Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Wote tumeona jinsi JK alivyoanza kampeni yake kwa rafu kubwa (achilia mbali ishara ile (tafsiri utakavyo) iliyotokea Jangwani siku ya ufunguzi wa kampeni.
Rafu hizi, kama alivyoziainisha Dr Slaa jana kwa ufasaha mkubwa, zinaonyesha nini? Mimi nadhani hofu ya kushindwa uchaguzi -- katika kura ya urais ndiyo unamsukuma JK kufanya rafu, kwamba kwa kuwa vyombo vyote vya dola na vile vinavyosimamia uchaguzi viko chini yake, kwani watafanya nini?
Ni udikteta kwa tafsiri yoyote ile. CCM wamefikia mahali kwamba sasa hawajali kitu chochote wanajifanyia wanalotaka, na watu kama Dr Slaa can as well go to hell, kwani watapata haki yao wanayodai wapi? Na wapambe wake wanitikia hivyo vibwagizo.
Tukumbushane kidogo: Kitu kama hiki tulianza kukiona wakati wa kesi ya mauaji iliyokuwa ikimkabali marehemu Ditopile (Mola amweke pema).
Kule mahakamani wapambe wa Ditopile walikuwa wanasikika wakijitapa: Serikali yetu hii, kwani yenu? Hanyongwi mtu hapa, mnajisumbua bure!
Lakini iko siku Mwenyezi Munguy atarudisha haki katika nchi hii inayozidi kupotezwa na utawala wa CCM. Iko siku ..