Makala Jr
JF-Expert Member
- Aug 25, 2011
- 3,395
- 1,110
Ikiwa ni baada ya miezi miwili kupita tangu mgomo wa madaktari uliopelekea kutekwa,kuteswa na kutupwa kwenye msitu wa Mabwepande.Hali bado siyo shwari katika hospitali nyingi nchini..! Leo nimetembelea hospitali ya mkoa Mbeya kumwona mdogo wangu anaesoma Ivumwe Sekondari aliyeugua ghafla | |Kwa mujibu wa Matron aliyefanikisha kumfikisha mdogo wangu hospitalini hapo amelalamikia kusuasua kwa huduma kwani tangu walipofika saa 10:07 asubuhi hawajahudumiwa hadi saa saba.Ukifika hospitalini-reception utakutana na kundi la watu wanaosubiri huduma,kwa upande mwingine utakutana na watu wasiopungua 100 wakisubiri kuwaona madaktari. Kwa mujibu wa Nesi mmoja amedokeza kuwa hali ya utoaji tiba siyo nzuri,dawa zimebaki kidogo sana kiasi kwamba uongozi umeamua kuhalalisha kuwaandikia dawa wagonjwa ili wakajinunulie. Miundombinu siyo nzuri kwani hakuna hata nyenzo za kubebea wagonjwa from A to B...Kimsingi huduma ni mbovu kiasi cha kutozungumzika.