Sesten Zakazaka
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 10,685
- 19,442
Powerful Argument !!Mtazamo wangu ni kuwa mgombea ni muhimu zaidi kuliko sera, tukiacha uchama. Ni heri uwe na mgombea mzuri, na sera si nzuri, kuliko mgombea mbaya, na sera nzuri.
Sera si msahafu. Unaweza ku add, delete au amend wakati wowote. Kwa katiba tuliyonayo, na tunavyoona, Raisi anaweza kufanya chochote, hata nje ya sera ya chama chake, bila ya kuwajibishwa.
Kwa hiyo ni muhimu mno kuwa na Raisi bora. Raisi bora anaweza kushughulika na sera zenye walakini, lakini Raisi mbovu hawezi kutekeleza sera nzuri, achilia mbali zikiwa na udhaifu.
Kwa hili nakubaliana na weweKamapeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 28 mwaka huu zimeingia wiki ya tatu huku ikiwa inajulikana sasa ushindani mkubwa upo kwa vyama vya CCM na CHADEMA.
Mwanzo wakati kampeni zinaanza kulikua na kutegeana ili kusikia mwenzako ameongea nini ili umkosoe na kumzodoa ila sasa naona kila mgombea anajipambanua kwa haiba yake mwenyewe na sera ya chama chake.
Kuna hoja iliyopo kwenye sera za CHADEMA, hoja ya kuwa na serikali za Majimbo naona imepamba moto. CHADEMA wanasema huo ndio muarubaini wa kuhakikisha Wananchi wanafaidika na rasilimali zinazopatikana katika maeneo yao na sio kila kitu kupelekwa serikali kuu kisha warudishiwe kidogo kama ruzuku. Mahali ambapo kuna mapungufu kutokana na uchache wa rasilimali serikali kuu ndio itaongeza nguvu.
CCM kupitia Mgombea wao wanapinga na kusema kwamba hiyo ni sera ya kuigawa nchi na kutaleta matabaka ya kiuchumi, kikabila na hata kidini. Ni sera ambayo msingi wake ni wakikoloni. Pia kuna maeneo ambayo hayana rasilimali za kutosha kwahiyo kuna uwezekano yakaachwa nyuma zaidi kimaendeleo na kwamba sera ya mikoa kama ilivyo sasa ndio muafaka wa kuleta maendeleo ya watu.
Bila kujali sera ya chama kipi ndio nzuri nadhani wote wanastahili pongezi kwa kuanza kuleta mijadala ya sera na hoja ili wananchi waweze kupima na kuamua. Kama kuna uwezekano wagombea wajitahidi kupunguza ukali wa maneno/lugha na hakika kampeni za mwaka huu zitakua zenye ubora (quality) kuliko nyingi zilizopita kwa sababu yanaongelewa masuala na hoja nzito.
Para ya mwisho na maneno yako ya kumalizia yanahitaji mjadala mpanaHoja kuhusu utawala wa majimbo inaongeleka na pia ni yenye mashiko. Ni hoja ambayo inaondoa mlundikano wa majukumu kutoka ktk serikali kuu, na hivyo kuweza kuiongezea ufanisi zaidi. Lakini hili la Mzee Baba kutishia watu kutowapekea maendeleo endapo hatamchagua yeye, mbunge ama diwani wa CCM ni kufilisika kisera na kimaono.
Wajibu wa raia yeyote mwema ni kulipa kodi na maduhuli yote yaliyowekwa kisheria. Na pia ni jukumu la serikali kuwapa wananchi wake wote "public services" bila ya masharti wala upendeleo kutokana na misimamo yao ya kisiasa. Na hichi ndicho hasa ni "crux of a matter" cha hitaji la kuliweka kapu la hazina karibu na wananchi zaidi ya kuhodhiwa na viongozi wasio kuwa na maadili mema.
Shahuku ya kuleta serikali ni mfanano na ile ilyoletwa na Mwl. Nyerere ya madaraka. Isipokuwa majimbo yatajiendesha kwa kuwa na mabunge yake yenyewe, yenye madaraka ya kupanga bajeti zao kutokana na mipango ya mapato na matumizi yao.
Ni jambo la kustajaabisha mno kwa kiongozi wa juu kutishia wapigakura kuwa atawanyima maendeleo kwa kuwakomoa. Yaani fedha zitokanazo na wananchi wenyewe na kwa ajili ya maendeleo yao wenyewe, anatokea mtu mmoja anayethubutu kabisa, tena hadharani kuwananga nazo! Hapana! Lazima kuna tatizo kubwa sehemu fulani, nalo si lingine bali ni utimilifu wa lile neno la kinabii;
MENE, MENE, TEKELI & PERESI