Vox Populi Vox Dei
Member
- Jun 30, 2013
- 21
- 14
Ikumbukwe kuwa viongozi wa ngazi za juu wa CHADEMA kwa mara ya kwanza walifika wilayani Rorya katika Operation Sangara mwaka 2008 nami nikiwa mmoja kati ya wana Rorya waliojiunga na CHADEMA katika operation hiyo wilayani hapa.Baadaye viongozi wetu walionekana tena Rorya mwaka 2010 wakati wa kampeni za Urais ambapo Katibu Mkuu Dr.W.P.Slaa alifika katika miji midogo ya Shirati na Utegi tu.
Tangu 2010 hadi sasa hakuna kiongozi yeyote wa juu aliyewahi kufanya ziara ya kichama Rorya.Kufuatia hatua hiyo Rorya imeachwa kisiwani katika siasa za mageuzi nchi hii.Jambo la kusikitisha ni pale viongozi wetu wanapopata fursa ya kufika Mkoani Mara hufika katika wilaya za Musoma mjini na Bunda tu.Dr Slaa,Mhe Mbowe,Mwana wa Haki Godbless Lema,John Mnyika,Kamanda Heche na wengine tunawaambia kuwa huku pia kuna watanzania waliochoka,tunawahitaji..njooni mseme neno nasi,nasi tutasikia kwani tuko tayari! Kama kuna mahala wana rorya tuliikosea CHADEMA,nasi ni binadamu kama mlivyo ninyi,nasi tunafanya makosa.Njooni Rorya!
Tangu 2010 hadi sasa hakuna kiongozi yeyote wa juu aliyewahi kufanya ziara ya kichama Rorya.Kufuatia hatua hiyo Rorya imeachwa kisiwani katika siasa za mageuzi nchi hii.Jambo la kusikitisha ni pale viongozi wetu wanapopata fursa ya kufika Mkoani Mara hufika katika wilaya za Musoma mjini na Bunda tu.Dr Slaa,Mhe Mbowe,Mwana wa Haki Godbless Lema,John Mnyika,Kamanda Heche na wengine tunawaambia kuwa huku pia kuna watanzania waliochoka,tunawahitaji..njooni mseme neno nasi,nasi tutasikia kwani tuko tayari! Kama kuna mahala wana rorya tuliikosea CHADEMA,nasi ni binadamu kama mlivyo ninyi,nasi tunafanya makosa.Njooni Rorya!