Niende moja kwa moja kwenye mada,Leo maaskofu wametoa UJUMBE wao kama viongozi wa dini,Hatuna budi walengwa kwuyafanyia kaz, wametimiza wajibu wao Kwa mungu na Kwa wananchi, na baadhi ya viongozi wa dini hasa manabii tunaomba watoe UJUMBE wa serekali wasikae kimya au wao wanaona mambo yote yapo sawa?
Nimefarijika sana na ushauri wenu kwa wenye Mamlaka kuhususiana na Reforms mbalimbali juu ya uchanguzi,
nina wapongeza sana, Mungu Muumba azidi kuwalinda, kutetea na kuwabarikini, kwa kukubali kuwa miongoni mwa sauti za wanyonge wasio na majukwaa katika taifa hili,
Ujumbe wenu wazee wangu bila shaka umefika je utafanyiwa kazi na walengwa?
Je kama hautafanyiwa kazi mna plan ipi wazee wangu?
Mnakumbuka swala la Bandari yetu na DPW?
ushauri wenu ulifanyiwa kazi?
Aliudharau na siku ya ku saini mikataba akasaini siku na muda ambao mpo ibadani jumapili asubuhi,
Alizidi kuwa na kisirani hata sherehe ya ufunguzi wa jengo la Ikulu Dodoma siku ilipangwa mkiwa hampo nchini mpo Vaticani,
Na kwa kujiona yeye ni mbabe kuliko nyie alikimbilia kwa Papa Francis kujikosha.
Ombi kwenu ushauri wenu huu wa awamu hii asipoufanyia kazi, tunawaomba mtuongoze njia ya kuandamana kwa AMANI kutaka katiba Mpya, Tume Huru na Reforms mbalimbali za uchanguzi, je watawaangiza polisi wawashambulie viongozi wa dini ambao nanyi ni sehemu ya raia wa Taifa hili,
Nipo tayari kuwafuata mkoa wowote kuungana nanyi kufanya maandamano ya amani.
Asanteni Sana.