Hongera kaka Eddo Kumwembe

Hongera kaka Eddo Kumwembe

kwenye dunia ya ubepari wanakauli mbiu moja niliona wanafundisha hata madarasani kwenye nchi zilizobobea za ubepari kua "THERE IS NOTHING WRONG TO BE GREEDY''
 
Kuna sehemu ambayo tumekosea, tunakosea, na tunaendelea kukosea. Watanzania walio katika fani mbalimbali wamekosa ujasiri na uthubutu wa kufuata misingi ya sera ya Kibepari inavyohitaji.
Sera za kibepari (Capitalism) ingawa hazisemi wazi lakini zinamtaka mwanadamu awe mbinafsi katika maisha yake ya kila siku na awe makini katika kujijali mwenyewe kwa umakini mkubwa pamoja na Familia yake.
Ni katika Ujamaa tu ndipo ambapo mtu anaishi kwa ajili ya watu wengi waliomzunguka, pamoja na Serikali yake. Wanamichezo wetu na wasanii wamelala katika dunia ya zamani.
Wamelala katika dunia iliyowaaminisha kwamba wao ni wasanii au wanamichezo wa serikali pamoja na wananchi wake. Matokeo yake, matatizo mengi yanayowatokea katika siku za usoni wanayalaza katika mikono ya Serikali pamoja na Wananchi.
TAFAKARI

Na Katika maisha ya kila siku usifanye kosa la kutokujifunza yafuatayo, hata kama si fani yako Kielimu hakikisha kwa juhudi zako unayafahamu.
1. Neno la Mungu.
2. Uongozi (Leadership)
3. Ujasiria mali (Enterpreneurship)
4. Utunzaji fedha ( Accounts)
5. Uchumi ( Finance)
6. Pia Sheria
7. Na Tehama (Information Tech).

Kama mtu ni msanii, mwanamichezo, mfanyakazi, mfanyabiashara nk. anatakiwa ajitambue kwamba tayari yeye ni kama kampuni kwa kuwa anatengeneza pesa inayotakiwa igawanywe kwenye mafungu muhimu yanayofuata misingi ya kifedha kama ifuatavyo: Sadaka, Uwekezaji, Akiba, Matumizi Muhimu, na Matumizi Maalum ( i.e vacation , holday etc).

kwa staili hiyo kamwe mtu hawezi filisika kamwe.
 
Hii makala ya sept 2013 Ngasa kwenye ubora wake leo dec 2014 Ngassa anasubiri Sherpman aumie ndio aingie!
HONGERA EDDO.
 
hii habari kaandika mwaka jana kabla hajapata shavu la Azam, dongo ni kuwa alikuwa anajikomba.

Hivi unadhani hao Azam TV wangemuweka nani kwenye nafasi ya Edo?

na ushahidi wa kujikomba kwake uko Wapi?

irudie kusoma hiyo makala uone kama alichoongea ni porojo
 
Hivi unadhani hao Azam TV wangemuweka nani kwenye nafasi ya Edo?

na ushahidi wa kujikomba kwake uko Wapi?

irudie kusoma hiyo makala uone kama alichoongea ni porojo

baasi edo yaishe....:becky:
 
Edo ni mchambuzi na mwandishi mahiri sana....anakipaji...ametembea sehemu nyingi ameona ...anasoma sana na ni mbunifu sana...
 
Hivi ni nan aliyewalaan kna ngasa yaan unakataa ofa ya dola 5000 kwa mwez unabak yanga na kuongeza wake uswahilin...lunyamila alipata tmu ujeruman akatoroka na kuja kucheza kombe la hedex dar..lunyamila na muso walienda south na nonda shaban wakapata tmu wakarubiniwa na wapuuz wanaojiita watu wa mpra kna malinz..hans pope..kaburu..dweji n.k wakarud bongo mwezao nonda akagoma leo hii ametamba ulaya na amecheza fainali ya uefa..leo hii anajenga mahosptali kinshasa na amenunua malor 50 kama msaada ili kusafsha majiji ya kongo drc kna lunyamila wapo mbez ya kmara..ndolanga na rage walizuia kbali cha mwameja kucheza nje ksa wanataka mgao wakiwa FAT iliyoua soka letu..Mungu tuepushe na hizi laana za wachezaji na viongoz wa soka kutojtambua
 
Ata samata anatakiwa abadlke tmu kbao ulaya znamtaka I.e marsel ya ufaransa na tmu za ubelgji kla sku anatuambia et moise katumbi atak aondoke aache upuuz aende ulaya akavune ela ana mismu mitatu tu ya kung'ura
 
wabongo wengi cjui kwa nini wanakuwa na infiriority......wanapenda kuponda sana
 
Back
Top Bottom