waliuza utu wao na pale fedha na madaraka yatakaopoisha pia tambueni watauza uzaliwa wao wa baba wa kambo.
Jiulizeni Sumaye anakosa au anataka Nini kwa umri wake? Kwa alichokionyesha unadhani rasilimali za nchi waliziuza kwa makosa? Hawa watu wanataka madaraka bila kujali wananchi wataathirika vipi.
2015 waliuza gesi kwa kupitia sheria za bunge, leo Mwenyekiti wetu Mzee Magufuli asiposoma halama za nyakati wanaweza wakakiuza chama mara tu atakapoondoka.
Tunakwama kwa sababu tumeshindwa kuachana na waliotukwamisha.
Kufikia Sasa chama Cha mapinduzi kinazidi kukosa dira kwa sababu kimeshindwa kutofautisha Mambo ya kitaifa na maslahi ya chama, kimeshindwa kutofautisha asset and liability, kimeshindwa kuwatofautisha wasaka madaraka na viongozi wa wananchi, kimeshindwa kutofautisha uimara wa chama na uimara wa serikali, kimashindwa kujinasua kwenye serikali na kusimama Kama chama Cha siasa kinachoweza kupambana na kushinda uchaguzi.
Chama cha mapinduzi kwa uimara wa Mwenyekiti wa Sasa hakipaswi kumpokea Mhe. Sumaye wala Lowasa kwa sababu Hawa watu walishaiambia dunia wazi kwamba CCM siyo baba yao wala Mama yao. Walitamka adharani kwamba hawatarejea ccm kwa sababu ya MAPUNGUFU yaliyopo huko. Leo wamepokelewa na Kama ccm wanaweza kupima upepo watagundua hakuna mwananchi aliyeonyesha kuunga mkono kurejea kwao ccm kwa sababu siyo watu wetu kujua wanaamini Nini.
Leo Ccm inazoa viongoz kutoka upinzani lakini naamini Kati yao hakuna anayekwenda ccm kwa sababu anapenda tanzania, wanakwenda kwa sababu wanataka kula na kulishwa. Kesho njaa ikiwakaba wakapata wakuwalisha wataondoka tu.
Lakini kibaya zaidi ni kwamba CCM kwa hii miaka mitano wamewavunja moyo Wana ccm nakuwapa thamani wapinzani, vijana kwa wazee wamepokelewa ccm na kupewa madaraka huku vijana waliokuwa watiifu kwa ccm wakiwa hawana ajira. Imagine mtu anatokoa upinzani na uwezo wake mdogo anafika anapewa uwaziri, hao aliowakuta watafurahi?
CHADEMA wanayo historia nzuri ya kukabidhi watu wasio na uchungu na chama madaraka , waliwakaribisha 2015 Leo wapo wapi, walikuwa wanatafuta kula.
Kuelekea 2020 napenda kuwakumbusha ccm kuwa uongozi wa Dr.Bashiru umeongeza wasiojulikana kiitikadi kwenye chama jambo ambalo litakipa chama wakati mgumu sana kuchagua Nani awe Nani, mmewanunua watu ambao kwa fedha walizopata waliuza utu wao na pale fedha na madaraka yatakaopoisha pia tambueni watauza uzaliwa wao wa baba wa kambo.
Jiulizeni Sumaye anakosa au anataka Nini kwa umri wake? Kwa alichokionyesha unadhani rasilimali za nchi waliziuza kwa makosa? Hawa watu wanataka madaraka bila kujali wananchi wataathirika vipi.
2015 waliuza gesi kwa kupitia sheria za bunge, leo Mwenyekiti wetu Mzee Magufuli asiposoma halama za nyakati wanaweza wakakiuza chama mara tu atakapoondoka.
Tunakwama kwa sababu tumeshindwa kuachana na waliotukwamisha.