Ndio hii ndio jumla ya maneno yote, kwamba moto umewashwa tayari huko Ulaya na kichaka kinateketea Afrika. Walitamani sana afe lakini kwa uwezo wake Jalali bado yu hai, pia baada ya kosa kosa za tyu tyu tyu nyingi, bado Mungu anampigania.
Ndio inawezekana kabisa kuwa wamemuingiza katika kundi la walemavu, lakini akili zake bado zipo timamu na hicho ndicho wanaoona mbali ndani ya nchi hii wanachojivunia kwake.
Kwani alikosa nini au kuwa mkweli na kuutoa ushauri kwa uwazi jinsi alivyo fanya ilikuwa ni nongwa?
Ukweli utabaki kuwa ukweli kuwa huyu bwana Mwenyezi Mungu amemjalia kipawa cha kipekee sana. Hebu angalia ameongea tu kidogo huko ughaibuni huku watu wote ndani ya CCM wanaweweseka. Kila mmoja anakuja na matamko yake, ooo Mara akapimwe akili, na anayesema hivyo anatambua fika kuwa hafikii hata robo ya ufahamu alionao Tundu Lissu.
Mara wengine wanadai kuwa anaichafua nchi , kwani wakati wasiojulikana wanamshambulia kwa risasi ndio walikuwa wakisafisha nchi?
Ninachofahamu mimi ni kuwa licha ya ulemavu aliopewa , lakini tunamshukuru Mungu kuwa amezihifadhi akili zake ambazo ndizo hitajio letu kubwa.
Jambo linabaki kuwa hivi, ikiwa ameunguruma akiwa nje ya nchi na CCM yote imeweweseka ni kwa vipi akirudi na kuunguruma humu ndani ya nchi?
Ndio ili upone ni lazima umeze dawa hata kama ni chungu kiasi gani. Na ndio maana nasema kuwa huyu wakili msomi bado amewafunika wote.
ASANTE MUMGU KWA KUTUPATIA MTU MUHIMU NA KWA WAKATI MUHIMU. May God bless you all.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio inawezekana kabisa kuwa wamemuingiza katika kundi la walemavu, lakini akili zake bado zipo timamu na hicho ndicho wanaoona mbali ndani ya nchi hii wanachojivunia kwake.
Kwani alikosa nini au kuwa mkweli na kuutoa ushauri kwa uwazi jinsi alivyo fanya ilikuwa ni nongwa?
Ukweli utabaki kuwa ukweli kuwa huyu bwana Mwenyezi Mungu amemjalia kipawa cha kipekee sana. Hebu angalia ameongea tu kidogo huko ughaibuni huku watu wote ndani ya CCM wanaweweseka. Kila mmoja anakuja na matamko yake, ooo Mara akapimwe akili, na anayesema hivyo anatambua fika kuwa hafikii hata robo ya ufahamu alionao Tundu Lissu.
Mara wengine wanadai kuwa anaichafua nchi , kwani wakati wasiojulikana wanamshambulia kwa risasi ndio walikuwa wakisafisha nchi?
Ninachofahamu mimi ni kuwa licha ya ulemavu aliopewa , lakini tunamshukuru Mungu kuwa amezihifadhi akili zake ambazo ndizo hitajio letu kubwa.
Jambo linabaki kuwa hivi, ikiwa ameunguruma akiwa nje ya nchi na CCM yote imeweweseka ni kwa vipi akirudi na kuunguruma humu ndani ya nchi?
Ndio ili upone ni lazima umeze dawa hata kama ni chungu kiasi gani. Na ndio maana nasema kuwa huyu wakili msomi bado amewafunika wote.
ASANTE MUMGU KWA KUTUPATIA MTU MUHIMU NA KWA WAKATI MUHIMU. May God bless you all.
Sent using Jamii Forums mobile app