Ketoka
JF-Expert Member
- Sep 23, 2015
- 1,121
- 1,981
Kumekuwepo na dhana dhidi ya jamii ya wakurya kuwa ni wakatili lakini nawapongeza wakurya kwa hili
Wakurya ni kabila ambalo watu wake hawawezi kuulizana DNA ya watoto tofauti na makabila mengine
Mwanaume wa kikurya hana muda wa kuchunguza mtoto kazaliwa na nani au ana fanana na nani,yeye huamini kitanda hakizai haramu
Mwanaume wa kikurya anaweza kuoa mwanamke aliye na watoto zaidi ya wanne na akawatunza kama wanae na akawabadilisha majina wakaitwa majina ya ukoo wake,na ukoo ukawatambua hao watoto kama ndugu zao,na watoto waliokuja na mama watapewa urdhi,kuhudumiwa kama vile matibabu,elimu, na kuozwa au kuoa kwa gharama za mwanaume bila ubaguzi wowote
Ndio maana ni nadra sana kukuta watoto wa kikurya ni mahouse girl, au watoto wa mitaani, wakurya wanadhamini watu wao sana.
Wakurya huwa wanadhamini sana watoto,awe amemzaa,au hajamzaa,ila anahesabika ni mtoto wake
Ndio maana siku hizi wanawake wa makabila mengine wanatamani waolewe na wakurya,maana wamechoka watoto wao kuchunguzwa mara kwa mara wazaliwapo na wanaume waliozaa nao
Nimeshuhudia wanawake wawili wenye asili ya mkoa wa Tabora,wakitafuta waolewe na mwanaume wa kikurya kisa hawana complication kwenye ndoa zao
Kama wewe ni mwanamke una mtoto unasita kuolewa kisa mwanao ataenda kunyanyasika,tafuta mkurya,mwanao ataishi vizuri sana,na atahudumiwa kama watoto wengine
Wakurya ni kabila ambalo watu wake hawawezi kuulizana DNA ya watoto tofauti na makabila mengine
Mwanaume wa kikurya hana muda wa kuchunguza mtoto kazaliwa na nani au ana fanana na nani,yeye huamini kitanda hakizai haramu
Mwanaume wa kikurya anaweza kuoa mwanamke aliye na watoto zaidi ya wanne na akawatunza kama wanae na akawabadilisha majina wakaitwa majina ya ukoo wake,na ukoo ukawatambua hao watoto kama ndugu zao,na watoto waliokuja na mama watapewa urdhi,kuhudumiwa kama vile matibabu,elimu, na kuozwa au kuoa kwa gharama za mwanaume bila ubaguzi wowote
Ndio maana ni nadra sana kukuta watoto wa kikurya ni mahouse girl, au watoto wa mitaani, wakurya wanadhamini watu wao sana.
Wakurya huwa wanadhamini sana watoto,awe amemzaa,au hajamzaa,ila anahesabika ni mtoto wake
Ndio maana siku hizi wanawake wa makabila mengine wanatamani waolewe na wakurya,maana wamechoka watoto wao kuchunguzwa mara kwa mara wazaliwapo na wanaume waliozaa nao
Nimeshuhudia wanawake wawili wenye asili ya mkoa wa Tabora,wakitafuta waolewe na mwanaume wa kikurya kisa hawana complication kwenye ndoa zao
Kama wewe ni mwanamke una mtoto unasita kuolewa kisa mwanao ataenda kunyanyasika,tafuta mkurya,mwanao ataishi vizuri sana,na atahudumiwa kama watoto wengine
