Hoja ya Msingi Watanganyika na Wazanzibari

GHIBUU

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
4,432
3,006
Muandishi: Makaimati

Nimejaribu kusoma hoja mbali mbali katika makala hii ilioanzishwa na HMaster na nimebaini kwamba kilichomo zaidi ni dharau, kejeli na mazungumzo yasio na ukweli au yanayotokana na wazungumzaji kutojua au kuukubali ukweli kuhusu huu Muungano. Muungano huu ulikuwa ni baina ya nchi mbili huru, yaani Jamhuri ya Watu wa Zanzibar na Jamhuri ya Tanganyika. Wakati huo, Zanzibar ilikuwa ni Mwanachama wa Jumuiya ya Madola na Umoja wa Mataifa na baadhi ya Agencies zake kama vile ILO, WHO na UNCTAD.


Wakati Nyerere alipokuja na proposal ya Muungano kwa Karume, alitumia vitisho hivyo hivyo vya kwamba Waarabu watarudi na mambo kama hayo. Hio ilitumika kwa muda mrefu na ukawa ni wimbo kwa Viongozi wa Zanzibar mpaka mara moja, Mwalimu akamwambia Marehemu Dr. Omar,

"Viongozi wetu hawana la maana kuwaeleza wananchi wao, isipokuwa Hizbu,imefanya hili na Sultani alikuwa akifanya lile na lile.Jee, jamani vijana wetu tuliokuwa nao, hivi sasa ni nani anaeijuwa Hizbu ni nani anaemjuwa Sultani? Hivi kweli hamna zaidi ya haya kuwaeleza wananchi?"

Muungano huu tangu kuanza kwake una mashaka na ndio maana kila uchao tunazungumzia kero ambazo hata viongozi wote wa pande mbili wanajua kuwa hazitakwisha. Kuna mambo kadhaa ambayo yalitakiwa kufanyika hayakufanyika kama vile kuitisha Mkutano wa Katiba na pia Muungano huu haukuridhiwa na Baraza la Mapinduzi ambalo wakati huo lilikuwa na executive na legislative powers.

Muungano huu una matatizo tangu mwanzo kufahamika. Hebu jiulizeni, nchi ilioungana na Zanzibar yaani Tanganyika iko wapi? Sisi tunajua kwamba Tanganyika ndio hio hio Tanzania kutokana na mfumo uliopo. Tatizo linalojitokeza ni kwamba kila mambo ya Muungano yanapoongezeka, mamlaka na madaraka ya Zanzibar yanapungua kiasi cha kwamba imekuwa tegemezi kwa Tanganyika, jambo lililoandaliwa kwa ufundi mkubwa. Muungano una matatizo kiasi cha kwamba hata muasisi wake aliliona hilo na aliwahi kusema,

”Without any question, the manner and the implications of the union between Tanganyika and Zanzibar is the most misunderstood aspect of Tanzania’s political development. It may not matter very much when foreigners get confused, but unfortunately there are many times when Tanzanians themselves appear to misunderstand"

Muungano huu umedumu kwa muda wote huu kutokana na Chama Dola cha CCM/SMZ/SMT na matumizi mabaya ya hizo nguvu za Dola.

Mbinu nyengine ni zile zilizotumika kuwagawa Wazanzibari kwa misingi ya Ukabila, Kivyama (baada ya kuja mfumo wa Vyama vingi) na Umajimbo.

Wazanzibari sasa wamelitambua hilo na wanajitahidi kumaliza tofauti zao na matokeo yake ni GNU ingawa bado wako Wahafidhina wachache wanaofaidi peke yao wanaleta tabu. Mabadiliko ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ni kielelezo chengine cha umoja wa Wazanzibari ambapo Mswada huo wa Sheria ulipita kwa asilimia mia moja. Kura ya Maoni kuunda GNU ni kielelezo chengine.

Kwamba maoni yaliotolewa juzi, ni maoni ya wachache, ni kujifurahisha kwenu tu lakini ukweli mnaujua kwamba Wazanzibari wa rika zote bila ya kujali itikadi zao wamedhamiria kujipapatua na ukoloni wa Tanganyika. Kama hujui, mpaka Mawaziri, Watendaji Wakuu wa Serikali akiwemo Mwanasheria Mkuu walipinga huu udhalilishaji unaofanywa na Tanganyika dhidi ya Zanzibar. Hata muasisi wa CCM ambae amewahi kushika nyadhifa mbali mbali katika Vyama vya ASP/CCM na Serikali zote mbili za SMZ/SMT, Mzee Hassan Nassor Moyo, alisema,

"Ule wakati wetu na Nyerere tlikuwa tunakubali lakini hawa vijana wa leo hwakubali, Bw. Sitta, ITS OVER".

Jee huyu mzee wenu wa CCM nae ni mlevi? Ni vizuri kujadili hoja kwa hoja na wala si kwa jazba na dharau.

Napenda kumalizia kwa kukunukulia tena maneno ya Mwalimu aliposema,

"Ikiwa watu wa Zanzibar, bila ya kuingiliwa na watu wa nje na ikiwa wana sababu zao, wakaamua kuwa Muungano umekuwa kero kwa maisha yao, na kwamba hauna maslahi na wao sitowalazimisha kubakia na Muungano huo. Muungano huu utasita pale tu NCHI shiriki itakapoamua kujitenga"

by Mwalimu Julius Kambarage Nyerere

Wazanzibari wanatumia njia za kistaarabu kutaka kujipapatua katika huu "Muungano" feki na wanaona kuwa 'saa ya ukombozi ni sasa'. Kama kutakuwa na utaratibu mwengine wa kuungana basi uwe unatokana na kuheshimiana

Mwisho kabisa napenda kuwajuulisha kuwa Zanzibar itakuwepo bila Tanzania lakini Tanzania haiwezi kuwepo bila ya Zanzibar.

Isitoshe Zanzibar imekuwepo kabla ya Tanganyika (refer to the old map of Africa below) MAPAFRICAL0011.jpg View attachment 27059 1963-UN-Zanzibar.jpg 208238_10150146352486176_721596175_6946057_2281263_n.jpg




Nadhani mtanielewa.
 
Nimesoma maoni yako hayo bwana makaimati,umeeleza vitu muhimu na vya kueleweka kabisa,ila ninachoshangazwa mimi kwa nini watu hawaelewi haya na hawataki kukubali matokeo,hebu tujifunzeni libya,tunisia,egypt,

Libya gadafi sasa nchi nzima ameiharibu kwa tamaa zake na ku force madaraka,sasa jee kwa faida ya nani matokeo yale ? Gadafi sio mtu mbaya sanalakini pia ana weakness zake,na kibaya zaidi yule mtu ametawala miaka mingia sana,utafikiri mfalme,hali ile wananchi walichoshwa wametaka kubadilika mfumo ule,ndio huu ambao tulio nao sisi hapa tanganyika na zanzibar.

Serikali lazima ikubali matokeo au itakuwa worst mwaka huu haumalizi,,
 
well well said mkuu, huu mtazamo wangu kwa kuwa kwa sasa sisi watanganyika tuko busy na kureform hii nchi tungepitisha kura ya maoni sasa kuvunja muungano ili kuondoa hii kero mungano tukadili na mambo mengiNE . umoja ni nguvu utengano ni udhaifu ila kama mmeungana halafu mmoja ananunukia kuna nini hapo ? mwaacheni zanzibar taoke akajifikirie atarudi tu translation is a must in any changes so wacheni ndugu zetu waende hope waturudi tu kama EAC .
 
well well said mkuu, huu mtazamo wangu kwa kuwa kwa sasa sisi watanganyika tuko busy na kureform hii nchi tungepitisha kura ya maoni sasa kuvunja muungano ili kuondoa hii kero mungano tukadili na mambo mengiNE . umoja ni nguvu utengano ni udhaifu ila kama mmeungana halafu mmoja ananunukia kuna nini hapo ? mwaacheni zanzibar taoke akajifikirie atarudi tu translation is a must in any changes so wacheni ndugu zetu waende hope waturudi tu kama EAC .

Iwapo zanzibar ilitokea na moja kwa moja kuungana na Tanganyika basi msemo wa mtu haachi asili yake unaweza ukawa lakini kama ilikuwepo miaka na miaka zaidi ya hii 47 na matokeo yake kuwa huko nyuma ilikuwa bora naona na uwe na subira tu iwapo Muungano utavunjika huenda ikawa kama unavyoota!
 
well well said mkuu, huu mtazamo wangu kwa kuwa kwa sasa sisi watanganyika tuko busy na kureform hii nchi tungepitisha kura ya maoni sasa kuvunja muungano ili kuondoa hii kero mungano tukadili na mambo mengiNE . umoja ni nguvu utengano ni udhaifu ila kama mmeungana halafu mmoja ananunukia kuna nini hapo ? mwaacheni zanzibar taoke akajifikirie atarudi tu translation is a must in any changes so wacheni ndugu zetu waende hope waturudi tu kama EAC .

Kura ya Maoni kwa ajili ya kudai haki yake?

Yaani tuulizwe kama mnataka mpewe Uhuru wenu?

Kwani vile tuliwahi sisi wananchi wa Zanzibar na Tanganyika kuulizwa kama tunataka Muungano huu?

I dont think so.
 
Binafsi nawapongeza sana wazenj kwa kuilinda nchi yao mpaka leo ipo sisi watanganyika sijui nani katuloga jamani badala ya kudai nchi yetu tanganyika tunalalama katiba mpya ya tanzania. Hatujiulizi tanzania ni nini? Hii tanzania si ndo muungano wa nchi mbili Zanzibar na Tanganyika, mbona tanganyika haipo? zenj ipo sawa, yaani imefikia mahali wazanzibar wanatushangaa mbona hatudai nchi yetu? Wameanza kutusaidia sisi kudai nchi yetu baada yakutuona mpompompo wa ajabu, wanajiuliza wao wameungana na nchi gani? mbona hawamuoni mshirika wao katika muungano?
Katika katiba mpya watanganyika tudaini nchi yetu this is the only opportunity..
 
Binafsi nawapongeza sana wazenj kwa kuilinda nchi yao mpaka leo ipo sisi watanganyika sijui nani katuloga jamani badala ya kudai nchi yetu tanganyika tunalalama katiba mpya ya tanzania. Hatujiulizi tanzania ni nini? Hii tanzania si ndo muungano wa nchi mbili Zanzibar na Tanganyika, mbona tanganyika haipo? zenj ipo sawa, yaani imefikia mahali wazanzibar wanatushangaa mbona hatudai nchi yetu? Wameanza kutusaidia sisi kudai nchi yetu baada yakutuona mpompompo wa ajabu, wanajiuliza wao wameungana na nchi gani? mbona hawamuoni mshirika wao katika muungano?
Katika katiba mpya watanganyika tudaini nchi yetu this is the only opportunity..

Tena tunawashangaa sana tu kwani kila mkikaa kuishupalia Zanzibar na Wazanzibari, ndio hawa mafisadi mnawakawiza kuondoka.

Nyinyi mnasema hamfaidiki na Muungano na sisi ni halkadhalika, tujiulize anaefaidika ni nani?

Ni kweli BLW la Zanzibar lingepitisha Azimio la kuukataa lakini jee huo ni ustaarabu wa kuvunja ndoa ya miaka 47 japokuwa ni mfu?

Daini Tanganyika na sisi tudai Zanzibar yetu, tukiwa huru, si tunaweza kuungana kwa misingi ya kuheshimiana

Hivyo mkiendelea kututukana na kututishia kuwakuza Wazanzibari huko, ndio mtavunja dhamira yetu?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom