Kati ya mambo aliyoyaongelea ni kuhusu suala hili la kutoza kodi kwa kutumia mashine hizi. Alisema anawaomba wafanyabiashara watoe ushirikiano kwa kutumia mashine. Sasa ninajaribu kujiuliza ushiriano huu utawezekana vipi ikiwa hao TRA wenyewe tangu mwanzo hawajatoa ushirikiano kwa wafanyabiashara? Wao wameleta mashine, wamewateua wasambazaji, wamepanga bei za hizo mashine wanawalazimisha wafanyabiashara wazinunue na hakuna ushahidi wowote kuwa katika michakato hii wafanyabiashara walishirikishwa sasa leo wanakuja from no where wanawaomba ushirkiano.
Wanasema kuwa gharama za mashine zitarejeshwa kwenye marejesho ya VAT lakini wanachoshindwa kutuambia ni utafiti upi waliufanya wakaona kuwa kila mfanyabiashara anayelipa VAT anauwezo wa wakati mmoja kutoa fedha cash za kuinunua mashine na kuikopesha TRA na serikali ili baadaye wa mlipe kwa kukata kwenye marejesho ya VAT. Je serikali na TRA watamlipa Interest kiasi gani mfanyabiashara kwa huu mkopo wanao mkopa? Huu ununuzi wa hizi mashine ni ufisadi mwingine kama ilivyo Dawans, Richimond n.k. Mabilioni ya fedha za kodi zitakazokatwa kwenye marejesho ya VAT ni hela za walipa kodi wa TZ ambazo wanataka kuziiba kwa staili hii mpya kabisa. Hivyi haya makampuni ni yakina nani hasa? TRA waliyapata kwa kupitia utaratibu gani? Tutaendelea kuibiwa na kuonewa na viongozi kwa kutumia serikali yetu mpaka lini?
Anasema huu ni utaratibu utakao waondolea wafanyabiashara usumbufu. Yeye na serikali ya ccm kumlazimisha mfanyabiashara kutoa sh 1,100,000 mapaka millioni 3,000, 000 kwa wakati mmoja tena cash sio tatizo wala usumbufu, kweli aliyeshiba hamjui mwenye njaa. Inasemekana mashine hizi zinaweza kupatikana sehemu nyingine chini ya bei hizi ambazo sasa hivi huyu mfanyabiashara analazimishwa kunununua, kwa nini katika kipindi hiki cha soko huria wafanyabiashara wasipewe specifications za mashine wakanunua wenyewe kokote wanako weza kuzipata kwa bei nafuu? Huu kweli si ufisadi na utapeli mwingine tunao ushuhudia hapa Tanzania.
Mashine hizi baada ya kukatwa gharama zake kwenye marejesho ya VAT kimsingi zitakuwa mali ya Serikali kwa kupitia TRA, hii haingii akili kwanini serikali kwa kupitia TRA wasinunue machine hizi wao na kuja kuziweka kwa wafanyabishara ili wazitumie badala yake wanawalazimisha wafanyabiashara wa wakopeshe mabilioni haya ya fedha? Hapa kuna harufu ya ufisadi ambao hatujaustukia.
Kama serikali na TRA wanaamini kwa dhati kabisa kuwa mashine hizi zitaongeza ukusanyaji wa kodi katika mazingira haya ya TZ ya ukatikanaji wa umeme na si mradi mwingine wa kifisadi kwa nini wasinge enda wao kukopa bank, kutafuta grands au hata kuwaomba wafadhili wa wasaidie katika kufanikisha mradi wa kuweka mashine hizi?
Kimsingi nakubalina na serikali katika juhudi zake za kuongeza ukusanyaji wa kodi ambazo zitatumika vizuri kusaidia kuboresha kumhudumia mwananchi wala sio kama sasa ambapo zinatumika katika maisha ya kifahari ya viongozi wetu huku wakijua kuwa hii ni nchi maskini ( mfano tumejionea wenyewe kwenye Tsunami ya japani aina ya magari waliyo nayo ukilinganisha na haya yanayotumiwa na viongozi wetu tena mbaya zaidi wengine kutokea nyumbani Masaki kwenda ofisini mt wa Samora). Ila sikubaliani na watu wanaotumia mwanya huo kuwaibia wananchi ili wajinufaishe hii si haki na wananchi tupinge uonevu huu wa wazi kabisa.
