Frey Cosseny
JF-Expert Member
- Feb 4, 2015
- 1,984
- 1,405
Kaimu Katibu mkuu wa UVCCM Taifa Ndg Shaka Hamdu Shaka (MNEC) Mapema leo hii tarehe 20 Dec ameongoza ujumbe wa viongozi mbalimbali kumtembelea mjane mama AGRIPINA ANGERO ambaye nyumba yake ilibomolewa na Tetemeko na mhe Rais kuamua kumjengea Nyumba imeshakamilika imebakisha umaliziaji tu.
Akiwa hapo kaimu Katibu mkuu alipokea salamu za Shukrani kutoka kwa Mama mjane kwenda kwa mhe Rais kwa kumjali na kuguswa na Shida za wanyonge.Kaimu katibu mkuu Shaka Hamdu Shaka pia amewaagiza UVCCM wilaya ya Karagwe ndani ya siku 3 kwenda kwenye eneo hilo kufanya Usafi ili kumsaidia mama huyo
Baada ya tukio hilo katibu mkuu Shaka alishiriki zoezi la kugawa vifaa vya ujenzi kwa familia 10 Wahanga wa Tetemeko vifaa hivyo vimetolewa na Kanisa la Anglican Dayosisi ya Kagera usharika wa Karagwe akigawa vifaa hivyo kaimu katibu mkuu amelishukuru kanisa la Anglican kwa kuendelea kuguswa na maafa ya tetemeko.
Ameziomba familia zilizopata vifaa hivyo kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa
Wakati huo huo kaimu katibu mkuu ameendelea na ziara ya kujionea utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015-2020. Kukagua shughuli za vijana na kuhamasisha uwajibikaji wa Vijana Wilaya ya Kyerwa, amepokelewa kijiji cha CHANYA
Akiwa hapo kaimu Katibu mkuu alipokea salamu za Shukrani kutoka kwa Mama mjane kwenda kwa mhe Rais kwa kumjali na kuguswa na Shida za wanyonge.Kaimu katibu mkuu Shaka Hamdu Shaka pia amewaagiza UVCCM wilaya ya Karagwe ndani ya siku 3 kwenda kwenye eneo hilo kufanya Usafi ili kumsaidia mama huyo
Baada ya tukio hilo katibu mkuu Shaka alishiriki zoezi la kugawa vifaa vya ujenzi kwa familia 10 Wahanga wa Tetemeko vifaa hivyo vimetolewa na Kanisa la Anglican Dayosisi ya Kagera usharika wa Karagwe akigawa vifaa hivyo kaimu katibu mkuu amelishukuru kanisa la Anglican kwa kuendelea kuguswa na maafa ya tetemeko.
Ameziomba familia zilizopata vifaa hivyo kuvitumia kwa malengo yaliyokusudiwa
Wakati huo huo kaimu katibu mkuu ameendelea na ziara ya kujionea utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2015-2020. Kukagua shughuli za vijana na kuhamasisha uwajibikaji wa Vijana Wilaya ya Kyerwa, amepokelewa kijiji cha CHANYA