rashidikurwa
Member
- Jul 16, 2017
- 34
- 26
Huyu ni mkurugenzi mtendaji wa Itv/Radio One, ni Mama shupavu, jasiri na mwenye uthubutu ambapo kwa miaka zaidi 15 amezisimamia taasisi hizi kwa kuwa na vipindi imara vyenye kuleta tija ya maendeleo katika taifa letu.
Ikumbukwe kuwa huyu ni Mama pekee anayeongoza taasisi hii ya habari ambayo imeweza kudumu katika tasnia hii kwa zaidi ya miaka 20, na kuendelea kuaminiwa na watanzania walio wengi.
Kwa taifa lolote linalohitaji kuwa na maendeleo ya kiuchumi na kisiasa linahitaji kuwa na vyombo vya habari imara kama Itv/Radio One, uwezo aliounyesha Mama huyu ni mkubwa na sitaweza kuumaliza katika ukurasa huu. Itoshe tu kusema wewe ni miongoni mwa wazalendo wa taifa letu. Hongera sana.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ikumbukwe kuwa huyu ni Mama pekee anayeongoza taasisi hii ya habari ambayo imeweza kudumu katika tasnia hii kwa zaidi ya miaka 20, na kuendelea kuaminiwa na watanzania walio wengi.
Kwa taifa lolote linalohitaji kuwa na maendeleo ya kiuchumi na kisiasa linahitaji kuwa na vyombo vya habari imara kama Itv/Radio One, uwezo aliounyesha Mama huyu ni mkubwa na sitaweza kuumaliza katika ukurasa huu. Itoshe tu kusema wewe ni miongoni mwa wazalendo wa taifa letu. Hongera sana.
Sent using Jamii Forums mobile app