Habari zenu enyi watu wa Mungu vs Wapenda soka JF. Uzi huu unagusa neno la Mungu na mambo ya Mpira ndio maana nimeuweka hapa jukwaa hili.
Kwa kweli nianze kwa kutafakarisha kidogo;
Hivi kama binadamu wote duniani tungekuwa hatuja wahi kuona mpira wa miguu kabisa tangu kuzaliwa kwetu, ikatokea siku ukapelekwa katika sayali ukakuta kuna mechi watu wanacheza mpira, Ungewaelewaje?”.
Yamkini pengine ungewaona kama wamechanganyikiwa kwamba mibaba mikubwa inafukuza mpira kama kuku wa kienyeji halafu, na huenda waweza hata ukaukamata na kuwaambia kinachowasumbua hiki hapa. Tulieni;
Historia ya mpira wa miguu kwa ufupi;
Hiki tunachokiita mchezo wa mpira wa miguu si kitu cha zamani kama wengine wanavyofikiria. Hebu tuangalie historia fupi ya mchezo huu ndipo nitakueleza kwa nini mpira ni dhambi.
Huko zamani kile walichokuwa wanakiita mpira hakikuwa hivyo kwa sheria tulizo nazo kwa namna ya sasa. Kitu hichi kinachoitwa mpira kilianza mwaka 1863 mwezi 10, walikuwepo watu kadhaa waliotoka katika shule kadhaa uingereza na club chache zilizokuwapo hapo, wakawa wamewakilisha vikundi 11 na ndio wakakusanyika mwezi 10,1863 na kuanza kutunga sheria za kupatana za mchezo.
Hawa ndio waliosababisha kiundwe chama cha mpira ambacho kinaitwa FA (FOOTBALL ASSOCIATION) cha England mwaka huu 1863 ambao ni mwaka wa karibuni sana Baada ya Kristo.
JE; UNATAMBUA KUWA USHABIKI WA MPIRA NI KUSHABIKIA SHETANI?
Kama tulivyoona tafakari pale mwanzo, hivi wawezaje shabikia watu kufukuza mpira na ukawa na midadi na ushabiki wa juu kabisa hadi kufikia kujinyonga endapo Timu yako imefungwa pasipo misingi ya ushetani? “ Ni rahisi sana mtu kufa kwa ushabiki wa mpira wa miguu kuliko kufa kwa kumtetea Mungu wake”,
“Ni rahisi sana kukesha unaangalia mpira au mapambano ya ngumi kuliko kukesha ukiswali/kusali katika mkesha'',
PIA "Ni rahisi sana kutoa ofa ya mpira kwa mashabiki kuliko kutoa futari mwezi mtukufu",
BIBLIA INASEMAJE?
Ili kuweza kujua vitu kama hivi, tunatakiwa tuangalie kanuni. MUNGU ameweka kanuni ambazo zinatuongoza kupata ufahamu mapenzi ya MUNGU kwa kila jambo.
Pale ambapo jambo halijatajwa moja kwa moja, kanuni hizi zinaweza zikatuongoza.
Yako maandiko kadha wa kadha ambayo yanaweza kutuongoza katika kujua mapenzi ya MUNGU katika mipira hii.
1) (WAKOLOSAI 3:17) “KILA MFANYALO KWA NENO AU KWA TENDO, FANYENI LOTE KWA JINA LA BWANA YESU NA KUMSHUKURU MUNGU BABA“Ni muhimu kuelewa ndani yetu tuliokoka kuna mafuta au tuna dhamiri ambayo inatufundisha kujua mema na mabaya (1PET2:26-27).Hata kama jambo hatujajifunza kwa undani juu ya jambo fulani,ndani yetu kutakuwepo roho mtakatifu akitufundisha kuwa hapa siyo na hapa ndiyo.
Sasa kila tunalolifanya kwa neno au kwa tendo, anasema tulifanye hayo yote kwa kufungua kwamaombi.sasa kutokan na mafuta ndani yetu JE TUNAWEZA KUFUNGUA MECHI YA MPIRA KWA KUSHUKURU BABA KWA MAOMBI? Utaona ndani yetu inakataa.
2.) (YOHANA 5:19) “MWANA HAWEZI KUTENDA NENO MWENYEWE ISIPOKUWA AMEMUONA BABA ANALITENDA”. (YOH 14:6-9) Hivyo hatuna budi kujiuliza kutokana na maisha ya YESU, JE INAWEZEKANA YESU AKAWA ANACHEZA MPIRA? YESU KASHIKA MPIRA, MARA BEKi FULANI KAMKATA MTAMA AU TIMU YA YESU IMEPIGWA MAGOLI 6-0? kama dhamiri inakataa kuwa YESU hawezi kufanya hvyo na sisi hatuwezi kufanya hvyo.Tunatenda neno ambalo YESU anaweza kulitenda.
