Hoja za Matangazo kwenye jezi mpya Simba

Randy orton

JF-Expert Member
Apr 29, 2019
1,338
3,541
Sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu anayepinga uwepo wa matangazo kwenye jezi ila wengi wanaopinga wanapinga kwa hoja zifuatazo.

1. Mpangilio wa matangazo, matangazo kwenye jezi ya simba yamekaa hovyo hovyo sana, mengine mgongoni, mengine kwenye kola, mpaka yanapoteza mvuto wa jezi na sidhani kama walikosa muundo mzuri wa kuweka matangazo hayo kwa kuwa end product ni kama bango.

2. Mdhamini mmoja kujirudia mara nyingi, Kampuni moja inajirudia zaidi ya mara tano!! , Utajisikiaje ukivaa jezi ya arsenal halafu fly emrirates ipo mara 6!!

3. Mdhamini mkuu wa Simba anajulikana kuwa ni Sportpesa, kiasi anachokitoa kwaajili ya udhamini kinajulikana, huyu mdhamini mwingine anatoa shilingi ngapi ukilinganisha na idadi anayotokea kwenye jezi ya Simba.?

4. Wakati mwingine sio tu hela watu wanaangalia class, Simba imeshakuwa brand kubwa sana Tanzania, kuna vitu vidogo vidogo vinaweza kushusha hadhi ya kitu hata kama kuna hela inaingia, hivi club kubwa kama Manchester United inayomilikiwa na familia ya Glazer wanashindwa nini kutangaza jina na makampuni yao kwenye jezi, au Chelsea ya Roman Abramovich mbona hatuioni ikitangaza matangazo ya kampuni za mafuta za Roman Abramovich?

Jibu ni kwamba Roman Abramovich na Familia ya Glazer hawashindwi kujaza mitangazo kwenye hizo jezi, isitoshe wao ndio wamiliki kwa kiasi kikubwa, ila kinacholindwa ni hadhi ya hizo clubs ndio maana unawaona wadhamini kama Team Viewer wakijinafasi peke yao kama wadhamini wakuu na wadhamini wadogo wakionekana kwenye sehemu nyingine za jezi vizuri bila kuharibu haiba ya jezi

Itaendelea.
 
Mods msiunganishe huu uzi maana hamkawii.

Sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu anayepinga uwepo wa matangazo kwenye jezi , ila wengi wanaopinga wanapinga kwa hoja zifuatazo.

1. Mpangilio wa matangazo, matangazo kwenye jezi ya simba yamekaa hovyo hovyo sana, mengine mgongoni, mengine kwenye kola , mpaka yanapoteza mvuto wa jezi na sidhani kama walikosa muundo mzuri wa kuweka matangazo hayo kwa kuwa end product ni kama bango.

2. Mdhamini mmoja kujirudia mara nyingi , Kampuni moja inajirudia zaidi ya mara tano!! , Utajisikiaje ukivaa jezi ya arsenal halafu fly emrirates ipo mara 6!!

3. Mdhamini mkuu wa Simba anajulikana kuwa ni Sportpesa , kiasi anachokitoa kwaajili ya udhamini kinajulikana, huyu mdhamini mwingine anatoa shilingi ngapi ukilinganisha na idadi anayotekea kwenye jezi ya Simba.?

4. Wakati mwingine sio tu hela watu wanaangalia class, Simba imeshakuwa brand kubwa sana Tanzania, kuna vitu vidogo vidogo vinaweza kushusha hadhi ya kitu hata kama kuna hela inaingia, hivi club kubwa kama Manchester United inayomilikiwa na familia ya Glazer wanashindwa nini kutangaza jina na makampuni yao kwenye jezi, au Chelsea ya Roman Abramovich mbona hatuioni ikitangaza matangazo ya kampuni za mafuta za Roman Abramovich ?

Jibu ni kwamba Roman Abramovich na Familia ya Glazer hawashindwi kujaza mitangazo kwenye hizo jezi, isitoshe wao ndio wamiliki kwa kiasi kikubwa, ila kinacholindwa ni hadhi ya hizo clubs ndio maana unawaona wadhamini kama Team Viewer wakijinafasi peke yao kama wadhamini wakuu na wadhamini wadogo wakionekana kwenye sehemu nyingine za jezi vizuri bila kuharibu haiba ya jezi



Itaendelea.
Matangazo hata yakifunika jezi yote ni sawa cha muhimu mpunga unaingia, na kwa taarifa yako yale ya Mo yote yanalipiwa, Mo foundation inalipiwa, Mo extra inalipiwa na Mo soap pia inalipiwa. Mkuu hivi GSM analipa sh ngapi kwa kutokea kwenye jezi ya young Africans?
 
Sasa bado kuna kinywaji kinakuja kinaitwa MO Babra 😎😎😎
Screenshot_20210903-221812_Instagram.jpg
 
Matangazo hata yakifunika jezi yote ni sawa cha muhimu mpunga unaingia, na kwa taarifa yako yale ya Mo yote yanalipiwa, Mo foundation inalipiwa, Mo extra inalipiwa na Mo soap pia inalipiwa. Mkuu hivi GSM analipa sh ngapi kwa kutokea kwenye jezi ya young Africans?
Si kweli kuwa Mo foundation inalipiwa. Inaitwa Mo Simba foundation. Hii ni Taasisi ya kujitolea kwa jamii japo sijajua iko active kiasi gani, lakini kikubwa je makubaliano hayo ni kwa shilingi ngapi?
 
Matangazo hata yakifunika jezi yote ni sawa cha muhimu mpunga unaingia, na kwa taarifa yako yale ya Mo yote yanalipiwa, Mo foundation inalipiwa, Mo extra inalipiwa na Mo soap pia inalipiwa. Mkuu hivi GSM analipa sh ngapi kwa kutokea kwenye jezi ya young Africans?
Kwani hapo kuna mahali umeandika kiasi cha pesa ambazo Mo anacholipia kwenye jezi Simba kwa kuitangaza bidhaa za Mo? Anza kwanza kutaja thamani ya mkataba wa matangazo ya Mo kwenye jezi kisha ndipo uje kuuliza swali hilo kuhusu GSM.
 
Sasa mkuu unatolea mfano wa Manchester na Chelsea kulinganisha na timu za Tanzania!
Embu weka na mfano fly emirates wanawapa Chelsea kiasi gani na wao fly emirates wanapata returns kiasi gani?
Ulaya washapiga hatua kubwa sisi bado tunachechemea.
Kabla ya Mo na gsm hizi timu zilikua hoi bin taaban, bado hazina mifumo mizuri ya kujiendesha ni tegemezi mpaka maji ya kunywa ya wachezaji.
 
Matangazo hata yakifunika jezi yote ni sawa cha muhimu mpunga unaingia, na kwa taarifa yako yale ya Mo yote yanalipiwa, Mo foundation inalipiwa, Mo extra inalipiwa na Mo soap pia inalipiwa. Mkuu hivi GSM analipa sh ngapi kwa kutokea kwenye jezi ya young Africans?
Buku jero
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom