Hongera Rais kwa usajili wa alama za vidole, ila tambua kwamba haupo salama!

Yaani unahofia taifa kuwapa dhamana makampuni binafsi kufanya usajili wa fingure print kwaajili ya usalama, tena mratibu mkuu wa hili zoezi ni taasisi mbili za serikali yaani NIDA na TCRA?

Unasahau ni kampuni binafsi hizo hizo zinazotoa huduma ya mawasiliano, je huoni hofu ya kiusalama kwamba labda wakiamua vujisha taarifa nyeti za watumiaji wa huduma za mawasiliano???

Labda kabla ya huu uchambuzi wako wa hofu hofu, ni vyema ungejua ni jinsi gani huu mfumo wa usajili kwa njia ya fingure print unavyofanya kazi ili uweze kufanya hiyo risk assessment vizuri tujue udhaifu na ubora wa kimfumo.

Vingenevyo hiyo ni 'fear of unknown'.

Hizo Fingerprints zinakuwa stored kwenye servers za NIDA/TCRA au Makampuni ya simu?

Kwa sasa hivi ambapo hakuna system integration, sijaona ni kwa namna gani Makampuni ya simu yatunze taarifa zote za wateja wao kwenye servers zao isipokuwa tu eti Fingerprints zikatunzwe kwingine(NIDA na TCRA) , Kutokana na hilo ni dhahiri kuwa risk ya proliferation ya hizi fingerprints ipo na hilo ni jambo ambalo halitakiwi kuchukuliwa kimchezomchezo.
 
Usichokijua ni sawa na usiku wa giza,hizo line za buku tatu tatu zilizosajiliwa majina ya watu zinatoka wapi sasa?

Sent using Jamii Forums mobile app
Uthibitisho ni upi kwamba
Hizo Fingerprints zinakuwa stored kwenye servers za NIDA/TCRA au Makampuni ya simu?

Kwa sasa hivi ambapo hakuna system integration, sijaona ni kwa namna gani Makampuni ya simu yatunze taarifa zote za wateja wao kwenye servers zao isipokuwa tu eti Fingerprints zikatunzwe kwingine(NIDA na TCRA) , Kutokana na hilo ni dhahiri kuwa risk ya proliferation ya hizi fingerprints ipo na hilo ni jambo ambalo halitakiwi kuchukuliwa kimchezomchezo.
Risk should always be very caulculated, it should be taking greatest risk at highest profit not otherwise, sasa sijajua kwamba hawakufanya feasibility study kujua risk iliyopo kwenye hili???

Tujaribu angalia kwa upande wa pili, hivi bila kusajili kwa fingure print risk ni zipi? je ni kubwa kuliko ukisajili kwa fingure print. Maana risk zipo kote kote with or without fingure print.


Yote kwa yote, tutakuwa tunapiga ramli tu kama hatutajua hiyo mifumo ya biometric registration inafanyaje kazi.
 
Lakini, tunaambiwa mtandao mmoja unakubali uwe na laini moja inayoambatana na alama zako za vidole. Zaidi inasemwa, ukisajili laini nyingine kwa alama hizo hizo za vidole, system inakukataa...!! Kwa maelezo hayo, kuna uwezekano wanaouziwa laini 3000 tzs, wanaibiwa...hizo laini zitakuwa zimesajiliwa kwa mtindo wa zamani...na muda ukifika zitazimwa maana hazitakuwa zimekidhi vigezo vya kuwa hewani.
tatizo linakuja mtu mmoja anapokuwa na access ya kusajili line za mtandao zaidi ya mmoja...mfano ww utaenda kusajili mtandao X then unataja data zako zote lakini anaingiza namba ya mtandao Y(mpya ya kwake) anayoijua yeye anaisajili...atakuuliza umepata msg?(kitu ambacho hakitawezekana sababu msg itaenda kwenye namba ya mtandao Y(anayoijua yeye) baada ya hapo anakuambia network ime-fail eb tujaribu tena ndo anakusajilia kweli na msg unapata..hapo utaondoka na line moja lakini utakuwa unesajili line mbili ingawa watakusoma na mtu ulivyo na mwingine anaweza kukuuliza una namba za mtandao upi na upi ?nadhani ili kujihakikishia usalama kidogo sajilia kwenye ofisi za mtandao husika ambapo mtu mmoja anakuwa na access ya kusajili mtandao mmoja tu.
 
Kwani, usajili wa line kwa vidole unafuta usajili wa zamani? Mfano: awali line ilisajiliwa kwa jina na kitambulisho cha ASHA JUMA. Unaweza kusajili line hiyo kwa alama za vidole kwa namba ya NIDA ya HAMIS IDD?
 
W
Ujanja ujanja kwenye usajili upo na Tatizo la Tanzania ni kuwa na kampuni nyingi za simu kuliko Taifa lolote Duniani.
[/QUOT/
Kuna watu duniani wao ni kuhisi negative kwa kila jambo. Kitambulisho kimoja hakiwezi kusajili numba zaidi ya moja kwa mtandao mmoja.
 
Mada nzuri!!
Inatakiwa baada ya zoezi kukamilika unaenda mtandao husika(customer service) Unauliza jina langu lina line ngapi za mtandao husika!! Nina wasiwasi id yangu kutumika fomoko lilizima katikati ya process!!
 
Mada nzuri!!
Inatakiwa baada ya zoezi kukamilika unaenda mtandao husika(customer service) Unauliza jina langu lina line ngapi za mtandao husika!! Nina wasiwasi id yangu kutumika fomoko lilizima katikati ya process!!
mimi nimeenda vodacom kuulizia,IMESHINDIKANA.na wao hawajui,ndio jibu nililopewa.
 
Wanacho kifanya wale ma-freelancer (wasajiri) wanakwambia weka alama za vidole kisha utaweka zaidi ya mara moja ,akijadi kukwambia mtandao unasumbua rudia tena huku akisajili linw usizo zijua,mwisho anakwambia imekubali kisha unakuwa umesajiri line yako na zawengine kwa taarifa zako

Sent using Jamii Forums mobile app
Hiki kitu kimeshanikuta exactly unavosimulia ni kwa bahati nzuri wakati nasajili ilikuwa matumizi ya alama za vidole hayajaanza kufanya kazi. Wakati huo ilikuwa kitambulisho na picha yako unayopigwa muda huo huo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Private investigator, Nachofahamu mtu haruhusiwi kuwa na laini zaidi ya moja kwa mtandao mmoja bila kuwepo kwa maombi maalumu ya barua. Kuomba kumiliki laini 2 au zaidi kutoka mitandao mmoja. Unaruhusiwa kumiliki laini zaidi ya moja kutoka mitandao tofauti tu. Embu kafanye utafiti upya ndio uweke thread.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna tangazo lolote la serikali au sheria inayokataza mtu mmoja kumiliki zaidi ya laini moja? Je umeshajaribu kusajili ikakataa? Mimi nilidhani kitambulisho cha Taifa kikitumika kusajili laini moja ukitaka kusajili laini ya pili ikatae, iseme user name already exist. Kwa hiyo ina maana ili usajiri laini ya pili itabidi upate idhini ya TCRA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usichoke endelea kunipa darasa. Ikiwa mtu mwingine atapewa namba yako je line yako itaendelea kutumika? Yaani namba moja itaweza kutumiwa na watu wawili kwa wakati mmoja?
Hii haiwezekani mkuu. Nadhani kinachofanyika ni kutumia kitambulisho kimoja kusajili laini zaidi ya moja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NAOMBA NIONGEZEE KITU HAPA

Kuna Dogo lang nilimsajilia line kwa number yangu ya NIDA

Juzi kat ananiambia amesajili line ile ile kwa namba Yake ya NIDA

Namuuliza How anasema wakala wamefuta details zangu wameweka zake

Sijui mnapata picha gani hapo ??
Hiyo laini ilipaswa kufutwa na sio kusajiliwa upya kwa Id nyingine, laa sivyo mwenye kitambulisho kilichosajili laini ndio ulitakiwa kuidhinisha mabadiliko hayo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lakini, tunaambiwa mtandao mmoja unakubali uwe na laini moja inayoambatana na alama zako za vidole. Zaidi inasemwa, ukisajili laini nyingine kwa alama hizo hizo za vidole, system inakukataa...!! Kwa maelezo hayo, kuna uwezekano wanaouziwa laini 3000 tzs, wanaibiwa...hizo laini zitakuwa zimesajiliwa kwa mtindo wa zamani...na muda ukifika zitazimwa maana hazitakuwa zimekidhi vigezo vya kuwa hewani.
Mimi nimesajili laini mbili mtandao mmoja kwa alama za vidole

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mnachonishangaza nyinyi watu ni kuwekeza nguvu kubwa kwenye kukosoa badala ya kuja na namna nzuri ya kuboresha hilo zoezi.

Siasa za kipumbavu zimewaharibu sana
Mkuu unakosea sana, suala hili halina siasa hapa, suala ni TCRA wananihakikishia nini juu ya usalama wa taarifa zangu wakati wa usajili? Unajua kuwa aarifa zako zikitumiwa vibaya unaweza ukawa implicated kwenye kosa ambalo hujatenda kama masuala ya ujambazi, ugaidi n.k.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom