GHIBUU
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 4,432
- 3,006
Muandishi: Makaimati
Nimejaribu kusoma hoja mbali mbali katika makala hii ilioanzishwa na HMaster na nimebaini kwamba kilichomo zaidi ni dharau, kejeli na mazungumzo yasio na ukweli au yanayotokana na wazungumzaji kutojua au kuukubali ukweli kuhusu huu Muungano. Muungano huu ulikuwa ni baina ya nchi mbili huru, yaani Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika. Wakati huo, Zanzibar ilikuwa ni Mwanachama wa Jumuiya ya Madola na Umoja wa Mataifa na baadhi ya Agencies zake kama vile ILO, WHO na UNCTAD.
Wakati Nyerere alipokuja na proposal ya Muungano kwa Karume, alitumia vitisho hivyo hivyo vya kwamba Waarabu watarudi na mambo kama hayo. Hio ilitumika kwa muda mrefu na ukawa ni wimbo kwa Viongozi wa Zanzibar mpaka mara moja, Mwalimu akamwambia Marehemu Dr. Omar,
"Viongozi wetu hawana la maana kuwaeleza wananchi wao, isipokuwa Hizbu,imefanya hili na Sultani alikuwa akifanya lile na lile.Jee, jamani vijana wetu tuliokuwa nao, hivi sasa ni nani anaeijuwa Hizbu ni nani anaemjuwa Sultani? Hivi kweli hamna zaidi ya haya kuwaeleza wananchi?"
Muungano huu tangu kuanza kwake una mashaka na ndio maana kila uchao tunazungumzia kero ambazo hata viongozi wote wa pande mbili wanajua kuwa hazitakwisha. Kuna mambo kadhaa ambayo yalitakiwa kufanyika hayakufanyika kama vile kuitisha Mkutano wa Katiba na pia Muungano huu haukuridhiwa na Baraza la Mapinduzi ambalo wakati huo lilikuwa na executive na legislative powers.
Muungano huu una matatizo tangu mwanzo kufahamika. Hebu jiulizeni, nchi ilioungana na Zanzibar yaani Tanganyika iko wapi? Sisi tunajua kwamba Tanganyika ndio hio hio Tanzania kutokana na mfumo uliopo. Tatizo linalojitokeza ni kwamba kila mambo ya Muungano yanapoongezeka, mamlaka na madaraka ya Zanzibar yanapungua kiasi cha kwamba imekuwa tegemezi kwa Tanganyika, jambo lililoandaliwa kwa ufundi mkubwa. Muungano una matatizo kiasi cha kwamba hata muasisi wake aliliona hilo na aliwahi kusema,
Without any question, the manner and the implications of the union between Tanganyika and Zanzibar is the most misunderstood aspect of Tanzanias political development. It may not matter very much when foreigners get confused, but unfortunately there are many times when Tanzanians themselves appear to misunderstand"
Muungano huu umedumu kwa muda wote huu kutokana na Chama Dola cha CCM/SMZ/SMT na matumizi mabaya ya hizo nguvu za Dola.
Mbinu nyengine ni zile zilizotumika kuwagawa Wazanzibari kwa misingi ya Ukabila, Kivyama (baada ya kuja mfumo wa Vyama vingi) na Umajimbo.
Wazanzibari sasa wamelitambua hilo na wanajitahidi kumaliza tofauti zao na matokeo yake ni GNU ingawa bado wako Wahafidhina wachache wanaofaidi peke yao wanaleta tabu. Mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ni kielelezo chengine cha umoja wa Wazanzibari ambapo Mswada huo wa Sheria ulipita kwa asilimia mia moja. Kura ya Maoni kuunda GNU ni kielelezo chengine.
Kwamba maoni yaliotolewa juzi, ni maoni ya wachache, ni kujifurahisha kwenu tu lakini ukweli mnaujua kwamba Wazanzibari wa rika zote bila ya kujali itikadi zao wamedhamiria kujipapatua na ukoloni wa Tanganyika. Kama hujui, mpaka Mawaziri, Watendaji Wakuu wa Serikali akiwemo Mwanasheria Mkuu walipinga huu udhalilishaji unaofanywa na Tanganyika dhidi ya Zanzibar. Hata muasisi wa CCM ambae amewahi kushika nyadhifa mbali mbali katika Vyama vya ASP/CCM na Serikali zote mbili za SMZ/SMT, Mzee Hassan Nassor Moyo, alisema,
"Ule wakati wetu na Nyerere tlikuwa tunakubali lakini hawa vijana wa leo hwakubali, Bw. Sitta, ITS OVER".
Jee huyu mzee wenu wa CCM nae ni mlevi? Ni vizuri kujadili hoja kwa hoja na wala si kwa jazba na dharau.
Napenda kumalizia kwa kukunukulia tena maneno ya Mwalimu aliposema,
"Ikiwa watu wa Zanzibar, bila ya kuingiliwa na watu wa nje na ikiwa wana sababu zao, wakaamua kuwa Muungano umekuwa kero kwa maisha yao, na kwamba hauna maslahi na wao sitowalazimisha kubakia na Muungano huo. Muungano huu utasita pale tu NCHI shiriki itakapoamua kujitenga"
by Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
Wazanzibari wanatumia njia za kistaarabu kutaka kujipapatua katika huu "Muungano" feki na wanaona kuwa 'saa ya ukombozi ni sasa'. Kama kutakuwa na utaratibu mwengine wa kuungana basi uwe unatokana na kuheshimiana
Mwisho kabisa napenda kuwajuulisha kuwa Zanzibar itakuwepo bila Tanzania lakini Tanzania haiwezi kuwepo bila ya Zanzibar.
Isitoshe Zanzibar imekuwepo kabla ya Tanganyika (refer to the old map of Africa below) View attachment 27059
Nadhani mtanielewa.
Nimejaribu kusoma hoja mbali mbali katika makala hii ilioanzishwa na HMaster na nimebaini kwamba kilichomo zaidi ni dharau, kejeli na mazungumzo yasio na ukweli au yanayotokana na wazungumzaji kutojua au kuukubali ukweli kuhusu huu Muungano. Muungano huu ulikuwa ni baina ya nchi mbili huru, yaani Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika. Wakati huo, Zanzibar ilikuwa ni Mwanachama wa Jumuiya ya Madola na Umoja wa Mataifa na baadhi ya Agencies zake kama vile ILO, WHO na UNCTAD.
Wakati Nyerere alipokuja na proposal ya Muungano kwa Karume, alitumia vitisho hivyo hivyo vya kwamba Waarabu watarudi na mambo kama hayo. Hio ilitumika kwa muda mrefu na ukawa ni wimbo kwa Viongozi wa Zanzibar mpaka mara moja, Mwalimu akamwambia Marehemu Dr. Omar,
"Viongozi wetu hawana la maana kuwaeleza wananchi wao, isipokuwa Hizbu,imefanya hili na Sultani alikuwa akifanya lile na lile.Jee, jamani vijana wetu tuliokuwa nao, hivi sasa ni nani anaeijuwa Hizbu ni nani anaemjuwa Sultani? Hivi kweli hamna zaidi ya haya kuwaeleza wananchi?"
Muungano huu tangu kuanza kwake una mashaka na ndio maana kila uchao tunazungumzia kero ambazo hata viongozi wote wa pande mbili wanajua kuwa hazitakwisha. Kuna mambo kadhaa ambayo yalitakiwa kufanyika hayakufanyika kama vile kuitisha Mkutano wa Katiba na pia Muungano huu haukuridhiwa na Baraza la Mapinduzi ambalo wakati huo lilikuwa na executive na legislative powers.
Muungano huu una matatizo tangu mwanzo kufahamika. Hebu jiulizeni, nchi ilioungana na Zanzibar yaani Tanganyika iko wapi? Sisi tunajua kwamba Tanganyika ndio hio hio Tanzania kutokana na mfumo uliopo. Tatizo linalojitokeza ni kwamba kila mambo ya Muungano yanapoongezeka, mamlaka na madaraka ya Zanzibar yanapungua kiasi cha kwamba imekuwa tegemezi kwa Tanganyika, jambo lililoandaliwa kwa ufundi mkubwa. Muungano una matatizo kiasi cha kwamba hata muasisi wake aliliona hilo na aliwahi kusema,
Without any question, the manner and the implications of the union between Tanganyika and Zanzibar is the most misunderstood aspect of Tanzanias political development. It may not matter very much when foreigners get confused, but unfortunately there are many times when Tanzanians themselves appear to misunderstand"
Muungano huu umedumu kwa muda wote huu kutokana na Chama Dola cha CCM/SMZ/SMT na matumizi mabaya ya hizo nguvu za Dola.
Mbinu nyengine ni zile zilizotumika kuwagawa Wazanzibari kwa misingi ya Ukabila, Kivyama (baada ya kuja mfumo wa Vyama vingi) na Umajimbo.
Wazanzibari sasa wamelitambua hilo na wanajitahidi kumaliza tofauti zao na matokeo yake ni GNU ingawa bado wako Wahafidhina wachache wanaofaidi peke yao wanaleta tabu. Mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ni kielelezo chengine cha umoja wa Wazanzibari ambapo Mswada huo wa Sheria ulipita kwa asilimia mia moja. Kura ya Maoni kuunda GNU ni kielelezo chengine.
Kwamba maoni yaliotolewa juzi, ni maoni ya wachache, ni kujifurahisha kwenu tu lakini ukweli mnaujua kwamba Wazanzibari wa rika zote bila ya kujali itikadi zao wamedhamiria kujipapatua na ukoloni wa Tanganyika. Kama hujui, mpaka Mawaziri, Watendaji Wakuu wa Serikali akiwemo Mwanasheria Mkuu walipinga huu udhalilishaji unaofanywa na Tanganyika dhidi ya Zanzibar. Hata muasisi wa CCM ambae amewahi kushika nyadhifa mbali mbali katika Vyama vya ASP/CCM na Serikali zote mbili za SMZ/SMT, Mzee Hassan Nassor Moyo, alisema,
"Ule wakati wetu na Nyerere tlikuwa tunakubali lakini hawa vijana wa leo hwakubali, Bw. Sitta, ITS OVER".
Jee huyu mzee wenu wa CCM nae ni mlevi? Ni vizuri kujadili hoja kwa hoja na wala si kwa jazba na dharau.
Napenda kumalizia kwa kukunukulia tena maneno ya Mwalimu aliposema,
"Ikiwa watu wa Zanzibar, bila ya kuingiliwa na watu wa nje na ikiwa wana sababu zao, wakaamua kuwa Muungano umekuwa kero kwa maisha yao, na kwamba hauna maslahi na wao sitowalazimisha kubakia na Muungano huo. Muungano huu utasita pale tu NCHI shiriki itakapoamua kujitenga"
by Mwalimu Julius Kambarage Nyerere
Wazanzibari wanatumia njia za kistaarabu kutaka kujipapatua katika huu "Muungano" feki na wanaona kuwa 'saa ya ukombozi ni sasa'. Kama kutakuwa na utaratibu mwengine wa kuungana basi uwe unatokana na kuheshimiana
Mwisho kabisa napenda kuwajuulisha kuwa Zanzibar itakuwepo bila Tanzania lakini Tanzania haiwezi kuwepo bila ya Zanzibar.
Isitoshe Zanzibar imekuwepo kabla ya Tanganyika (refer to the old map of Africa below) View attachment 27059
Nadhani mtanielewa.