House Girls

House Girls

Me370

JF-Expert Member
Joined
Mar 10, 2008
Posts
985
Reaction score
293
Naombeni msaada w mawazo kidogo, Eti nini madhara ya kukaa na house girl mwenye mimba?

Au ni busara kufanya kama wanavyofanya wengi kwa kumpa nauli aende kwao?

Mfano wewe ukigundua House girl wenu ni mama kijacho miezi mitatu utachukua uamuzi gani haswa ukizingatia kaipatia mitaani huko?
 
Aisee muachie aende nyumbani maana akijifungua jukumu la kwanza linakuwa mtt wake.
 
Ujauzito unatofoutiana kati ya mtu mmoja na mwingine, mimi niliwahi kuletewa housegirl mjamzito alikuja kwangu mimba ikiwa na miezi miwili tu, na ilikuwa vigumu kumgundua coz alikuwa na umbile dogo halafu ushungi muda wote. alikuwa anafanya kazi zake kama kawaida hakuwa akiumwaumwa kama wamama wengine, so mimba ilvyofika miezi nane akasema anaenda kujifungulia kwao, nikamfungaishia akaenda kujifungua. mwingine nimekaa nae mwaka mzima akaiibua mimba huko mtaani, mimba yake ikawa ya kulala tu, nilimrudisha kwao mapema na mimba yake
 
waite baba kijacho na mama kijacho waamue wanafaya nini
 
sie wanaume huwa tunawasikiliza wake zetu tu katika maswala yanayohusu house girls, chamsingi km una mke ongea na mkeo umsikilize anasemaje kuhusu hilo, then fuata ushauri wake, naamini wao wanajua zaidi haya mambo kuliko sisi wanaume!
 
Naombeni msaada w mawazo kidogo, Eti nini madhara ya kukaa na house girl mwenye mimba? Au ni busara kufanya kama wanavyofanya wengi kwa kumpa nauli aende kwao? Mfano wewe ukigundua Hsg wenu ni mama kijacho miez mi 3 utachukua uamuzi gani haswa ukizingatia kaipatia mitaani huko?
Unatakiwa umlee mpaka ajifungue kwa sababu hakutoka kwao na mimba na kaipatia akiwa kwako na umeshindwa kumcontrol hadi kapata mimba.
 
Mbali ya title yake ya housegirl ,ni binadamu kama mwingine yeyote hivyo anahitaji kuangaliwa kwa jicho la binadamu na si jicho la housegirl
 
Unatakiwa umlee mpaka ajifungue kwa sababu hakutoka kwao na mimba na kaipatia akiwa kwako na umeshindwa kumcontrol hadi kapata mimba.

mhhhhh hapo kwenye kuncontrol unamuonea bhana
 
Unatakiwa umlee mpaka ajifungue kwa sababu hakutoka kwao na mimba na kaipatia akiwa kwako na umeshindwa kumcontrol hadi kapata mimba.

Mmmmmm! Sasa Angemcontrol Vp Asipate Mimba Kama Ni Mtu Mzima Mwenye Uwezo Wa Kupata Ujauzito?
 
Naombeni msaada w mawazo kidogo, Eti nini madhara ya kukaa na house girl mwenye mimba? Au ni busara kufanya kama wanavyofanya wengi kwa kumpa nauli aende kwao? Mfano wewe ukigundua Hsg wenu ni mama kijacho miez mi 3 utachukua uamuzi gani haswa ukizingatia kaipatia mitaani huko?

nani kakuambia kumpa nauli aende kwao ndo busara?????
take postion angekuwa wanao/dada ako/nduguyo unarudishiwa mtoto na unaambiwa ana mimba je huyo baba kijacho yupo wapi?humjui??angefanya nini??
ni madara kukaa kimya ila chunguza ujue nani kampa huyo ni dada yenu wa kazi kakusaidia kukaa na wanao

kaa na binti muulize nani kampa hiyo mimba may be ndugu zako or majirani wa mtaa na utakuwa unafahamu tabia zao
zen ndo utachuukua jukumu la kuwaambia wazazi wake mrudishe au aolewe na mweye mtoto
 
Unatakiwa umlee mpaka ajifungue kwa sababu hakutoka kwao na mimba na kaipatia akiwa kwako na umeshindwa kumcontrol hadi kapata mimba.

Kum control mwanadamu ni ngumu sana, labda Mungu mwenyewe!
 
Mimi wangu aliwahi kupata mimba, sikumrudisha kwao maana alikuwa anaendelea na majukumu yake vizuri huku akiwa mjamzito. Nilipanga kumrudisha miezi kama mi3 baada ya kujifungua maana niliuelewa ugumu wa maisha wa vijijini. Alijifungua, nikamuhudumia wakati nimeleta dada mwingine.

Baada ya wiki 2 tu, akaanza kupiga kazi kama kawaida, smtms kumzidi asiye na mtoto. Nikaamua kumuacha aendelee na kazi sikuona usumbufu mkubwa sana kwa yule mtoto wake. Baada ya miaka kama miwili hivi mtoto alichukuliwa na kaka yake. Ila yeye bado nipo naye. Trust me, kitendo cha kumuhudumia, hajawahi hata kuwaza kuondoka kwangu. shida ya maHG nazisikia kwa mashosti wangu, kwa muda mrefu sizijui.

watu wengi sana walinishauri nimuondoe, lkn nilikataa kutokana na jinsi alivyo mchapa kazi. kwani pamoja na mimba yake, kuwa na mtt, kila kitu kilikuwa kinaenda sawa nyumbani kwangu. Pia nilimuonea huruma kurudi kijijini. wale walionishauri nimuondoe, sasa wananionea donge wanasema nina bahati sana ya kupata msichana aliyedumu zaidi ya miaka mitano nyumbani kwangu. wameshasahau walivyokuwa wananishauri nimfukuze. Jamaa mwenyewe aliyempa mimba ni playboy tu wa mtaani kazi yake kuchukua maHG wa watu.
usiache watu wakuamulie maamuzi ya home kwako, kama unaona ana-worth kuendelea kukaa naye, usimuondoe
 
Unatakiwa umlee mpaka ajifungue kwa sababu hakutoka kwao na mimba na kaipatia akiwa kwako na umeshindwa kumcontrol hadi kapata mimba.

Utamzuije mtu mzima asipigwe dushelele?
 
Naombeni msaada w mawazo kidogo, Eti nini madhara ya kukaa na house girl mwenye mimba?

Au ni busara kufanya kama wanavyofanya wengi kwa kumpa nauli aende kwao?

Mfano wewe ukigundua House girl wenu ni mama kijacho miezi mitatu utachukua uamuzi gani haswa ukizingatia kaipatia mitaani huko?

Heeee we mkeo akipata mimba wkt yupo kazini anafukuzwa???? Acheni ujangili mwacheni afanye kazi kama anaimudu ili akusanye ngawira zake na pia ungesimamia jukumu la kama mzazi ambaye mwanaye angepata ujauzito ktk mazngra hayo ungefanyaje? muite huyoo mkwe kijacho umsomee hukumu yake na si kumtelekezeni mtoto wa mwenzio kwani KILE UMTENDEACHO MWANA WA MWENZIO NDICHO NACHO MWANA WA KWAKO ATATENDEWA.
 
1. Thibitisha ujauzito kwa vipimo
2. Wakutanishe baba na mama kijacho mujadili wa marefu na mapana wakubaliene what next.
3. Wape taarifa wazazi au ndugu ambao walikukabidhi Huyo binti.
4.ONYO: Usikubali aondoke hapo kwako bila kuwapa wazazi/ndugu taarifa utapata kesi and if possible msindikize hadi mikononi mwa wazazi/ ndugu au kama atapata kibali cha wazazi kuhamia kwa mchumba wake it's OK.
 
Mmmmmm! Sasa Angemcontrol Vp Asipate Mimba Kama Ni Mtu Mzima Mwenye Uwezo Wa Kupata Ujauzito?
Mama mwenye nyumba unamwachia housgirl amtunze mme wake unategemea nini? Siku hizi hata kumtandikia kitanda baba mwenye nyumba anaachiwa housegirl.
 
Back
Top Bottom