Wanasema kuwa gharama za mashine zitarejeshwa kwenye marejesho ya VAT lakini wanachoshindwa kutuambia ni utafiti upi waliufanya wakaona kuwa kila mfanyabiashara anayelipa VAT anauwezo wa wakati mmoja kutoa fedha cash za kuinunua mashine na kuikopesha TRA na serikali ili baadaye wa mlipe kwa kukata kwenye marejesho ya VAT. Je serikali na TRA watamlipa Interest kiasi gani mfanyabiashara kwa huu mkopo wanao mkopa? Huu ununuzi wa hizi mashine ni ufisadi mwingine kama ilivyo Dawans, Richimond n.k. Mabilioni ya fedha za kodi zitakazokatwa kwenye marejesho ya VAT ni hela za walipa kodi wa TZ ambazo wanataka kuziiba kwa staili hii mpya kabisa. Hivyi haya makampuni ni yakina nani hasa? TRA waliyapata kwa kupitia utaratibu gani? Tutaendelea kuibiwa na kuonewa na viongozi kwa kutumia serikali yetu mpaka lini?
Anasema huu ni utaratibu utakao waondolea wafanyabiashara usumbufu. Yeye na serikali ya ccm kumlazimisha mfanyabiashara kutoa sh 1,100,000 mapaka millioni 3,000, 000 kwa wakati mmoja tena cash sio tatizo wala usumbufu, kweli aliyeshiba hamjui mwenye njaa. Inasemekana mashine hizi zinaweza kupatikana sehemu nyingine chini ya bei hizi ambazo sasa hivi huyu mfanyabiashara analazimishwa kunununua, kwa nini katika kipindi hiki cha soko huria wafanyabiashara wasipewe specifications za mashine wakanunua wenyewe kokote wanako weza kuzipata kwa bei nafuu? Huu kweli si ufisadi na utapeli mwingine tunao ushuhudia hapa Tanzania.
Mashine hizi baada ya kukatwa gharama zake kwenye marejesho ya VAT kimsingi zitakuwa mali ya Serikali kwa kupitia TRA, hii haingii akili kwanini serikali kwa kupitia TRA wasinunue machine hizi wao na kuja kuziweka kwa wafanyabishara ili wazitumie badala yake wanawalazimisha wafanyabiashara wa wakopeshe mabilioni haya ya fedha? Hapa kuna harufu ya ufisadi ambao hatujaustukia.
Kama serikali na TRA wanaamini kwa dhati kabisa kuwa mashine hizi zitaongeza ukusanyaji wa kodi katika mazingira haya ya TZ ya ukatikanaji wa umeme na si mradi mwingine wa kifisadi kwa nini wasinge enda wao kukopa bank, kutafuta grands au hata kuwaomba wafadhili wa wasaidie katika kufanikisha mradi wa kuweka mashine hizi?
Kimsingi nakubalina na serikali katika juhudi zake za kuongeza ukusanyaji wa kodi ambazo zitatumika vizuri kusaidia kuboresha kumhudumia mwananchi wala sio kama sasa ambapo zinatumika katika maisha ya kifahari ya viongozi wetu huku wakijua kuwa hii ni nchi maskini ( mfano tumejionea wenyewe kwenye Tsunami ya japani aina ya magari waliyo nayo ukilinganisha na haya yanayotumiwa na viongozi wetu tena mbaya zaidi wengine kutokea nyumbani Masaki kwenda ofisini mt wa Samora). Ila sikubaliani na watu wanaotumia mwanya huo kuwaibia wananchi ili wajinufaishe hii si haki na wananchi tupinge uonevu huu wa wazi kabisa.