3) Mashabiki wengi wa jambo hilo, vinara wa jambo hilo , JE NI MATAIFA? Kama wanaongoza ni mataifa, basi nyuma ya jambo hilo kuna mashetani (UFUNUO 18:2-3,23).
Mataifa yote yanapokuwa wanachukuliwa hivyo katika jambo hilo, ndio vinara, mashabiki, kwa namna hiyo hiyo uchawi unavyotajwa lazima tujue kuna roho za mashetani. Ukiona vinara au viongozi ndio waasherati au walevi, wavuta bangi. Hawa wanaotajwa washauri wa mambo ya kifundi katika timu hizo ndio wachawi wa timu.
Watakatifu wa kanisa la kwanza walilijua vema jambo hili na kutokana na jinsi walivyokuwa wakamilifu hawakushiriki katika michezo na walichukiwa na jamii iliyowazunguka kwasababu walionekana “washamba”.
Haya ni maelezo kuhusu watakatifu wa kanisa la kwanza:
” The Christians were charged with being unsocial and came to be hated and counted as enemies of societies, they were simple and modest in dress, strictly moral in their conduct and would not go to the games and feast “maneno haya yanapatikana katika biblia iitwayo THOMPSON CHAIN REFERENCE BIBLE(NIV)”
MWISHO: Misingi ya ushetani pekee ndiyo inayo ufanya ushabiki wa mpira uwe na nguvu na kushangiliwa na mataifa.
Ni rahisi sana kutoa ofa ya mpira kwa mshabiki na ukashangliwa kuliko kusaidia masikini wanaoteseka na adha ya dunia hii ukasifiwa huu mwezi mtukufu”.
Ni heri mtu Yule atoae sadaka na kufuturisha wanyonge kuliko anaetumia milioni za fedha kufadhili mpira kwa dk 90 tu .. Yamkini huenda ndiyo maana juzi ile timu ilifungwa chanzo kikawa ni hiki (washabiki kumradhi)
Mungu awaongoze msiwe na jaziba kuchangia, maana Jazba ni mizizi ya dhambi!
Karibuni..
UPDATES
Kwa wale wanakumbuka kisa cha mfalume suleimani hapo utagundua ndipo mpira siyo kusudi la Mungu;
1. Ukisoma hiki kisa vizuri utagundua kile kisa cha mfalme suleiman na taranta za dhahabu 666 na zilivyopokwa na mpinga kristo, ambapo makombe ya dunia ya mpira yanaandaliwa kwa dhahabu.
2. Ukiendelea kusoma vizuri utaona kuwa mfalme Suleimani akawa kaulaani upepo, na alisema pia pamoja na utajiri wote huu ni sawa na kujilisha upepo, hilo neno upepo, lilikuwa na maana ya bure kabisa, na baada ya hapo kilitengenezwa kitu mithili ya mpira kikajazwa upepo ili kuzihilisha u-bure huo usiofaa machoni pa Mungu... HUO UPEPO ndio unaojazwa mipira hadi leo na kukimbizwa kwa kulenga magoli.
3. Kile kitufe mithili ya mpira chenye upepo, kilichezwa kwa kulenga ktk ya milingoti miwili mithili ya magoli na kushangiliwa na kerubi akiwa ndiyo mwamuzi REFA.
4. Wanafunzi wa yesu walikuwa 12, ukiondoa yule mmoja YUDA, walibaki 11 wenye Haki. Hao 11 ndio waliofungwa nira za kristo, lakini shetani hapo Kageuza, kwa kuweka wachezaji 11 katika team ya mpira, jiulize kwanini asingeweka 15? hao kumi na moja ndiyo wanaoshindana na kufungwa kwa mchezo wa kulenga ktk ya milingoti (magoli).
5. Katika mchezo shetani ndipo alipouteka ulimwengu kwa kugeuza ahadi za Mungu.
Ukisoma bibilia Mungu kasema "Nitabariki kazi ya mkono yenu" lakini hapo shetani akageuza, wacheza mpira ndiyo wanaolipwa pesa ndefu zaidi kwa mda mfupi sana.. Maanake Hapo shetani aligeuza baraka za mikono kuwa za miguu (Agano la mapinduzi); Kama vile kule bustani ya edeni nyoka alivyogeuza.
