Hizi fedha zinazogawiwa na TASAF

Hizi fedha zinazogawiwa na TASAF

segela

Member
Joined
Jun 28, 2013
Posts
78
Reaction score
69
Wadau,
Kwa muda sasa serikali inagawa pesa katika vijiji na wilaya mbalimbali kwa kisingizio cha kuwapa kaya masikini hii sio rushwa kwa hizi kaya zinazoitwa masikini tunapoelekea uchaguzi wa mwaka huu?
 
mkuu hii ni rushwa ya wazi jana nimememuona mh.mary nagu akigawa pesa kwa anaoita wazee ,ukiangalia kwa makini hakuna cha wazee pale ,endapo ni strategy yake hii kuelekea uchaguzi atakuwa na kesi ya kujibu mahakamani .sioni uhalali wa kutangaza upunguzaji wa umaskini kwa kumpa mtu mama mwenye nguvu zake 60000.kwa wakati huu wa kuelekea uchaguzi kwa hili atapona endapo hatagombea ile ni rushwa ya mchana kweupe tuseme no ,yatosha sasa
 
Ukitaka kuwa na uhakika si uwende huko TASAF makao makuu ukawaulize kaahh.
Usihukumu bila kuwa na taarifa kamili.
 
Ukifanya utafiti kutoka kwa watu wengi jinsi wanavyochangia mambo ambayo yanagusa masilahi ya maisha alafu MTU anafanya mzee tena msomi inashangaza kwelikweli
 
Zingekuwa zinagawiwa kila mwezi kwa miaka yote ya kuanzishwa TASAF, tungesema siyo rushwa lakini kwa kipindi hiki, ni typical Mlungula. Tena kuna wilaya zingine wanahamasisha watu wabaki nyumbani ili wagawiwe vyandarua-HII NI HONGO kama hongo zingine.

Uhamasishaji huu mkubwa sikuuona wakati wa kujiandikisha mpaka kujitokeza kuipiga kura kwenye Chaguzi za serikali za mitaa wala kujiandikisha kwenye BVR! Iweje leo wahamasishe TASAF na VYANDARUA kiasi hiki? CCM imechokwa. Na watashangaa pamoja na yote hayo watapigwa chini kama walivyo katwa watia nia wao.
 
Kumbe ni tatizo eeh? Niliona itv habari Mary Nagu akisaidiana na watu wa Tasaf kugawa pesa kule Hanang na juzi kati Rombo. Nikajiuliza ni kwanini sasa na siyo kabla? Huo umaskini haukuwepo kabla? Hii ni rushwa dhahiri kwani kuna kura za maoni na uuchaguzi mkuu. Waliopewa washtuke na kuwanyima kura kwani wanawadhalilisha kwa vijihela vyao. Na Takukuru wamenyamaza tu kana kwamba hawaoni na kutafsiri matukio yanayonukia rushwa.
 
Wadau,
Kwa muda sasa serikali inagawa pesa katika vijiji na wilaya mbalimbali kwa kisingizio cha kuwapa kaya masikini hii sio rushwa kwa hizi kaya zinazoitwa masikini tunapoelekea uchaguzi wa mwaka huu?
ni uelewa wako mdogo tu. hilo zoezi mbona lipo kitambo sana. tatizo lenu mnakurupuka tu. kwa nini msiulize kwanza kuliko kukimbilia kulaumu? tumieni akili, sio kila kitu kupinga tu.
 
Wadau,
Kwa muda sasa serikali inagawa pesa katika vijiji na wilaya mbalimbali kwa kisingizio cha kuwapa kaya masikini hii sio rushwa kwa hizi kaya zinazoitwa masikini tunapoelekea uchaguzi wa mwaka huu?

ukisikia kufilisika kisiasa ndio huku, serikali kuwasaidia wananchi wake mnaita rushwa, halafu huu mpango wa tsafu haukuanza leo wala jana uliasisiwa na mzee Mkapa,

cha ajabu ni kwamba wabunge wengi wkiwemo w upinzani walitaka hivi fedha ziongezwe leo mnaita rushwa.
 
Na upinzani pia wanapewa pesa za kugawa kutoka TASAF au ni kwa CCM peke yao?
 
Alafu wameanza na sehemu zenye upinzan wakati maeneo mengine kama morogoro bado hakuna chochote wakati ndo walikua wakwanza kufanya utambuzi wa kaya maskini.
 
Na wewe kachukue halafu kura kipe chama chako tuondolee post zenye ulemavu wa mawazo humu
 
Kweli mwenye nacho hamjui asiye nacho. Tunaiona 60,000 ndogo??? Tunashangaa TASAF kutoa fedha kwa kaya maskini?? JF is no longer more kwa watoa hoja popoma wa namna hii. Umezaliwa Dar hata umaskini wa Watanzania walioko Vijijin naamin huujui. Kaa kimia kuliko kutumia vidole vyako kubofya kismat phon chako cha kichina dorooooooobo wewe.
 
sio rushwa hilo zoezi lipo muda mrefu na pia sio kila mtu anapewa hizo fedha kuna mkakati maalumu ulipangwa ni mpango wa kunusuru kaya maskini. tasaf (iii) kuna kamati zake kwenye ngazi ya kijiji pia wale waliopitishwa kwenye mikutano mikuu ya kijiji kweli wanaostahili kupewa fedha za kunusuru kaya maskini.....vigezo zinawasaidia kwenye miradi midogomidogo na wanaopokea fedha hizo kuna masharti yake afya,elimu na kujiendeleza kiuchumi kama kununulia kuku kufuga,ada,uniform pia na lishe kwa wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.....hata msumbiji ipo zinaitwa (antigu)....nawasilisha kwa hayo machache. kwa wasio na masharti 17000-20000 pia 24000-46000 kwa kaya kubwa na baadae kutakua na miradi ya kimaendeleo wenye kaya watachagua nguvu kazi atakayewasilisha kwenye shughuli za miradi ya kimaendeleo ujira ule utakaopatikanika utaendelea kusaidia kaya ile kiuchumi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom