Maendeleo tu
JF-Expert Member
- Oct 9, 2010
- 347
- 107
Nimekuwa nikifuatilia ukosoaji wa wananchi kwa wenye nchi juu ya mambo mbalimbali. Ukosoaji huu umekwenda mbali mpaka kwenye matibabu ya mkuu wa nchi. Hapa imebidi niweke pozi na badala ya kubebwa na hoja za ukosoaji na wanaojitoa muhanga kutetea, imebidi nianze kujiuliza maswali hivi sisi watanzania tunaweza nini hasa tunachoweza kujivunia. Nikasafiri mpaka North Korea ambapo kuna kila aina ya vikwazo toka kwenye mataifa yenye nguvu lakini hatuingii hata chembe kwenye maendeleo yao. Nikafika Switzerland ambako hakuna mali asili yoyote lakini ndiyo mabingwa wa kutengeneza chocolate duniani wakati hata hawalimi. Kufika hapa nikakubali kubebwa na upepo wa wakosoaji wa matibabu ya Rais na kujiuliza hivi ni nchi gani zinazojitambua viongozi wao wanaumwa na wanakwenda kutibiwa nchi nyingine. Zinazofanya hivyo mara nyingi viongozi wake hawadumu sana.
Sasa najiuliza hivi sisi watanzania tunaweza nini jamani tukipigie chepuo kitutoe kama huko mbele kwa wenzetu? Hapo kale tuliwacheka wachina kwa kugeza vitu vya nchi nyingine, kupitia kugeza huko leo wanatisha duniani na tumebaki tu kusema miaka hiyo China ilikuwa sawa na Tanzania. We need visioned leaders who have mission to transform lives of Tanzanians, a leader who thinks about today and 200 years to come... Aagh naanza kupata hasira na najihisi kuanza kutoka nje ya msitari. Haya wanajamvi toeni mawazo ya kuijenga hii nchi
Sasa najiuliza hivi sisi watanzania tunaweza nini jamani tukipigie chepuo kitutoe kama huko mbele kwa wenzetu? Hapo kale tuliwacheka wachina kwa kugeza vitu vya nchi nyingine, kupitia kugeza huko leo wanatisha duniani na tumebaki tu kusema miaka hiyo China ilikuwa sawa na Tanzania. We need visioned leaders who have mission to transform lives of Tanzanians, a leader who thinks about today and 200 years to come... Aagh naanza kupata hasira na najihisi kuanza kutoka nje ya msitari. Haya wanajamvi toeni mawazo ya kuijenga hii nchi