BARIKIWA!
Kwa kweli nianze kwa kutafakarisha kidogo;
Hivi kama binadamu wote duniani tungekuwa hatuja wahi kuona mpira wa miguu kabisa tangu kuzaliwa kwetu, ikatokea siku ukapelekwa katika sayali ukakuta kuna mechi watu wanacheza mpira, Ungewaelewaje?”.
Yamkini pengine ungewaona kama wamechanganyikiwa kwamba mibaba mikubwa inafukuza mpira kama kuku wa kienyeji halafu, na huenda waweza hata ukaukamata na kuwaambia kinachowasumbua hiki hapa. Tulieni;
Historia ya mpira wa miguu kwa ufupi;
Hiki tunachokiita mchezo wa mpira wa miguu si kitu cha zamani kama wengine wanavyofikiria. Hebu tuangalie historia fupi ya mchezo huu ndipo nitakueleza kwa nini mpira ni dhambi.
Huko zamani kile walichokuwa wanakiita mpira hakikuwa hivyo kwa sheria tulizo nazo kwa namna ya sasa. Kitu hichi kinachoitwa mpira kilianza mwaka 1863 mwezi 10, walikuwepo watu kadhaa waliotoka katika shule kadhaa uingereza na club chache zilizokuwapo hapo, wakawa wamewakilisha vikundi 11 na ndio wakakusanyika mwezi 10,1863 na kuanza kutunga sheria za kupatana za mchezo.
Hawa ndio waliosababisha kiundwe chama cha mpira ambacho kinaitwa FA (FOOTBALL ASSOCIATION) cha England mwaka huu 1863 ambao ni mwaka wa karibuni sana Baada ya Kristo.
JE; UNATAMBUA KUWA USHABIKI WA MPIRA NI KUSHABIKIA SHETANI?
Kama tulivyoona tafakari pale mwanzo, hivi wawezaje shabikia watu kufukuza mpira na ukawa na midadi na ushabiki wa juu kabisa hadi kufikia kujinyonga endapo Timu yako imefungwa pasipo misingi ya ushetani? “ Ni rahisi sana mtu kufa kwa ushabiki wa mpira wa miguu kuliko kufa kwa kumtetea Mungu wake”,
“Ni rahisi sana kukesha unaangalia mpira au mapambano ya ngumi kuliko kukesha ukiswali/kusali katika mkesha'',
PIA "Ni rahisi sana kutoa ofa ya mpira kwa mashabiki kuliko kutoa futari mwezi mtukufu",
BIBLIA INASEMAJE?
Ili kuweza kujua vitu kama hivi, tunatakiwa tuangalie kanuni. MUNGU ameweka kanuni ambazo zinatuongoza kupata ufahamu mapenzi ya MUNGU kwa kila jambo.
Pale ambapo jambo halijatajwa moja kwa moja, kanuni hizi zinaweza zikatuongoza.
Yako maandiko kadha wa kadha ambayo yanaweza kutuongoza katika kujua mapenzi ya MUNGU katika mipira hii.
1) (WAKOLOSAI 3:17) “KILA MFANYALO KWA NENO AU KWA TENDO, FANYENI LOTE KWA JINA LA BWANA YESU NA KUMSHUKURU MUNGU BABA“Ni muhimu kuelewa ndani yetu tuliokoka kuna mafuta au tuna dhamiri ambayo inatufundisha kujua mema na mabaya (1PET2:26-27).Hata kama jambo hatujajifunza kwa undani juu ya jambo fulani,ndani yetu kutakuwepo roho mtakatifu akitufundisha kuwa hapa siyo na hapa ndiyo.
Sasa kila tunalolifanya kwa neno au kwa tendo, anasema tulifanye hayo yote kwa kufungua kwamaombi.sasa kutokan na mafuta ndani yetu JE TUNAWEZA KUFUNGUA MECHI YA MPIRA KWA KUSHUKURU BABA KWA MAOMBI? Utaona ndani yetu inakataa.
2.) (YOHANA 5:19) “MWANA HAWEZI KUTENDA NENO MWENYEWE ISIPOKUWA AMEMUONA BABA ANALITENDA”. (YOH 14:6-9) Hivyo hatuna budi kujiuliza kutokana na maisha ya YESU, JE INAWEZEKANA YESU AKAWA ANACHEZA MPIRA? YESU KASHIKA MPIRA, MARA BEKi FULANI KAMKATA MTAMA AU TIMU YA YESU IMEPIGWA MAGOLI 6-0? kama dhamiri inakataa kuwa YESU hawezi kufanya hvyo na sisi hatuwezi kufanya hvyo.Tunatenda neno ambalo YESU anaweza kulitenda.
3) Mashabiki wengi wa jambo hilo, vinara wa jambo hilo , JE NI MATAIFA? Kama wanaongoza ni mataifa, basi nyuma ya jambo hilo kuna mashetani (UFUNUO 18:2-3,23).
Mataifa yote yanapokuwa wanachukuliwa hivyo katika jambo hilo, ndio vinara, mashabiki, kwa namna hiyo hiyo uchawi unavyotajwa lazima tujue kuna roho za mashetani. Ukiona vinara au viongozi ndio waasherati au walevi, wavuta bangi. Hawa wanaotajwa washauri wa mambo ya kifundi katika timu hizo ndio wachawi wa timu.
Watakatifu wa kanisa la kwanza walilijua vema jambo hili na kutokana na jinsi walivyokuwa wakamilifu hawakushiriki katika michezo na walichukiwa na jamii iliyowazunguka kwasababu walionekana “washamba”.
Haya ni maelezo kuhusu watakatifu wa kanisa la kwanza:
” The Christians were charged with being unsocial and came to be hated and counted as enemies of societies, they were simple and modest in dress, strictly moral in their conduct and would not go to the games and feast “maneno haya yanapatikana katika biblia iitwayo THOMPSON CHAIN REFERENCE BIBLE(NIV)”
MWISHO: Misingi ya ushetani pekee ndiyo inayo ufanya ushabiki wa mpira uwe na nguvu na kushangiliwa na mataifa.
Ni rahisi sana kutoa ofa ya mpira kwa mshabiki na ukashangliwa kuliko kusaidia masikini wanaoteseka na adha ya dunia hii ukasifiwa huu mwezi mtukufu”.
Ni heri mtu Yule atoae sadaka na kufuturisha wanyonge kuliko anaetumia milioni za fedha kufadhili mpira kwa dk 90 tu .. Yamkini huenda ndiyo maana juzi ile timu ilifungwa chanzo kikawa ni hiki (washabiki kumradhi)
Mungu awaongoze msiwe na jaziba kuchangia, maana Jazba ni mizizi ya dhambi!
Karibuni..
UPDATES
Kwa wale wanakumbuka kisa cha mfalume suleimani hapo utagundua ndipo mpira siyo kusudi la Mungu;
1. Ukisoma hiki kisa vizuri utagundua kile kisa cha mfalme suleiman na taranta za dhahabu 666 na zilivyopokwa na mpinga kristo, ambapo makombe ya dunia ya mpira yanaandaliwa kwa dhahabu.
2. Ukiendelea kusoma vizuri utaona kuwa mfalme Suleimani akawa kaulaani upepo, na alisema pia pamoja na utajiri wote huu ni sawa na kujilisha upepo, hilo neno upepo, lilikuwa na maana ya bure kabisa, na baada ya hapo kilitengenezwa kitu mithili ya mpira kikajazwa upepo ili kuzihilisha u-bure huo usiofaa machoni pa Mungu... HUO UPEPO ndio unaojazwa mipira hadi leo na kukimbizwa kwa kulenga magoli.
3. Kile kitufe mithili ya mpira chenye upepo, kilichezwa kwa kulenga ktk ya milingoti miwili mithili ya magoli na kushangiliwa na kerubi akiwa ndiyo mwamuzi REFA.
4. Wanafunzi wa yesu walikuwa 12, ukiondoa yule mmoja YUDA, walibaki 11 wenye Haki. Hao 11 ndio waliofungwa nira za kristo, lakini shetani hapo Kageuza, kwa kuweka wachezaji 11 katika team ya mpira, jiulize kwanini asingeweka 15? hao kumi na moja ndiyo wanaoshindana na kufungwa kwa mchezo wa kulenga ktk ya milingoti (magoli).
5. Katika mchezo shetani ndipo alipouteka ulimwengu kwa kugeuza ahadi za Mungu.
Ukisoma bibilia Mungu kasema "Nitabariki kazi ya mkono yenu" lakini hapo shetani akageuza, wacheza mpira ndiyo wanaolipwa pesa ndefu zaidi kwa mda mfupi sana.. Maanake Hapo shetani aligeuza baraka za mikono kuwa za miguu (Agano la mapinduzi); Kama vile kule bustani ya edeni nyoka alivyogeuza.
BARIKIWA!